Showing posts with label Habari/News. Show all posts
Showing posts with label Habari/News. Show all posts

Monday, November 22, 2010

Dk Bana: Chadema wana hoja ya msingi

Sadick Mtulya
MKUU wa Idara ya Sayansi ya Siasa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Benson Bana, amesema Chadema kina hoja ya msingi kushinikiza uundaji katiba mpya na kwamba, tatizo lipo njia wanayotumia.
Kauli ya Dk Bana inakuja ikiwa ni siku chache, baada ya wabunge wa Chadema kutoka nje ya ukumbi wa Bunge wakati Rais Jakaya Kikwete akianza kuhutubia, kuashiria kuzindua rasmi.

Chadema ilifaya hivyo ikiwa ni hatua yao kupinga matokeo ya urais yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) na kushikiza uundaji wa katiba mpya, Nec na uundaji Tume ya uchunguzi wa yaliyoajiri uchaguzi mkuu uliopita.
Kufuatia kitendo hicho, wasomi, wanasiasa, viongozi wa dini na wananchi waliibuka na maoni tofauti.
Akizungumza katika kipindi cha ‘Tuongee Siasa’ kupitia Kituo cha Televisheni cha Star Tv jana, Dk Bana alisema madai ya chama hicho yana msingi.
“Madai ya Chadema ni ya msingi, lakini tatizo ni njia waliyotumia kutozingatia utamaduni wa Watanzania katika kudai haki,’’ alisema.

Dk Bana alisema Chadema imetumia njia hasi ambayo kimantiki itajenga tabia kwa wananchi wa kada tofauti kususia vikao au mikutano itakayokuwa inaitishwa na viongozi.
“Kama njia hii itakubalika katika jamii, itafikia hatua hata wanafunzi watatoka nje ya darasa wakati mwalimu akiwa anafundisha, kwa hoja kwamba hawamtaki jambo ambalo ni kinyume na maadili ya Watanzania na hatari kwa mustakabali wa baadaye wa taifa,’’ alisema.

Kuhusu Katiba, alifafanua kwamba kulingana na mabadiliko ya wakati, Katiba ya sasa ambayo ilitungwa mwaka 1977, haikidhi haja na tija ya Watanzania inastahili kutungwa upya.

“Kulingana na wakati, inahitajika katiba mpya itakayokidhi haja na tija kwa Watanzania wote, Katiba ambayo itatoa fursa zaidi kwa wananchi kuweza kuwajibisha viongozi,” alisema na kuongeza:
“Itatoa fursa ya kujadiliwa zaidi kwa masuala ya muundo wa muungano, uteuzi wa mawaziri, uteuzi wa watendaji wakuu wa taasisi za serikali, uwepo wa tume huru ya uchaguzi, rais kupunguziwa madaraka na mambo mengine.’’

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, amenukuliwa akisema uamuzi wao ulizingiatia demokrasia na kwamba, ulipeleka ujumbe mzito kwa Watanzania na Jumuiya ya Kimataifa ili kuibua mjadala wa kitaifa juu ya umuhimu wa masuala hayo matatu.

chanzo : gazeti mwananchi

Chadema: Tuko tayari kukaa mezani na serikali

Sunday, 21 November 2010


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe

Mwandishi Wetu

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kipo tayari kukutana na serikali, chama au taasisi nyingine yoyote itakayotaka kujadiliana kuhusu hatua yao ya kutoyatambua matokeo ya uchaguzi wa urais na madai yao ya katiba mpya.

Katika tamko ambalo halijawahi kutokea kwenye siasa za Tanzania, Chadema ilitangaza kuwa haitambui matokeo ya uchaguzi wa rais kwa madai kuwa taratibu nyingi zilivurugwa kwa lengo la kumbeba mgombea wa chama tawala na ilidhihirisha msimamo wao wakati wabunge wa chama hicho walipotoka kwenye ukumbi wa Bunge mara baada ya Rais Jakaya Kikwete kuanza kuhutubia.

Lakini jana mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliiambia Mwananchi kuwa wako tayari kukaa meza moja na serikali au taasisi ambayo wataiona kuwa inaweka mbele maslahi ya taifa ili kujadiliana nayo kuhusu msimamo huo wa kwanza kuweka dhidi ya rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano. Msimamo wa Chadema umetolewa wakati mwandishi msaidizi wa rais, Premi Kibanga akikitaka chama hicho au Mbowe kufuata taratibu zilizopo iwapo wana lengo la kweli la kutaka majadiliano.

Kibanga alisema kuwa Mbowe, kama mwanasiasa na kiongozi wa kitaifa, anazifahamu taratibu na njia za kutumia iwapo anataka kukutana na serikali. Lakini mbunge huyo wa Hai alisisitiza kuwa hawangependa majadiliano yao ya serikali yachukue sura ya kisiasa kwa kuwa kufanya hivyo hakutafanikisha kufikiwa kwa lengo wanalolikusudia. “Lengo letu ni kuhakikisha kuwa tunalifikisha taifa hili mahali ambapo amani na utulivu utaendelea kuwepo.


Kati ya madai yetu yote hakuna jambo ambalo ni kwa ajili ya Chadema... tunayoyadai yatainufaisha CUF, CCM, vyama vingine vya siasa na wananchi wote,” alisema. Hata hivyo, Mbowe alionya kuwa mazungumzo hayo yasitawaliwe na aina ya maoni yanayotolewa na viongozi kadhaa wa CCM, yakiwemo ya katibu mkuu wa chama hicho tawala, Yusuf Makamba na katibu wa itikadi na uenezi, John Chiligati. “Hawa wameonekana kuzungumzia suala hili kisiasa zaidi wakati lengo letu sisi si kupiga siasa. Angalia hata mambo wanayosema eti tutaleta hoja ya kuwafukuza Chadema bungeni... hoja kama hiyo haina msingi kwa sababu hawana ubavu kisheria wa kufanya hivyo,” alisisitiza.

Alisema mazungumzo wanayoyalenga ni yale yatakayohakikisha kuwa madai yao yanafikiriwa kwa kina huku maslahi ya taifa yakiwekwa mbele. Alisema wanafurahi kuona kuwa kitendo chao cha kutoka bungeni wakati wa hotuba ya Rais Kikwete kimesaidia kuibua mjadala mzito nchini ambao iwapo utapewa nafasi ya kujadiliwa bila kuweka ushabiki wa kisiasa, nchi inaweza kupata mabadiliko makubwa siku za usoni.

Alitoa mfano wa wa watu kama waziri mkuu wa zamani, Jaji Joseph Warioba na Jaji Mkuu Augustino Ramadhani ambao walikaririwa wakisema kuwa suala la kuwa na katiba mpya ni muhimu. “Maoni kama haya, ambayo yanatoka kwa watu wazito kama hawa, yanaonyesha kuwa kitendo chetu kimeamsha mjadala wa maana kwa taifa hili,” alisema.

Alipoulizwa iwapo kitendo chao cha kutaka kukutana na serikali hakiathiri uamuzi wao wa kutotambua matokeo ya urais, alisema kuwa walishatamka tangu awali kuwa hawakatai kuwa kuna rais ingawa wanachopinga ni jinsi alivyopatikana. “Tunajua kuwa Kikwete ndiye ametangazwa kuwa rais, lakini tunachopingana nacho ni jinsi alivyoelezwa kuwa ameshinda katika uchaguzi... tunachokidai si kuwa uchaguzi urudiwe au kwamba Dk (Willibrod) Slaa atangazwe rais, la hasha. Tunalenga kuwa na mfumo bora siku za usoni ambao hautaacha shaka kwenye matokeo ya urais,” alisisitiza.


Alisema ni hatari sana kuwa na sheria ambayo hairuhusu watu kuhoji matokeo ya kura za urais katika mazingira ambamo watu wengi wanaingia kwenye kinyang’anyiro hicho. Alisema kuwa sheria ya kukataza kuhoji matokeo ya urais ilitungwa wakati wa mfumo wa chama kimoja wakati kukiwa hakuna mgombea wa kutoka vyama vya upinzani. “Wakati ule Mwalimu Nyerere ndiye kila mara alikuwa mgombea pekee, alikuwa hashindani na mtu yeyote kwa hiyo hakukuwa na mtu wa kuhoji. Wenzetu hawa wameichukua sheria hiyo na kuileta kwenye mfumo wa vyama vingi. Hauwezi kuitumia sheria hiyo hiyo wakati huu wa ushindani,” alisema.


Alisema iwapo matokeo ya uchaguzi wa ubunge na udiwani yanaweza kupingwa mahakamani, hakuna misingi ya kidemokrasia ya kukataza kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais. Alitaka serikali kuiga mfano wa Senegal ambayo ina mahakama ya katiba ambayo moja ya majukumu yake ni kusikiliza malalamiko yote kuhusiana na uchaguzi wa rais na kiongozi mpya wa nchi haapishwi hadi mahakama hiyo imethibitisha matokeo hayo. Alisema pamoja na madai ya katiba mpya, madai yao mengine ambayo wangependa yajadiliwe iwapo watakutana na serikali ni kuundwa kwa tume huru itakayochunguza matukio yote kuhusu uchaguzi wa rais.

Alisema kwa mazingira yaliyopo, tume hiyo inaweza kuundwa na Rais Kikwete lakini kwa kuwachagua watu makini ambao wanaheshimika nchini. “Watu kama hao wapo wengi tu,” alisema.

Alionya kuwa si vema tume hiyo ikachukua mrengo wa kisiasa kwani kufanya hivyo kunaweza kupotosha majadiliano. “Kuna nafasi ya Chadema au CCM kuunda tume hiyo, lakini itaonekana kuwa ni ya kichama zaidi. Pia kuna nafasi ya Bunge kuunda tume, lakini Bunge nalo lina wanasiasa ambao wana maslahi kutoka katika vyama vyao. Hii ndiyo maana tunashauri rais anaweza kuunda tume hiyo lakini kwa kuhakikisha kuwa anawateua watu ambao wanaheshimika katika jamii ambao kila mmoja anajua kuwa wanajali zaidi maslahi ya taifa,” alisema.

