Friday, September 24, 2010

UJUMBE TOKA KWA DR SLAA



Dk. Slaa nyumbani kwa Mbowe

Akiwa katika Jimbo la Hai, mkoani Kilimanjaro, Dk Willibrod Slaa alifanya mikutano 12 kwa siku moja. Kesho yake akafanya mikutano katika majimbo ya Rombo na Vunjo. Akahitimisha kampeni za awali mkoani humo kwa kufanya kampeni katika majimbo ya Moshi Vijijini, Moshi Mjini, Same Mashariki na Same Magharibi.

Alichokifanya mkoani Kilimanjaro kimeelezwa vema na wale waliosema “ameiteka Moshi” kwa maandamano ya watembea kwa miguu, waendesha baiskeli, pikipiki na magari; huku yakisindikizwa na helikopta katika maeneo ya Moshi Mjini. Umati wa wakazi wa Moshi, uliandamana na kusimamisha shughuli zote za kijamii na kibiashara kwa zaidi ya saa nne – kuanzia saa 8 alasiri hadi saa 12 jioni.

Ujumbe kutoka kwa Dk Slaa:

Watanzania wameshakubali kufanya mabadiliko makubwa. Rais Jakaya Kikwete ajiandae kuaga Ikulu, astaafu baada ya mika mitano ambayo haikuleta matumaini yaliyotarajiwa. Serikali isitumie mabavu kuumiza wananchi wanaotaka mabadiliko. Isimwage damu kwa ajili ya maslahi binafsi ya wanaotafuta madaraka au wanaong’ang’ania madaraka.
Rais Kikwete asiviingize vyombo vya ulinzi katika dhuluma inayoweza kusababisha damu ya Watanzania kumwagika kwa ajili ya madaraka ya wachache.

Ujumbe kutoka kwa Freeman Mbowe:

Hatuwezi kuwa na serikali inayoongozwa kwa nguvu za giza badala ya nguvu za Mungu; rais anayelindwa na majini badala ya vyombo ya ulinzi na usalama. Rais Kikwete ajitokeze, akanushe kuhusika na majini ya Sheikh Yahya Hussein, ambayo aliahidiwa kutumiwa yamlinde ili asianguke tena hadharani.

Katika picha hii, Mbowe anawaongoza wananchi wa Moshi Mjini kuzomea CCM kwa kilio huku wamejishika vichwa katika uwanja wa Mashujaa.

0 comments:

Post a Comment