CHADEMA Special Seats MP from Kigoma Hon. Mhonga S. Ruhwanya with Malaysian ex PM Tun. Dr. Mahathir Mohamad

CHADEMA Special Seats MP from Kigoma Hon. Mhonga S. Ruhwanya with Malaysian ex PM Tun. Dr. Mahathir Mohamad after a discussion in his Office at Petronas Twin Towers, Kuala Lumpur.

MHE ZITTO KABWE ALIPOKUWA MALAYSIA



Kigoma North MP Hon. Zitto Kabwe with Malaysian ex PM Tun. Dr. Mahathir Mohamad after a discussion in his Office at Petronas Twin Towers, Kuala Lumpur. Zitto is in Malaysia on a one week long private visit at the invitation of Malaysian ex PM Tun. Dr. Mahathir Mohamad who was a very close friend of Mwalimu Nyerere, to learn more on the Malaysian development experience and the palm-oil industry.

After our meeting this is what Tun. Dr. Mahathir Mohamad said to ZITTO:

“Put your country at heart, don't destroy your country for political expediency or for fulfilling your ambition. Serve your country”

Saturday, November 20, 2010

WABUNGE WA CHADEMA WALIPOSUSIA HOTUBA YA JK

Wabunge wa CHADEMA wakitoka Bungeni

Chadema 'yaitikisa' nchi :NI KUTOKANA NA WABUNGE WAKE KUSUSIA HOTUBA YA JK

source : mwananchi

Na Waandishi Wetu

HATUA ya wabunge wa Chadema kutoka nje ya ukumbi wa bunge mjini Dodoma wakati Rais Jakaya Kikwete akianza kuhutubia, imetikisa nchi kutokana na wasomi, wanasiasa, viongozi wa dini na wananchi kuibuka na maoni tofauti.

Chadema wametangaza kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais wakidai kuwa kulikuwa na kasoro nyingi kwenye zoezi zima la uchaguzi na kwamba Tume ya Uchaguzi (Nec) ilikuwa imelenga kumbeba mgombea urais kutoka chama tawala.

Chadema, ambayo safari hii imeingiza watu wengi bungeni, imeamua kutumia njia hiyo ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais kushinikiza kuundwa kwa katiba mpya kutokana na katiba ya sasa kutotoa haki ya kupinga matokeo ya urais na inataka kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi.

Katika mahojiano ambayo Mwananchi iliyafanya jana katika mikoa tofauti nchini lilibaini kuwa wapo wanaoona kitendo hicho kilikuwa halali wakieleza uamuzi huo unaweka bayana msimamo wao wa kutokubaliana na mfumo uliomweka madarakani Rais Jakaya Kikwete , huku wengine wakikosoa kwa kusema kwamba hawakustahili kufanya hivyo mbele ya rais, wakitafsiri kuwa huenda hizo ni chokochoko za kuvuruga amani na utulivu nchini.

Wasomi, wanazuoni wanaounga mkono
Mhadhri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Abdallah Safari alisema kitendo hicho nio cha ni aibu kwa serikali ya Kikwete na Nec na kutaka kitafsiriwe kuwa ni kiashirio cha udhaifu katika uchaguzi na mahitaji ya tume hiyo.

“Ni silaha ya haki kwa kila mwanasiasa, ndio maana hata katika historia wabunge waliokuwa kwenye mabunge aliyokuwa akihutubia Fidel Kastro walikuwa wakitoka nje. La kujitakia halina majuto,” alisema Profesa Safari.

Mhadhiri mwingine katika Chuo hicho, Dk Azaveli Lwaitama alisema kitendo cha Chadema cha kawaida kwa kuwa siasa huambatana na suala la kisheria na hisia.

“Wao wamesema kuwa hawamtambua, lakini tayari rais wetu ameshaapishwa, hivyo kinachowafanya waseme hivyo ni hisia tu. Wanataka kuwaonyesha Watanzania kuwa hawakubaliani na matokeo ya urais, lakini kisheria hawawezi kufanya lolote kwa kuwa sheria inawabana,” alisema Dk Lwaitama.

Mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Tumaini mkoani Kilimanjaro ambaye aliomba jina lake lisitajwe gazetini alisema hakuna kosa lolote kwa wabunge kutumia njia hiyo kuonyesha dhamira yao ya kutokubaliana na matokeo ya Urais kwa kuwa hawana njia nyingine.

“Ibara ya 41 Ibara ndogo ya 7 ya katiba yetu inakataza matokeo ya urais kuchunguzwa baada ya kutangazwa na Nec… sasa kama umemfunga mshindani wako mikono, afanyeje kukuonyesha hakubaliani nawe,” alihoji.

"Katika hali ya kawaida ni jambo lisilowezekana kukubali goli ambalo unaamini limefungwa kwa mkono na kwamba hakuna mfumo unaomlazimisha mtu kumsikiliza Rais.”

Alisema haiwezekani Tanzania kujisifu kwa maendeleo ya kidemokrasia wakati katiba inazuia watu kuhoji uhalali wa matokeo ya urais, lakini katiba hiyo inaruhusu watu kuhoji uhalali wa matokeo ya wabunge na madiwani.

“Senegal kuna mahakama ya katiba ambayo inataka baada ya matokeo ya uchaguzi wa rais kutangazwa, ni lazima yathibitishwe na Mahakama ya Kikatiba… kunakuwepo kipindi maalumu cha kushughulikia malalamiko kabla ya Rais kuapishwa,” alisema.

Harod Tairo, mhadhiri wa sheria wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema kitendo cha Chadema hakikumfurahisha kwa sababu kilijenga taswira ya mgawanyiko na machafuko bungeni.

“Mimi nashauri CCM wakae chini na Chadema wazungumze tatizo lilikuwa wapi ili kuziba mianya itakayoweza kuleta machafuko kama yaliyotokea Zanzibar,” alisema Tairo na kuongeza kuwa kama serikali inataka kukuza demokrasia, ni lazima ikubali msimamo na kitendo kilichofanywa na Chadema.

Naye mhitimu wa shahada ya sheria wa Chuo Kikuu cha Tumaini, Iringa, Clement Kihoko alisema kitendo hicho ni kabisa japokuwa wanaweza kueleweka tofauti.

“Ni utaalamu wa kifalsafa na ni mambo ya kuangalia kwa umakini zaidi kwa sababu kama walivyosema awali kwamba hawamtambui Kikwete kama rais ,wangebaki kumsikiliza bungeni wangeonyesha kumuunga mkono na kumkubali,” alisema Kihoko.

Kihoko alibainisha kuwa katika tafsiri ya kifalsafa na hata falsafa ya sheria, kitendo walichokifanya chadema ni sahihi kabisa.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Morogoro (MUM), Ali Nassor alisema kitendo cha Chadema ni kuwaonyesha wananchi kwamba wako makini na wanatambua jukumu walilokabidhiwa na wananchi bungeni.
“Kwa kitendo hiki Chadema wanajiweka hadharani ili kupata wanachama wengi,” alisema Nassor.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tumaini, Dk Fairles Ilomo alielezea Chadema kuwa ni wapigania makabadiliko wachache waliojitoa kuwambwa msalabani kwa manufaa ya wananchi wengi.

Hata hivyo Dk Ilomo hakuunga mkono njia waliyotumia kupigania mabadiliko kwa kusema kuwa hawakupaswa kususia hotuba ya rais bali walipaswa kuwa wavumilivu na kutumia Bunge kufanya mabadiliko.

“Ni kitendo kilichoonyesha ujasiri kwa sababu kukiwa na viongozi ambao ni waoga watupu itachukua muda mrefu kufanya mabadiliko,” alisema Dk ILomo.

“Hayati Baba wa taifa Julias Nyerere alipoanza kupigania uhuru wakoloni walisema ni mvurugaji wa amani na kumweka rumande kwa saa kadhaa, lakini sasa tunafaidi matunda ya uhuru aliopigania. Vivyo hivyo wananchi watakuja kufaidi matunda ya mgomo Chadema."

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) walisema kitendo cha wabunge wa Chadema kinastahili kupongezwa kwa kuwa wameonyesha kwa vitendo kuwa uchaguzi ulikuwa na dosari.

Wanafunzi hao ambao wapo Jijini Tanga kwa ajili ya mazoezi walisema wabunge hao hawakutaka kuwa wanafiki mbele ya Rais Kikwete na badala yake wakaonyesha kilichokuwa mioyoni mwao.

“Walichofanya ni kupaza sauti ili dunia ielewe kwamba kulikuwa na dosari kubwa katika zoezi zima la kutangaza matokeo na hilo linaegemea kwa upande wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,” alisema Saida Hamis mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika chuo hicho.

Mawakili na Wanasheria
Mwanasheria wa Ngorongoro mkoani Arusha, Imanuel Saringe alisema: "Kisheria jambo hili halina tatizo na binafsi ninaaamini ujumbe wao umefika kwa walengwa bila vurugu au damu kumwagika."

Hata hivyo, alisema hutuba ya Rais Kikwete imekuwa ya ujumla sana na hivyo ni vigumu kuitathimini katika utekelezaji wa aliyosema.

Naye wakili mashuhuri mjini Moshi (jina limehifadhiwa) alisema kwa mtu mwenye mawazo finyu anaweza kusema kitendo cha Wabunge hao ni usanii fulani, lakini mtu upeo mpana atagundua Tanzania ina mgogoro wa kikatiba.

“Tuna tatizo la ubovu wa sheria nzima ya uchaguzi na kwa bahati nzuri sana wabunge hawa wameishia tu kutoka nje lakini tukiendelea na mfumo huu wa katiba unaokataza kuhoji matokeo ya rais, iko siku tutamwaga damu.”

Alisema: ”Tukiendelea na katiba hii tutajikuta tunakuwa na kiongozi aliyetangazwa kuwa ni rais, lakini si kiongozi aliyeshinda urais... kisheria anakuwa Ikulu, lakini kiuhalali hastahili na hapa ndipo mgogoro unapoanzia.”

Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali
Mkurugenzi mtendaji wa wanaharakati wa Agenda 2000, Moses Malaba alisema kitendo kilichofanywa na Chadema, kimefikisha ujumbe uliokusudiwa.

“Kisiasa walichofanya Chadema ni sawa; wamefanikiwa kufikisha ujumbe wa kutoridhishwa na mchakato wa uchaguzi kama walivyokusudia,” alisema Malaba lakini akaonyesha wasiwasi kama wananchi wataelewa lengo la chama hicho.

“Lakini wameenda mbali sana... wanachotaka wananchi waliowachangua ni kupata uwakilishi bungeni. Kwa sasa wanataka kujivunia kuwa na wabunge wengi.”

Mchungaji kiongozi wa Usharika wa Karanga wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Fred Njama alisema haoni kosa lolote kwa wabunge hao kufanya kitendo hicho.

“Kwa maoni yangu walichokifanya ni sahihi kwa sababu usipokubaliana na mtu huwezi kumsikiliza... ni vizuri hisia zako usizifanye ni siri ni vizuri ukazionyesha badala ya unafiki; mimi sioni tatizo hapa,” alisema.

Vyama vya siasa
Aliyekuwa mgombea urais wa TLP, Mutamwega Mugahwa alisema kitendo cha Chadema kinampasa Rais Kikwete kukaa chini na kutafakari tatizo lililopo na kulipatia ufumbuzi.

“Ningekuwa mimi ndio nimesusiwa Bunge, kiukweli nisingeweza kuchukulia kirahisi; lazima ningekaa na wahusika na kujua tatizo lililopo na kutafuta njia ya kulitatua kwa mujibu wa sheria za nchi,” alisema Mugahwa.
Alisema kwa mujibu wa katiba mtu ana uhuru wa kusikiliza na kutosikiliza ili mradi tu katika maamuzi yake asiingilie uhuru wa mtu mwingine.

Muasisi wa Chadema, Edwin Mtei alisema kitendo hicho binafsi kimempa faraja na kwamba huo ni mwendelezo wa kupinga katiba na kutaka ibadilishwe.

Mtei ambaye pia aliwahi kuwa gavana wa Benki Kuu nchini pia alimuunga mkono mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini, Jaji Amir Manento kuwa sasa ni muda wa kulilia katiba mpya.

Wananchi na makundi mengine
Mkoa wa Iringa
Baadhi ya wananchi wamewapongeza wabunge wa Chadema kwa hatua yao wakieleza kuwa msimamo huo unaweza kumfanya rais ajue kwamba wapo Watanzania wengi ambao hawana imani na utendaji kazi wa Nec.

Walisema Chadema wangeweza kuitisha maandamano na kufanya fujo kama ilivyowahi kutokea nchini Kenya, lakini kwa busara wametumia njia ya kususia hotuba kuonyesha kuwa hawamtambui rais kama alivyotamka katibu mkuu wa Chadema, Dr Willibrod Slaa.

Enock Mwasondole ambaye ni mkazi wa Mtwivila alisema umefika wakati ambao Nec inapaswa kuwa huru ili malalamiko yatokanayo na uchaguzi yapungue.

“Ni bora kususia kuliko wangeitisha mgomo na maandamano makubwa kama yaliyotokea Kenya. Rais asipuuzie hali ile badala yake anapaswa kuhakikisha Tume ya Uchaguzi inakuwa huru na kutenda haki,” alisema Mwasondole.

Mkazi mwingine wa Gangiolonga, Anania Mlelwa alisema huu ni wakati wa Tanzania kubadilisha katiba ambayo Iliandaliwa wakati wa chama kimoja na hivyo kusababisha tume hiyo kuwa mikononi mwa rais ambaye ni mwanachama wa chama kimoja.

“Katiba ndiyo tatizo kubwa; kama katiba ingelingana na wakati wa vyama vingi, tume isingekuwa ikilalamikiwa kwa kuwa isingekuwa chini ya rais,” alisema.

Naye rais wa Muungano wa Vyama vya Waandishi wa Habari, Keneth Simbaya alisema suala hilo ni la kiitikadi zaidi la kwamba wabunge hao wanapaswa kusikilizwa kwa kuwa yawezekana wana madai sahihi,

"Mara nyingi tuhuma za wanasiasa zinatakiwa kuangaliwa pande mbili kwa kuwa upande mmoja inaweza kuwa ni kweli na kwa upande wa pili inaweza kuwa si kweli, hivyo wabunge hao wasikilizwe ili kubaini wanachokilalamikia," alisema mwanahabari huyo.

Mkoa wa Mwanza
Uamuzi wa Chadema pia uliungwa mkono mkoani Mwanza ambako walisema unalenga kurejesha thamani ya kura.
Yohana Kagenzi, mkazi wa jijini Mwanza, alisema Chadema wameanzisha njia ya amani na ya kiungwana ya kudai katiba na tume huru ya uchaguzi ambayo haiwezi kusababisha umwagaji wa damu na kuzusha vurugu.

“Walisema kuwa hawayatambui matokeo, lakini serikali iliona ni jambo la kawaida nadhani njia hii sasa itamkera rais na kuamua kuwasikiliza. Kama hakuchakachua kura kwa nini asisikilize malalamiko yao,” alihoji Kagenzi.

Mkazi mwingine, Saida Mbwana alisema kitendo hicho kisipuuzwe kwa kuwa kinaweza kuwa na athari kubwa.
"Kama hawamtambua Rais Kikwete, basi hata serikali atakayoiunda hawataitambua, jambo ambalo litawakosesha maendeleo katika majimbo," alisema.

Mkoa wa Arusha
Arnold Kamde, Gervas Mgonja pamoja na Prosper Mfinanga ambao ni wakazi wa Arusha walidai ya kuwa kitendo hicho si tu kwamba kimeonyesha dalili za kukua kwa demokrasia nchini, bali pia kinatoa ujumbe kwa serikali ya Rais Kikwete kuwa Chadema hawakubaliani na matokeo ya urais kwa kuwa yalichakachuliwa.

"Sheria ya nchi inasema kuwa mara matokeo ya urais yakishatangazwa, hakuna mtu wa kuyapinga mahakamani. Sasa hiki kitendo si tu kwamba kinaonyesha kukua kwa hali ya demokrasia nchini bali pia ni ujumbe tosha kwa serikali ya Kikwete," alisema Mgonja.

Mfanyabiashara John Lyimo wa soko kuu la Arusha alipongeza wapinzani kwa kuonyesha hasira zao za kupinga matokeo na pia alimpongeza Rais Kikwete kwa kutoa hutuba nzuri.

"Mimi sina chama ila naona Chadema wamefanya vizuri tu na wamefanikiwa kufikisha ujumbe... rais aliongea vizuri na ameonyesha ameupata ujumbe," alisema Lyimo.

Mkoa wa Mbeya
Watu wengi walioongea na Mwananchi mkoani Mbeya waliunga mkono kitendo cha Chadema wakisema ujumbe waliotaka kumfikishia rais ulifika.

“Chadema wana ujumbe ambao wamewasilisha kwa serikali ya Rais Kikwete na ni haki yao kufanya hivyo,” alisema Jeremiah Osward ambaye ni mkazi wa Vwawa wilayani Mbozi.

"Kutokana na tamko lao la kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais, isingekuwa ni rahisi kwao kumsikiliza."

Mkazi wa Mwanjelwa, Zawadi Pangani alisema wabunge hao walikuwa sahihi kwa kuwa wanajua wanachokifanya ni kwa ajili ya maslahi ya wananchi na kwamba bila kufanya hivyo, haki haitaweza kupatikana.

Alisema inawezekana Chadema wana uhakika kuwa mgombea wao wa urais, Dk Slaa alishinda, lakini matokeo yakatangazwa kuwa ameshindwa, hivyo wana haki ya haki yao kufanya hivyo.

Mkoa wa Morogoro
Mmoja wa wakazi wa Morogoro, Anthony Chalamila alisema tukio hilo lilitarajiwa kwa sababu mgombea wao alitamka wazi kuwa hakubaliani na matokeo yaliyomtangaza Kikwete kuwa rais kwa madai yana walakin.

“Ni lazmima wasimamie na kuyatetea maamuzi yao, hivyo haingewezekani mtu ambaye walisema hawamtambui, wakae kumsikiliza,” alisema.

"Kama wangekubali kukaa na kumsikiliza rais akihutubia, ingeonyesha wazi kuwa hawana msimamo."
Mkazi mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Naye Simon alisema ni haki yao kufanya hivyo kwa kuwa walishatoa sababu za msingi za kutomtambua rais.

Wanaopinga kitendo cha Chadema
Wasomi na wanazuoni
Mbali na wengi kuunga mkono kitendo hicho, wapo ambao wanakipinga wakiongozwa na kiongozi wa zamani wa waasi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Profesa Ernest Wamba dia Wamba ambaye alisema si cha kiungwana.

Akizungumza katika mkutano wa wanafalsafa ulioandaliwa na Chama wa Falsafa Tanzania (Phata) uliofanyika jijini Dar es Salaam, Wamba alisema ni vizuri kama chama hicho kingekubaliana na matokeo hayo.

“Kawaida katika siasa changamoto ni jambo la kawaida, lakini kwa jinsi ulivyoniuliza kuhusu uchaguzi wa hapa Tanzania ni kweli umefanyika na mshindi kapatikana, lakini ingekuwa vizuri kama walioshindwa wangekubali tu matokeo,” alisema Profesa Wamba.

“Wabunge wameshakula kiapo, lakini wanasema hawatambui ushindi wa rais. Wana haki ya kuzungumza kwa kuwa hiyo ndio maana ya falsafa, lakini kwa hili la kiapo litawabana. Wangekubaliana na matokeo.”

Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali......

Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) limeelezea kutofurahshwa na kitendo kilichofanywa na Chadema na kukitaka kutafuta njia mbadala ya kutoa dukuduku lao.

Katibu wa TEC, Padri Antony Mkunde alisema vyama vya siasa na Watanzania kwa ujumla wanapaswa kutambua kuwa amani iliyopo haikushuka kutoka mahali popote bali ni mshikamano na busara katika uongozi.

"Mahali penye vurugu hata viongozi wa dini hawawezi kuhubiri; kinachotakiwa ni busara za viongozi wa nchi katika kuhakikisha amani na utulivu vinakuwapo," alisema Makunde.

Kwa upande wake Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania (MISATAN) imekielezea kitendo cha Chadema kuwa ni utovu wa nidhamu.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Rose Haji alisema viongozi wa Chadema ni kati ya viongozi waliokula kiapo walipoapishwa hivyo wasingepaswa kususia hotuba ya rais.

"Chadema wanatakiwa kumheshimu rais kama baba mzazi kwa sababu baba anapokosea huwezi kumdhalilisha mbele ya kadamnasi hivyo heshima inatakiwa pia katika suala la uongozi," alisema Haji.

Naye mwenyekiti wa taasisi ya kiislamu ya Imam Bukhary, Sheikh Khaliha Khamis alisema uamuzi wa Chadema utasababisha chuki dhidi ya chama hicho na wananchi waliowachagua.

Alisema kitendo hicho kinaonyesha dhahiri kuwa chama hicho hakiko tayari kukubali misingi ya demokrasia nchini na kuwatumikia wananchi.

Vyama vya siasa....

CCM imewataka wabunge wote waliokiri kutomtambua rais kujitoa haraka bungeni vinginevyo wataondolewa na azimio la bunge hadi watakapotambua uwepo wa rais.

Katibu wa kamati kuu ya CCM, John Chiligati alisema kuwa kila mbunge amekula kiapo cha kutii na kulinda katiba na kitendo cha kutomtambua rais ni uvunjaji wa katiba na hivyo wabunge hao wanatakiwa kujiondoa bungeni.

Chiligati alisema kitendo cha Chadema kuruhusu wabunge na madiwani wake kuendelea na kazi wakati hawamtambui rais na serikali ni unafiki wa hali ya juu.

Chiligati aliwataka wananchi kukataa tabia za viongozi wanaokataa matokeo kwa kuwa ni tabia inayoweza kusababisha matatizo na kuchochea vurugu nchini.

Katibu mwenezi wa NCCR-Mageuzi, David Kafulila alisema kitendo hicho hakikuwa cha kiungwana huku akikielezea kuwa ni sanaa ya maigizo.

Wananchi na makundi mengine
Mkoa wa Kagera
Aliyewahi kuwa waziri kwa nyakati tofauti katika awamu ya kwanza na pili Balozi Joseph Rwegasira amewaponda wabunge wa Chadema kwa kususia hotuba hiyo.

Mwanasiasa huyo alisema kitendo hicho kilikosa hekima kwa madai kuwa hawakujua sheria na taratibu.

Balozi Rwegasira, ambaye pia aliwahi kuwa mbunge wa Jimbo la Nkenge, alisema rais hawezi kususiwa na wabunge kwa kuwa kwa mujibu wa taratibu hata yeye ni sehemu ya Bunge na kuhoji iweje wasisusie Bunge zima.

Mkoa wa Kilimanjaro
Mwenyekiti wa Umoja wa Wafanyabiashar Wenye Viwanda na Kilimo (TCCIA) mkoani Kilimanjaro, Patrick Boisafi alisema kilichofanywa na wabunge hao wa Chadema hakikuwa cha uungwana na si mfano mzuri wa kuigwa.

“Kama hawataki kutambua matokeo yaliyompa Kikwete urais ina maana kwa miaka yote mitano hakuna siku watashiriki kutunga sheria Bungeni kwa sababu ni lazima mwisho wa siku iidhinishwe na Rais wanayemkataa,” alisema.

Alisema anachokiona ni ubinafsi wa Chadema kwamba kionekane ndicho chama kikuu cha upinzani nchini kama ilivyo CUF kwa Zanzibar ili siku za usoni wapate nafasi ya kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Bendera Isinika, ambaye mkazi wa Kaloleni anayefanya kazi ya uchoraji, alipinga kitendo cha wabunge wa Chadema kususia hotoba ya Rais Kikwete kwa madai kuwa hawakuwatendea haki wananchi waliowachagua kwa kuwa walipaswa kuwashirikisha kwanza kabla ya kufanya tukio hilo.

"Kama kuna tatizo la uchakachuaji wa kura wao walipaswa kutumia njia bora na sio kususia hotuba ya Rais Kikwete kwa kuwa wao tumewachagua sisi hivyo wangetuambia kwanza kama wanataka kutoka nje ya Bunge na si kuchukua maamuzi yao," alisema Isinika.

Mkoa wa Mbeya
Mkazi wa wilayani Mbozi, Imelda Ngarawa alisema kuwa hayo ndiyo matokeo ya upinzani kwa kuwa wanafikiri bungeni ni mahali pa kufanya sanaa, hivyo wameenda huko si kwa ajili ya kuwatetea wananchi bali kufanya sanaa.

Naye mkazi wa Tukuyu wilayani Rungwe, Fadhili Sikumoja alisema kuwa wabunge hao hawajafanya vizuri kwani rais Kikwetye bado ni rais wao kwani yupo madarakani na kwamba ilikuwa vizuri wangemsikiliza hotuba yake na kama wanahopja za msingi wangewasilisha wakati wa bunge lijalo.

Mkoa wa Morogoro
Mkazi wa Morogoro Leonard Mtete alisema kuwa hatua iliyoonyeshwa na wabunge wa chama cha Chadema haikuwa nzuri kwa vile inaweza kuwashushia umaarufu ulioanza kujijenga katika chama hicho.

Alisema kuwa hali hiyo pia inaweza kuionyesha jamii kuwa chama hicho ni chama cha washari na wagomvi tofauti na jinsi ambavyo watu walinavyokichukulia kuwa mapambano yake ni kidemokrasia na ya amani.

“Mimi nafikiri wabunge wa chadema wangetumia fursa waliyonayo bungeni kupambana kwa hoja na siyo kutoka kama walivyofanya wao” alisema mkazi huyo wa Morogoro.

Mkoa wa Iringa
Mkazi wa Iringa, Fanuel Kagambo alisema haoni kama msimamo huo unaweza kuwa na manufaa zaidi ya kuwaumiza Chadema na akawashauri kuanzisha njia nyingine ya kudai madai yao kwa vile kumkataa rais na kushiriki kupiga kura za kumthibitisha waziri mkuu aliyeteuliwa naye kuonaonyesha kumtambua.

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe anasemaje...
Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu jana, Mbowe alisema wanaowapinga au kuwa na mawazo tofauti na uamuzi huo, wasilitazame suala hilo juu juu na badala yake waangalia hoja wanazozitoa.

Alisema Chadema haikuamka tu na kutangaza kutomtambua rais, bali inazo sababu za msingi ambazo imeziweka bayana na imekuwa ikizieleza kila kukicha na kulaumu vyombo vya habari vinavyoshindwa kuainisha malalamiko au hoja zao kwa wananchi.

Mbowe alisema, msingi wa madai na malalamiko ya Chadema ni kutaka mazingira mazuri katika chaguzi zijazo wananchi wapate viongozi waliowachagua.

“Harakati ni kitu endelevu, michakato huzaa tunda la haki, miaka 19 sasa tangu siasa za vyama vingi ziruhusiwe, kumekuwa na vilio vingi toka kambi ya upinzani na kwa wananchi, lakini wenzetu walioko madarakani hawaonekani kusikia, tunatafuta lugha mbadala baada ya lugha ya upole kusikia” alisema.

Alisema, jambo wanalopigia kelele sio kilio cha Chadema pekee, bali ni kilio cha watanzania wote na akasema wanachofanya ni kutengeneza mazingira mazuri ya uchaguzi wa mwaka 2015.

“Yapo matatizo ya msingi na ni lazima yafanyike mabadiliko ya haraka na ya msingi, kwanza ni suala la katiba, tutahitaji kuangalia katiba kama chombo muhimu kinachoweza kumkomboa mtanzania na kupunguza vilio vya watu wengi” anasema.

Akizungumza kwanini wanayakubali matokeo ya wabunge na kuyakataa yale ya rais, Mbowe anasema, “Hili ni muhimu likawa wazi, sheria iko wazi kabisa, kwamba Rais akishatangazwa na Tume ya Uchaguzi hakuna anayeweza kubadilisha wala kwenda mahakamani, lakini ukiwa huridhiki na ushindi kwa wabunge au madiwani, sheria inaruhusu kwenda mahakamani kupinga” anasema.

Anasema, kutokana na sheria hizo ambazo anasema ni miongoni mwa mambo wanayoyapigia kelele wameamua kutumia njia hiyo ya kutomtambua rais ikiwa ni katika hatarakati za kutaka marekebisho katika sheria kandamizi kama hiyo ya kutokuwa na haki ya kupinga endapo wagombea wengine watakuwa hawajaridhishwa na ushindi wa mgombea mwingine.

Hata hivyo Mbowe alisema, Chadema inatambua kuwa kwa kufanya hivyo hakuwezi kubadilisha matokeo na hakuwezi kuzuia Kikwete kuwa rais au kuongoza serikali isipokuwa kwa kufanya hivyo kutafikisha ujumbe wao kwake Kikwete na serikali yake pamoja na dunia nzima.

Habari hii imeandaliwa na Joyce Mmasi, Nora Damian, Tumsifu Sanga, Fidelis Butahe, Hussein Kauli, Minael Msuya, Fredy Azzah, Michael Matemanga, Petro Tumaini, Hussein Issa, Aziza Masoud, Hidaya omary, Burhani Yakub,Tanga, Daniel Mjema, Moshi, Moses Mashalla na Mussa Juma,Arusha, Brandy Nelson, Mbeya, Tumaini Msowoya na Habel Chidawali,Iringa,Venance George, Morogoro, Phinias Bashaya,Bukoba, Geroda Mabumo na Masoud Masasi Dodoma na Frederick Katulanda, Mwanza.

Friday, November 19, 2010

Tanzania opposition says to push for electoral reform

Fri Nov 19, 2010

By Fumbuka Ng'wanakilala

DAR ES SALAAM (Reuters) - Tanzania's main opposition party said on Friday it would push for reforms of the country's electoral system after walking out of parliament during the president's speech to protest disputed elections.

The opposition said the October 31 vote was heavily rigged in favour of the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) party and want an independent electoral commission and constitutional amendments to allow presidential election results challenged in court.

President Jakaya Kikwete, who won re-election for a second and final term in office by 61 percent, delayed his speech for a few minutes on Thursday as lawmakers from Chadema party, which makes up the official opposition camp, marched out.

"The decision to walk out was made in line with our decision not to recognise results of the presidential election," Chadema's parliamentary chief whip, Tundu Lissu, told Reuters.

"We have reasons to believe that the results of the presidential vote were heavily rigged in favour of the incumbent president."

Chadema, whose presidential candidate Willibrod Slaa garnered 26 percent of the vote, said it would snub meetings officiated by the president.

Under the constitution, parliamentary and local council results can be challenged in the courts but final presidential results as announced by the National Electoral Commission cannot be challenged.

"The only legal recourse left is to register our displeasure and walk out. We know our action may not have any legal consequences, but we will not give legitimacy to the deeply flawed election process," Lissu said.

"We will hit the road and streets of Tanzania. We will explain to the people of Tanzania what happened."

ELECTORAL REFORM

Independent election observers said the electoral commission and government officials openly favoured the ruling party during the election process.

Lawmakers from the ruling CCM party, which has a two-third majority in the 335-seat parliament, heckled Chadema legislators as they walked out of parliament.

Members of parliament from other opposition parties did not join Chadema in the walk out.

One analyst said Tanzania's constitution, which was written more than three decades ago when the east African country was under one-party rule, had become obsolete.

"I think the need for a new constitution is more scaled up now than at any other time in the country's history," political commentator Deus Kibamba said in a phone interview with Reuters.

"To avoid a political crisis, the government should start the process of writing a new constitution that will take into consideration all the major changes that have occurred in Tanzania, including the introduction of multi-party politics in 1992."

In his speech on Thursday, Kikwete urged political leaders to work together to heal wounds that emerged after the election.

He outlined priorities of his government in the next five years, which include boosting economic growth, investing in agriculture, infrastructure and improving access to social services such as education, water and electricity.

He said his government would add 640 MW of electricity to the national power grid by 2015.

East Africa's second largest economy has energy demand close to 900 MW capacity, but produces less than 800 MW. Only 14 percent of its 40 million people are hooked to the grid, while demand grows by 10 to 15 percent annually.

Source: Tanzania opposition says to push for electoral reform | Top News | Reuters

UFAFANUZI ZAIDI TOKA KWA DR SLAA

Nadhani message ya Wabunge na ya kwangu iko very clear isipokuwa kwa mtu anayetaka tu kui spin au kuibadilisha kwa sababu anayoitaka mwenyewe. Naomb kurejea mambo ya msingi kwa wale ambao kwa bahati mbaya yamewapita na wana nia ya kuelewa ili spinning hii isiwabughudhi.

i) Mara baada ya uchaguzi, tarehe 3 November, 2010 Dr. Slaa alifanya Press Conference Makao Makuu ya Chadema kama Mgombea Urais ambaye hakuridhika na mchakato wa uchaguzi na Matokeo yaliyokuwa yakitolewa kupita Vituo vya TV na Jaji Lewis Makame, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Katika Press Conference hiyo Dr. Slaa alitaja dosari nzito katika mchakato wa uchaguzi na hasa katika hatua ya kujumlisha na kutangaza Taifa ambapo matokeo yaliyokuwa yakitangazwa na NEC yalitofautiana kwa kiwango kikubwa sana na yale yaliyotangazwa na Wasimamizi wa Uchaguzi (W) pale ambapo zoezi hilo lilifanyika. Nikatoa Mfano wa Geita. Pili, nilieleza kuwa Katika majimbo takriban 25 zoezi la majumlisho halikufanyika kama inavyotakiwa na sheria na hivyo matokeo kutangazwa na wasimamizi kwa utaratibu kinyume na sheria na kanuni za uchaguzi. Tatu, nilieleza kuwa katika maeneo mengine kama Kinondoni masanduku yapatayo 25 ambayo tunayo namba zake tunazo yalipatikana katika ghala la Shule ya Sekondari ya Biafra Jijini Dar-Es-Salaam ambayo hayajahesabiwa na matokeo yamekwisha kutolewa.Nne, Siku ya tarehe 28 October, Tume ya Taifa ya uchaguzi ilialika Wataalam wa IT wa vyama, na kuwa mbele ya Wataalam hao mfumo wa computer uliokuwa unatumika uli "collapse" na Tume kuwajulisha Wataalam kuwa wataita LapTop zote kutoka nchi nzima zirejeshwe Dar kwa matengenezo ya program husika. Ni kuwa wataitwa tena kujulishwa kama zimetengenezwa. Hawakuitwa tena. Hivyo mfumo wa Computer uliotumika kukusanya matokeo na upeleka Taarifa NEC unatia mashaka makubwa.Hata hivyo,baadaye tulipokea Barua kutoka NEC ya tarehe 28/10 ambayo ililetwa kwa Dispatch Makao Makuu Chadema tarehe 5 November, ikisema " Watalaam walikuwa na kukagua mfumo wa IT unaotumika na Tume na waliridhika" . Ni dhahiri barua hii inatia mashaka kwanini barua ya tarehe 8/10 iletwe kwa dispatch na ifike siku takriban 8 baadaye? Hali hii inatia mashaka kuwa barua hii imekuwa backdated kwa Tume kuficha ukweli wa Scandal kubwa iliyotokea katika mfumo ambao uligharimiwa kwa fedha nyingi na UNDP. Iwapo Tume inaweza kudanganya katika swala kama hili tutatukuwa na imani gani na Tume tena. Kutokana na dosari hizo kubwa (pamoja na mambo hayo yaliyojitokeza baadaye) Dr. Slaa, kama Mgombea aliitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi ifanye mambo yafuatayo:

i) Kusimamisha Zoezi la Kutangaza matokeo hadi uchunguzi kamili utakapokuwa umefanyika ili kuondoa hisia na tofauti zilizoanza kujitokeza. Ikumbukwe kuwa Tofauti hizi kimsingi ziligundulika na Wananchi wenyewe kutokana na Tarakimu alizosoma Jaji Makame kutofautiana na zile zilizotangazwa na Wasimamizi katika maeneo yao. Matokeo yake wananchi waliingia mitaani kupinga hali hiyo. Hayo yalitokea Geita, Shinyanga, Mbozi Mashariki na kadhaa. Matokeo yake wananchi hao waliokuwa wanadai haki zao walipigwa mabomu na polisi. Njia ya Busara ilikuwa kuitaka Tume kusitisha zoezi hili ili lisilete athari zaidi, japo hawakufanya hivyo. Chadema tulifanya jitihada za ziada kuwasihi wananchi wetu wasiingie mitaani kuepusha shari. ii) Kuitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kufuta uchaguzi na kutangaza upya marudio ya uchaguzi kwa kuwa Tofauti zilizoko ni kubwa sana, na nikatoa mfano wa Tarakimu za Geita CCM 17,792 CDM 3,789 ( Iliyotangazwa na RO Geita CCM 30,960 CDM 22031) Ni wazi kilichotokea hapa ni kuchakachua kwa lengo la kupunguza kabisa kura za Dr. Slaa, japo za JK nazo zimepunguzwa). Jimbo la Hai CCM 35,910 CDM 18,513 (Iliyotangazwa Hai na RO CCM 20,120 CDM 26,724 = Uchakachuaji uliofanyika hapa ni wa kumwongezea JK kwa zaidi ya kura 15,000 na kupunguza za Dr. Slaa kwa zaidi ya 8,000). Nilitoa pia mfano wa Ubungo ambapo kwa mujibu wa CCM 68,727 CDM 65,450(iliyotangazwa na RO CCM 70,472 CDM 72,252 hapa nako uchakachuaji ulioafanyika ni wa kupunguza kura za Dr. Slaa kwa Takriban 8,000 na kupunguza za CCM kwa kama 2000 hivi) Katika Jimbo la Bunda CCM 20,836 CDM 571 ( Iliyotangazwa na RO CCM 20,836 CDM 18,445 = Tarakimu za Bunda zimerekebishwa katika Taariffa ya mwisho ya NEC. Taarifa hii inaonyesha kuwa Dr. Slaa alipewa kura za Lipumba). Jimbo la Karatu ni kichekesho zaidi kwani kwa mujibu wa Taarifa ya awali ya NEC iliyonukuliwa na Mwananchi CCM 24,364 CDM 41 ( iliyotolewa na RO CCM 24,364 CDM 43,137. Taarifa ya mwisho ya NEC imerekebishwa kufanana na ya RO Karatu. Tume ilikiri kuwa imekosea Taarifa ya Geita japo hadi leo haijarekebisha Taarifa hiyo.Hadi leo hii tarehe 19/11 Tume haijatangaza matokeo ya Geita, Tumbe, Tunduru Kaskazini, na Vunjo kwenye Website yake. ( Tume ilikiri siku ya kujumlisha matokeo Taifa kuwa Vunjo kulikuwa na Taarifa mbili na ikaamua kutumia ile ambayo haikusainiwa na mawakala na kutumia ambayo haina saini ya mawakala. Ni akili ya kawaida tu kujua kuwa kuna jambo hapo.

Hivyo basi kutokana na Dosari hiyo kubwa mgombea yeyote anayekubali kupokea matokeo atakuwa mwendawazimu. Ndiyo maana nikakataa kutambua matokeo na kumtambua Rais aliyepatikana kwa matokeo hayo.

2:Tarehe 15 November, katika Press Conference iliyofanyika Dodoma, Dr. Slaa, alikabidhi rasmi majukumu kwa Chama kwa kuwa kazi ya Mgombea Urais imefikia mwisho wake Baada ya Rais kutangazwa kwa mujibu wa Katiba (Mbovu) ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa chombo ambacho kilikasimiwa madaraka na Kamati Kuu ya Chama ( Sekretariat) mbele ya Wabunge wa Chama. Chama kilipokea majukumu na kuelekeza utekelezaji na ufuatiliaji maazimio hayo ya kukataa matokeo na kumkataa Rais kufanyika kuanzia siku hiyo na Vyombo mbalimbali na ngazi mbalimbali za Chama, na Wabunge wa Chama. Hivyo kilichotokea Bungeni ni utekelezaji wa maamuzi ya Chama hadi pale ngazi za juu za Chama zitakapobariki au kubadilisha msimamo huo. Ni dhahiri basi, i) Wabunge wetu wala Dr. Slaa, hawakuhitaji kurudia madia ya msingi ikiwa ni pamoja na kurudia uchaguzi. Madai ya Mabadiliko ya Katiba au Katiba ya Wananchi na kudai Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kujiuzulu na Kuundwa kwa Tume ya uchunguzi ni madai yaliyotolewa katika Press Conference ya Tarehe 15/11. Hata hivyo, msisitizo wa awali ni kwa kuundwa kwa Tume ya Uchunguzi ambayo inaweza kutupelekea kwenye yote hayo. Mtu yeyote asiyemakini kufuatilia mtiririko huo anaweza kupotosha na kusababisha vurugu na uchochezi ambao Chadema, pamoja na jitihada zake za kudai haki zake na za wananchi waliochakachuliwa kura zao inapenda kufuata njia za kistaarabu na za amani. Ni vema yeyote anayetaka kufanya analysis ya hatua za Chadema kwanza akajielimisha vizuri badala ya kuweka hisia zake ( hakuna sababu ya kuandika na mate wakati wino upo), na wakati wowote Chadema tuko tayari kutoa ufafanuzi utakao hitajika, isipokuwa ule unaopaswa kupitia kwenye vyombo vyetu vya maamuzi kama chama cha kidemokrasia.

Thursday, November 18, 2010

CHADEMA kumsusa Kikwete

Mbowe akataa kuzungumzia msimamo wao

na Mwandishi wetu

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), leo kinatarajiwa kutohudhuria sherehe za kuapishwa kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, pamoja na uzinduzi wa Bunge la 10 utakaofanywa na Rais Jakaya Kikwete.

Sababu za CHADEMA kutohudhuria uzinduzi wa Bunge na kuapishwa kwa Pinda, kunatokana na msimamo wao walioutangaza wiki iliyopita kuwa hawamtambui kiongozi huyo kwa sababu matokeo yaliyompa ushindi yalichakachuliwa.

Habari ambazo zilizagaa maeneo mbalimbali mkoani hapa zilibainisha kuwa CHADEMA hawatohudhuria uzinduzi huo wa Bunge, ili kushibisha hoja yao ya kutomtambua Rais Kikwete ambaye alipata ushindi kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka huu.

Tanzania Daima, limedokezwa kuwa msimamo huo wa CHADEMA, unamaanisha kuwa chama hicho hakitahudhuria shughuli zozote ambazo Rais Kikwete atakuwa mgeni rasmi.

Msimamo kama huo uliwahi kutolewa na Chama cha Wananchi (CUF), ambacho kiliwahi kutoyatambua matokeo yaliyowaingiza madarakani waliokuwa marais wa Zanzibar, Dk. Salmin Amour na Dk. Amani Abeid Karume.

CUF ilikataa kuhudhuria mikutano ya Baraza la Wawakilishi pamoja na ile ya Bunge sambamba na kutoshiriki kwenye shughuli mbalimbali za kitaifa zilizokuwa zikiongozwa na marais hao.

Tofauti na CUF, CHADEMA imetoa msimamo wa kutomtambua Rais Kikwete, lakini kimeweka wazi kuwa wawakilishi wake wataendelea kuwatumikia wananchi kulingana na sheria na Katiba za nchi.

Tanzania Daima, lilizungumza na msemaji wa kambi ya upinzani bungeni ambaye pia ni Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, kuhusu tetesi hizo na kusema hayuko tayari kuzungumzia tetesi bali aliwataka wananchi wavute subira, ili waone kama watahudhuria au hawatohudhuria.

Alibainisha kuwa hawezi kuzuia mawazo ya watu au maneno yao, lakini ukweli utajulikana wakati ukifika kama wabunge wa CHADEMA wataingia bungeni wakati Rais Kikwete akilizindua na kulihutubia Bunge.

“Taarifa za CHADEMA kutohudhuria sherehe hizo umezipata wapi?....mimi naomba uvute subira ili kujua ukweli wa tetesi hizo, wanaozieneza wanajua walikozipata...muda utaamua,” alisema Mbowe.

Tanzania Daima, lilidokezwa na watu walio karibu na wabunge wa CHADEMA kuwa msimamo wao ni kutohudhuria sherehe hizo, kwani wakifanya hivyo ni sawa na kwenda kinyume na msimamo wao walioutoa mwanzoni mwa wiki hii wa kukataa kumtambua Rais Kikwete.

CHADEMA inadai kuwa Kikwete alipata madaraka kwa sababu ya uchakachuaji wa kura uliofanywa na Usalama wa Taifa kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ili kumuwezesha Kikwete kuibuka na ushindi.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, leo asubuhi katika viwanja vya Ikulu Ndogo ya Chamwino, anatarajia kuapishwa kushika wadhifa huo baada ya kuidhinishwa na Bunge juzi.

CHADEMA yamwadhiri Ndugai

Yamtuhumu kumbeba Sophia Simba

na Salehe Mohamed, Dodoma

NAIBU Spika wa Bunge, Job Ndugai, juzi alianza kuonja machungu ya kiti chake baada ya kukaliwa kooni na wabunge wa CHADEMA kwa madai anakipendelea Chama cha Mapinduzi (CCM).

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, na John Mnyika wa Ubungo, walipinga kitendo cha mbunge wa viti maalum kupitishwa bila kupingwa kuwakilisha Tanzania katika Bunge la nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara (SADC).

Mnyika aliomba mwongozo wa Naibu Spika kuhoji ni kanuni ipi iliyotumika kumpitisha Simba ilhali wenzake walijieleza kwa lugha ya Kiingereza na baadaye kupigiwa kura.

Alisema kanuni za uchaguzi wa wabunge wanaokwenda kwenye vyombo vingine vya uwakilishi kifungu cha 5(2)c kinasema mgombea mmoja wa nafasi inayohusika wabunge watampigia kura za ndiyo au hapana.

“Mimi napinga Sophia Simba, kutoitwa kujieleza, kuulizwa maswali na kupigiwa kura, kinyume na kanuni ametangazwa na amepita bila kupigwa,” alisema Mnyika.

Akitoa mwangozo, juu ya jambo hilo Naibu Spika Ndugai, alisema Mnyika yuko sahihi, lakini alichelewa kutoa hoja na Spika wa Bunge, Anne Makinda ndiye aliyeanza mchakato wa uchaguzi kabla ya kumuachia kiti hicho.

Jibu hilo lilimfanya Zitto na Mnyika kupinga hoja hiyo na kuzua mjadala ambao ulimfanya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Federick Werema kuingilia kati.

Werema, alisema hoja iliyotolewa na Mnyika ni sahihi lakini haitoweza kujadiliwa au kubadili utaratibu uliofanyika kwa sababu ilichelewa kutolewa.

Alisema kuwa makundi mengine yalishafanya uchaguzi huo hivyo haitokuwa rahisi kwa Sophia Simba kuitwa kujieleza, kuulizwa maswali na hatimaye kupigiwa kura.

Maelezo hayo, yalipingwa na Zitto kwa madai kuwa kanuni zimekiukwa na Bunge haliwezi kuendeshwa kwa ukiukaji kanuni au upendeleo kwa chama fulani.

Mjadala wa kupinga jambo hilo ulizidi kushika kasi na kumfanya Mbunge wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge (CCM), kusimama kutoa taarifa kwa mujibu wa kanuni ya 5 (4) inayohusu mamlaka ya Spika.

Alisema kanuni hiyo, inamtaka mbunge ambaye hataridhika na uamuzi wa Spika kuwasilisha sababu za kutoridhika kwake kwa katibu wa Bunge, ambaye atawasilisha malalamiko hayo kwa Spika.

Chenge alibainisha kuwa vifungu vidogo vya (5) na (6) vinaeleza Spika atawajibika kuitisha kikao cha Kamati ya Kanuni za Bunge na kulijulisha Bunge kuhusu uamuzi utakaotolewa na kamati.

Aliongeza kuwa Spika au Naibu wake hawatakuwa wenyeviti wa kikao hicho, ili kutoa nafasi na haki kwa shauri husika kusikilizwa.

Aliongeza kuwa majibizano kati ya kiti (Spika au Naibu Spika) na baadhi ya wabunge kutokana na uamuzi wa Spika hayana nguvu.

Zitto aliinuka na kumjibu Chenge kuwa Kamati ya Kanuni za Bunge bado haijaundwa, hivyo hawawezi kuwasilisha taarifa ya kutoridhishwa kwake.

Akizungumzia kuhusu uadilifu kwa kiongozi wa Bunge (Spika, Naibu wake au wenyeviti wa Bunge), kwa kutumia kanuni ya nane, inayozuia upendeleo, Zitto alitaka Sophia ajieleze na apigiwe kura.

Mjadala huo ulihitishwa na Naibu Spika, Job Ndugai, ambaye aliwaonya wabunge wanaotaka kucheza na mamlaka ya Spika au Naibu Spika kujirekebisha mara moja, ili kuepuka adhabu.

Mjadala huo, ulisababishwa na uchaguzi wa wajumbe wa Bunge la SADC.

Aliongeza kuwa mabishano hayo yanapaswa yachukuliwe na wabunge wapya kwa umakini mkubwa hasa kwa kusoma sheria na kanuni za kudumu za Bunge.

Pamoja na Sophia, wajumbe wengine wa Bunge la SADC-PF ni Mohammed Habib Mnyaa (Mkanyageni-CUF), ambaye baada ya kutangazwa mshindi kwa kura 275 dhidi ya kura 47 za mgombea wa CHADEMA, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa.

Mwingine ni Mbunge wa Arumeru Magharibi, Goodluck Ole Medeye (CCM) aliyepata kura 180. Waliopiga kura walikuwa wabunge 324.

Wednesday, November 17, 2010

Lissu, Mnyika wamtikisa Spika

TANZANIA DAIMA

WABUNGE machachari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu (Singida Mashariki) na John Mnyika (Ubungo), jana walianza kumpa wakati mgumu Spika wa Bunge, Anne Makinda, kwa kumbana kwenye kanuni kwa kutaka awape ufafanuzi.

Akizungumza kwa kujiamini, Mnyika alikuwa wa kwanza kutaka mwongozo wa Spika, kwa kutaja kanuni ya 68 (7) ya Bunge inayozungumzia usiri wa kura lakini katika karatasi walizotoa kwa ajili ya kupiga kura za kuidhinisha jina la waziri mkuu zilikuwa na namba.

Mnyika alisema uwepo wa namba hizo kunaweza kumfanya mtu kujua nani alipewa karatasi namba ngapi na kura aliyopiga ili kumkubali au kumkataa mtu Fulani, hivyo hakutakuwa na usiri tena.

“Mimi nimepata karatasi yenye namba 278, hivyo ni rahisi mtu kujua kura yangu nilimkataa au kumkubali mgombea, hapa siri haitakuwapo, naomba mwongozo wako,” alisema.

Spika wa Bunge, Anne Makinda, alisema ni kweli kuwapo kwa namba hizo kunaweza kuathiri zoezi hilo lakini kwa sababu awali hakuna mtu aliyekuwa anajua jina la waziri mkuu mteule, uwepo wa namba hizo si tatizo, kwani umefanywa na mashine.

Alisema jina la yeyote lingeweza kuteuliwa na Rais Kikwete, hivyo Bunge lingefahamu jina hilo baada ya bahasha iliyoletwa na Rais kufunguliwa bungeni.

Lissu, naye alimbana Makinda kwa kutumia kanuni 53 (6)a, (6)c ambapo alisema endapo hoja itatolewa na serikali bila kupitia katika Kamati ya Kudumu ya Bunge, kiongozi wa upinzani bungeni atapata fursa ya kujadili hoja lakini Bunge halikufanya hivyo baada ya hoja ya kumuidhinisha Waziri Mkuu kutolewa.

Kabla ya kutoa mwongozo huo, Makinda, alitaka uchaguzi uendelee na kura zihesabibiwe, jambo lililozusha mzozo wa pande mbili (wabunge wa CCM na wale wa CHADEMA).

Hata hivyo swali hilo lilionekana kuwaumiza vichwa wanasiasa wengi, ambapo Spika wa Bunge la tisa Samuel Sitta, alilazimika kunyanyuka kwenye kiti chake na kwenda kwenye kiti cha Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuteta naye, huku akiwa na kitabu cha kanuni za Bunge.

Wakati Sitta akifanya hivyo, Ukumbi wa Bunge ulilipuka kwa shangwe za kumshangilia, jambo lililomfanya Makinda kusema kuwa angalau amelichangamsha Bunge kwa kuwa lilikuwa kimya kwa muda kidogo.

Wakati hayo yakitendeka, Makinda naye alikuwa akipokea ujumbe wa baadhi ya wabunge ulioonekana kumsaidia namna ya kutoa mwongozo kwa wabunge hao wa CHADEMA.

Baada ya matokeo ya uchaguzi kurejeshwa kutoka kwenye chumba yalikokuwa yakihesabiwa, Makinda alitolea ufafanuzi jambo hilo, ambapo alisema kuwa aliruhusu hoja hiyo kujadiliwa ambapo wa kwanza kuijadili alikuwa ni Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela.

Alisema baada ya Kilango kutoa mchango wake, alitoa hoja ya kutaka hoja hiyo isijadiliwe na kuungwa mkono na wabunge zaidi ya 10, hivyo hakukuwa na haja ya kumpa nafasi Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

Alisema kwa mujibu wa kanuni, hoja ikiungwa mkono na wabunge zaidi ya 10 haina haja ya kuendelea kujadiliwa, ndiyo maana hoja hiyo ilifungwa.

Aidha, alisema hoja yoyote iliyoamuliwa na wabunge na Spika akiifunga, hakuna mbunge atakayeruhusiwa kuizungumzia tena.

Baada ya maelezo hayo ambayo yalionekana kupingwa na wabunge wengi, hasa wa CHADEMA, Naibu Msemaji wa Kambi ya Upinzani, Zitto Kabwe, alisimama kutaka kuuliza swali, lakini Makinda alimnyima nafasi na kuendelea na utaratibu wa kuhesabu kura.

Katika hatua nyingine Lissu, aliteuliwa kuwa msimamizi wa zoezi la kuhesabu kura za kumuidhinisha waziri mkuu, jambo ambalo lilizusha shangwe na makofi mengi kutoka kwa wabunge wa CCM.

Shangwe hizo zilitokana na msimamo uliotolewa juzi na CHADEMA wa kutomtambua Rais Kikwete kwa madai kuwa matokeo yaliyompa ushindi yalikuwa ya wizi.

Wabunge wa CCM na watu wengi walitaka kuona kama Lissu atakataa kwenda kuhesabu kura kwa sababu jina la waziri mkuu, lilipendekezwa na Rais Kikwete ambaye CHADEMA haimtambui.

Hata hivyo Lissu alionekana akijadiliana jambo na viongozi wenzake na baadaye aliinuka kwenda kwenye zoezi hilo huku akishangiliwa na wabunge.

Pinda anatarajiwa kuapishwa kesho katika Ikulu ndogo ya Chamwino mjini hapa.

Tuesday, November 16, 2010

Wagombea wa nafasi ya ubunge jimbo la Mpanda mjini

Wagombea wa nafasi ya ubunge jimbo la Mpanda mjini na mpanda vijijini wakiwa katika picha ya pamoja mbunge mteule wa jimbo la Mpanda kata Bw Said Arfi (Chadema) wa pili kulia baada ya kumalizika kwa mdahalo wa wagombea ubunge katika majimbo hayo uliomalizika katika ukumbi wa Katavi Mpanda mjini,mdahalo huo uliendeshwa na jumuiko la asasi za kiraia Tanzania na kuratibiwa na asasi ya kiraia mkoa wa Rukwa (Rango) kutoka kushoto ni Juma Shaban (CUF) Said Arfi (Chadema) Ezekia Ndimubenya (CUF , Masanja Katambi ( Chadema) na Masanja Kakofia ( NCCR-Mageuzi ) . Picha na habari na Francis Godwin

chadema waanza mchakato wa kudai tume huru ya uchaguzi

Na Ripota Wetu.

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesisitiza bado hakiyatambui matokeo yaliyotangazwa na tume ya Taifa ya uchaguzi na kumpa ushindi Rais Jakaya Kikwete ,lakini imefafanua kuwa hatua hiyo haina maana kwamba wabunge wake na madiwani hawatatekeleza wajibu wao.

Chama hicho kimesema kuwa kutokana na mfumo uliopo sasa kuendelea kupendelea chama tawala, tayari kimeanza mchakato wa kudai tume huru ya uchaguzi kupitia Bunge na mabadiliko ya katiba ili uwanja wa kisiasa uweze kutoa fursa sawa kwa wote.

Mwenyekiti wa Chama hicho Bwana Freeman Mbowe amewaambia waandishi wa habari Mjini Dodoma kuwa amesema kuwa ni muhimu sasa kuundwa kwa tume maalumu kwa ajili ya kufuatilia mwenendo wa uchaguzi uliopita ili hatimaye ibainishe kasoro zilizopo na kutoa majibu sahihi kwa nini wananchi wengi hawakujitokeza kupiga kura.

Kwa upande wake aliyekuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia CHADEMA Dokta Willbroad Slaa amesema yupo tayari kutaja majina ya maofisa wa usalama wa Taifa waliohusika katika kuvuruga zoezi la uchaguzi iwapo majina hayo yatahitajika kama ushahidi mahakamani maana kitendo kilichofanywa ni kosa la jinai.

source : jiachie blog

Monday, November 15, 2010

CHADEMA yashinda Mpanda

na Walter Mguluchuma, Mpanda



MGOMBEA ubunge kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Jimbo la Mpanda Mjini, Said Arfi, aliyekuwa akitetea kiti hicho, ameibuka mshindi.

Habari za kuaminika zilizopatikana kutoka Mpanda jana usiku wakati tukienda mitamboni, zilisema Arfi aliibuka mshindi kwa kupata kura 8,841 dhidi ya mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Sebastian Kapusi, aliyepata kura 8,235.

Hata hivyo, matokeo rasmi yanatarajiwa kutangazwa leo, baada ya msimamizi wa uchaguzi huo, ambaye pia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mpanda, Henry Haule, kushindwa kufanya hivyo jana usiku kwa sababu za kiusalama.

“Ni kweli zoezi la kuhesabu kura limefanyika mara tatu, kwa kila mgombea kujiridhisha kutokana na mchuano kuwa mkali… msimamizi alihofia kutangaza matokeo usiku kutokana na hali ya usalama wa hapa,” alisema mmoja wa maofisa wa CHADEMA.

Alisema licha ya jana kutwa nzima polisi wenye silaha na mabomu ya machozi kuzunguka maeneo ya mji huo kuimarisha ulinzi, hali bado ilikuwa inaonekana kuwa tete.

Wakati huo huo, kundi la vijana wanaosadikiwa kuwa ni kikundi cha ulinzi (Green Guards) cha Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanadaiwa kumvamia nyumbani kwake, Mbunge wa Viti Maalumu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Stella Malaki, kwa kile walichodai kuwa hawakuridhishwa wala kufurahishwa na uteuzi uliompa nafasi hiyo na kumtishia kifo.

Akizungumza na Tanzania Daima mjini hapa, Malaki alisema kamwe hatishiki wala kutetereka, kwa kuwa yeye ni mtetezi wa wanyonge, ambaye yuko tayari kufa akitetea msimamo wake.

“Vitisho vyote hivi ni vya kisiasa, kwani wapo baaadhi ya wanasiasa wa chama kingine wamekasirishwa na mie kuteuliwa kuwa mbunge kupitia CHADEMA mkoani hapa… mie sitishiki na niko tayari kufa kwa ajili ya kuwatetea wanyonge.

“Isitoshe lazima wafahamu mimi ni mzawa wa Wilaya ya Mpanda, nimesomea shule ya sekonadari mkoani Mbeya na niliamua kugombea nafasi hii ambayo ni haki yangu kikatiba, ili ni watetee wanyonge… sasa chuki ya nini?” alihoji Malaki.

Alisema mkasa huo ulitokea juzi majira ya saa 4 usiku, ambapo yeye na mumewe aliyemtambulisha kwa jina la John Malaki, wakiwa pamoja na watoto wao wawili Happiness Bayone (30) na Emmanuel Malaki (20), ambaye alikuwa akiendesha gari la familia aina ya Chaser lenye namba za usajili T 983 AGP, wakitokea Hospitali ya Wilaya ya Mpanda na kuelekea kwao Mtaa wa Nsemulwa mjini hapa.

“Mie tangu kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu Oktoba 31, mwaka huu, nilikuwa napata matibabu…hata wakati nilipotangazwa kuwa ni mbunge mteule kupitia CHADEMA nilikuwa nimelazwa … hivyo usiku wa jana nilikuwa natokea hospitali ya wilaya nachomwa sindano za masaa, nikashtukia navamiwa na kundi la vijana.

“Kwa kuwa leo (jana) nasafiri kwenda Dodoma kuapishwa, niliona ni busara kupitia usiku ule nyumbani kwa mgombea wa Jimbo la Mpanda Mjini, Said Arfi (CHADEMA), ili niweze kuagana naye na kumuelezea mkasa mzima,” alisema Malaki.

Alidai baada ya kuagana na Arfi, walipita Mtaa wa Kawajense wakielekea nyumbani kwao ndipo walifika mbele ya baa iitwayo ‘ Seven Hills’, walisikia sauti za miluzi na kuwaona vijana wakiwa wamevaa miwani mieusi na makoti marefu wakirukia gari lake bila kuelewa sababu ni nini.

Alisema yeye na familia yake walidhani gari lililokuwa likiwafuata nyuma kwa kasi ni la polisi wa doria, lakini walisitaajabu walipoingia nyumbani kwao na gari hilo nalo liliingia.

Alisema ghafla walishuka, aliodai walinzi wa CCM maarufu kama ‘Green Guards’, ambao walikuwa na mapanga na visu, huku mmoja wao akisikika akisema anzisha, kabla ya kuzingirwa, na kuambiwa uteuzi wake haukuwafurahisha.

“Ndipo watoto wangu waliponiomba kwa usalama wangu niingie ndani, lakini niliwakatalia nikawambia kuwa hapa ni nyumbani, nikakataa kuingia ndani kwa kuwa nilikuwa tayari kufa hadi nione nini vijana hao walikuwa wakitaka kutoka kwangu.

“Niliwaambia vijana hao kuwa pamoja na kwamba mimi ni mwanamke, siwaogopi na kama kweli wamedhamiria kuniua basi wafanye hivyo mbele ya famila yangu, msimamo wangu uliwapumbaza na kuamua kuondoka,” alisema.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Isuto Mantage, alipoulizwa, alisema polisi wanafanya uchunguzi wa tukio hilo, ili kubaini vijana hao walitumwa na nani ili waweze kukamatwa.

Mpendazoe: Taifa linaelekea utumwani

na Ratifa Baranyikwa



ALIYEKUWA mgombea ubunge wa Jimbo la Segerea kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Fred Mpendazoe, amesema nchi inaelekea utumwani kwa sababu ya kundi la watu wachache wenye nguvu ya fedha kuamua juu ya nani awe kiongozi.

Mpendazoe aliyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Segerea, kwa ushirikiano waliouonyesha wakati wa kampeni mpaka Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 31, mwaka huu.

Katika mkutano huo, uliofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Liwiti, eneo la Tabata Segerea, Mpendazoe alisema kutokana na matukio mbalimbali ya kisiasa yaliyojiri wakati wa uchaguzi hadi kutangazwa kwa matokeo, ana kila sababu ya kubashiri kuwa nchi inaelekea kwenye utumwa.

“Ninasema hivyo, kwa sababu hivi sasa watu wachache wenye nguvu ya fedha wanaamua mustakabali wa viongozi kwa maslahi yao binafsi,” alisema.

Mpendazoe alisema ikiwa Watanzania hawatakataa kuamuliwa nani awe diwani, mbunge, rais au spika, ina maana hakuna tofauti ya kuwa watumwa, kwa sababu hawawezi kuchagua kiongozi wanayemtaka.

Alisema rais aliyechaguliwa kwa uovu, kamwe hawezi kutenda haki na badala yake atacheza muziki mmoja na mafisadi.

Akizungumzia uchaguzi wa kiti cha ubunge katika jimbo hilo uliompatia ushindi Makongoro Mahanga (CCM), Mpendazoe aliwaambia wananchi hao kuwa hakuna ambaye atabisha kama CHADEMA walishinda Segerea, lakini kwa sababu ya udhalimu, matokeo yaliyotangazwa na tume yalikuwa kinyume.

Aliwaambia kuwa amefungua kesi Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kwa ajili ya kupigania haki ambayo ni ya wananchi.

Alisema leo watakwenda kwa Msajili wa Mahakama, kufuatilia gharama za kuendesha kesi, na kwamba tayari wananchi waliojitokeza awali wamekwisha wachangia kiasi cha sh mil. tano.

TANZANIA DAIMA

Sunday, November 14, 2010

Mheshimiwa Dk Wilbrod Slaa

Katibu Mkuu wa Chadema na aliyekua Mgombea Uraisi kupitia chama hicho Mheshimiwa Dk Wilbrod Slaa akielekea kwenye mkutano maalum na wabunge wateule wa chadema kwenye Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma

Mbunge Zitto Kabwe akisisitiza jambo

Mbunge Zitto Kabwe akisisitiza jambo wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za mitaa ilipofanya ziara wilayani Mbozi, nyuma ni Picha ya Rais mstaafu wa awamu ya pili Ally Hassan Mwinyi.

Mbunge Zitto Kabwe akichangia hoja bungeni

Mbunge Zitto Kabwe akichangia hoja bungeni.

ZITTO KABWE AKISALIMIANA NA WATOTO

Zitto Kabwe akisalimiana na watoto nje ya nyumba aliyokulia huko Kigoma



Wanawake mliochaguliwa saidieni taifa - TAMWA

CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA), kimewataka wanawake waliochaguliwa katika nafasi mbalimbali za uongozi mwaka huu wajiwekee malengo ya kuwatumikia kwa bidii, ubunifu, uadilifu na ujasiri mkubwa wananchi bila kujali itikadi.

Wanawake hao ni Anna Makinda aliyechaguliwa kuwa Spika wa Bunge, wanawake waliochaguliwa kuwa wabunge na madiwani kupitia majimboni na Viti Maalumu.

Taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari mjini Dar es Salaam na kusainiwa na Mkurugenzi wa TAMWA, Ananilea Nkya, ilisema Spika Makinda ni mwanamke mwenye busara, msimamo thabiti, hekima na ujasiri na kwamba atatoa uongozi mpya wenye mtazamo wa kijinsia unaojali zaidi masilahi ya taifa na wananchi wengi.

“Tuna imani Bunge hili jipya chini ya uongozi wa mwanamke litaonyesha mfano kwa vitendo kwamba katika mfumo wa vyama vingi vya siasa inawezekana kuweka mbele masilahi ya wananchi na taifa kuliko masilahi ya vyama vya siasa au viongozi au mbunge mmoja mmoja.

“Ni matarajio yetu makubwa pia kwamba Spika Makinda atajenga mazingira mazuri yatakayoliwezesha Bunge lijalo kufanikisha taifa letu kupata katiba mpya ambayo pamoja na mambo mengine katiba hiyo itachochea uwajibikaji wa viongozi katika ngazi mbalimbali na kujituma kwa wananchi kufanya kazi kwa bidii ili kujenga taifa jipya lenye kujitegemea,” ilisema taarifa hiyo.

Makundi hayo ni pamoja na wanawake wasio na uhakika wa kipato mijini na vijijini, vijana wa kike na wa kiume waliokata tamaa ya maisha, watu wenye ulemavu, wajane na watoto yatima wanaonyang’anywa haki zao, watu wanaoishi na virusi vya ukimwi na wazee.

Tanzania Daima