Showing posts with label Makala. Show all posts
Showing posts with label Makala. Show all posts

Thursday, November 25, 2010

Serikali mpya isimamiwe

MOJA ya habari kubwa leo ni Baraza jipya la Mawaziri lililotangazwa jana na Rais Jakaya Kikwete, Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Baraza la Mawaziri lenye jumla ya mawaziri 50 huku likiwa limefanyiwa mabadiliko ya kimuundo katika wizara mbalimbali zilizokuwepo awali, lilifafanuliwa jana na Rais Kikwete kuwa linalenga kurahisisha ufanisi wa utendaji kazi wa serikali yake.

Izingatiwe kuwa katika idadi hiyo mawaziri ni 29 na manaibu waziri ni 21, na baraza hilo limezidi kuwa kubwa zaidi kuliko lile lililopita ambalo lilikuwa na mawaziri 47.

Ikumbukwe kuwa aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, alikuwa akilalamikia sana ukubwa wa baraza la mawaziri lililopita huku akianisha takwimu mbalimbali zilizoonyesha kuwa lilikuwa likiongeza gharama kubwa zisizo za lazima katika uendeshaji wa serikali.

Aidha, hoja hiyo ya Dk. Slaa ilikuwa ikiungwa mkono pia na wasomi, wanaharakati na watu wa kada mbalimbali huku wakisisitiza kuwa ni muhimu kuwa na serikali ndogo yenye tija na inayobana matumizi.

Kinyume cha kilio hicho cha wadau wa siasa na masuala ya kiutawala, tunasikitika kuona Rais Kikwete ameshindwa kuwa msikivu na kurudia kuunda baraza kubwa tena kuzidi hata lile la awali.

Tunajua kuwa hoja ya Rais Kikwete kuongeza wizara na mawaziri ni kurahisisha utendaji na ufanisi wa serikali yake kama alivyoeleza jana wakati anafafanua sababu za kuigawa wizara ya miundombinu kuwa wizara mbili za Ujenzi na Miundombinu.

Hata hivyo bado tunachelea kushawishiwa na hoja hizo za rais, kwani ukweli ni kwamba mawaziri si watendaji bali ni wanasiasa wanaofanya zaidi kazi ya kuratibu na kusimamia sera ambayo inaweza kufanywa na mawaziri wachache ili mradi kuwe na watendaji bora.

Kwa mantiki hiyo, tulitegemea badala ya Rais Kikwete kuongeza ukubwa wa Baraza la Mawaziri, angefanya mabadiliko ya mfumo wa utendaji na watendaji wenyewe ili kuwarahisishia kazi mawaziri wachache na kuokoa fedha za walipa kodi kwa manufaa ya wananchi.

Kwa dosari hiyo kubwa, ni matumaini yetu kuwa wadau mbalimbali na taifa zima, kila mmoja kwa wakati wake na kwa nafasi yake ataendelea kutimiza wajibu wa kumsihi mkuu huyo wa nchi kupunguza ukubwa wa baraza lake. Bado tunaamini ni msikivu na ataitikia kilio hiki mbele ya safari.

Pamoja na dosari hiyo, bado tunawasihi Watanzania wote kuipa ushirikiano mzuri serikali hiyo mpya iliyotangazwa jana kwani ipo kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wote bila kujali itikadi na tofauti zetu mbalimbali.

Hivyo basi, tunatoa rai kwa chombo kikuu cha kuwakilisha wananchi na kuisimamia serikali (Bunge) kuhakikisha kuwa linashauri, kuifuatilia na kuisimamia serikali hiyo mpya ili iwajibike vizuri na kwa uadilifu wa hali ya juu kwa masilahi ya vizazi vya leo na vya kesho vya taifa hili.

Tunahitimisha kwa kuwataka wananchi wa kawaida na vikundi shinikizi, zikiwamo asasi zisizo za kiserikali (NG’Os na CSO’s) pamoja na asasi za kidini kuunga mkono rai hii ya kuipa ushirikiano serikali yetu pamoja na kuisimamia.

source : tanzania daima

Thursday, November 18, 2010

Mfumo wa uchaguzi unawabana wanawake

na Datus Boniface

WANAWAKE waliokuwa wagombea ubunge na udiwani katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 31, mwaka huu, wamesema mazingira na mfumo wa uchaguzi nchini haumruhusu mwanamke kushiriki na kushindana na wanaume katika kugombea nafasi za uongozi nchini.

Wakizungumza katika kongamano la kutathmini ushiriki wa wanawake katika Uchaguzi Mkuu, lililoandaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) na kufanyika Mabibo, Dar es Salaam juzi, walisema wanawake wanapaswa kujipanga upya ili kuubomoa mfumo kandamizi wa kibepari unaohitaji kutumia fedha kwa kila kitu, ili waweze kushiriki vema katika Uchaguzi Mkuu 2015.

Mwakilishi wa kamati ya wanawake wanaotoka katika vyama visivyo na wabunge, Eliana Mshana, alisema serikali kupitia Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), ilipaswa kuwawezesha wagombea kwa kuwalipia mawakala wa kusimamia kura, lakini haikufanya hivyo.

“UNDP ilitupa taarifa za kimaandishi kuwa wao na mashirika ya kiraia wasingeweza kutuwezesha nyenzo za kugombea bali wangetoa mafunzo ya kutujengea uwezo, ili tuwe jasiri na kujiamini katika kugombea. Serikali ilipaswa kutuwezesha wanawake lakini haikufanya hivyo,” alisema Mshana.

Wakizungumzia changamoto zilizowakumba wanawake katika Uchaguzi Mkuu uliopita, walisema tatizo kubwa lilikuwa ni kuwalipa mawakala ambapo kila mmoja alipaswa kulipwa sh 10,000 kwa siku na kwamba wanawake wengi walishindwa kuzilipa.

Nuru Kimwaga kutoka Chama cha Demokrasia Makini, aliyegombea ubunge Jimbo la Gairo, mkoani Morogoro, alisema changamoto kubwa aliyokumbana nayo ni matumizi makubwa ya rasilimali fedha na vyombo vya usafiri ambavyo yeye hakuwa navyo.

Akizungumzia changamoto hizo, Ofisa Programu Mwandamizi wa TGNP, Anna Mushi, alisema kuna haja ya kujipanga mapema kuhakikisha raslimali zinatafutwa za kutosha kwa ajili ya kuweka mawakala katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Wanawake hao wametoka katika vyama 17 ambavyo ni CHADEMA, NCCR Mageuzi, CUF, TLP, SAU, CHAUSTA, UPDP, UDP, SAU, APPT-Maendeleo, DP, Jahazi Asilia NRA, Demokrasia Makini, UMD na TADEA wakati Chama cha Mapinduzi pekee hakikuwa na muwakilishi katika kongamano hilo.

Jumla ya wanawake 190 waligombea ubunge majimboni mwaka huu wakiwepo 25 CHADEMA, 24 CCM, 15 NCCR-Mageuzi, 14 CUF , 14 UDP, 14 UPDP, 12 TADEA, 11 DP na 10 UMD. Wanawake 557 waligombea udiwani majimboni.

Wednesday, November 17, 2010

Unabii wa kuanguka kwa CCM utatimia hivi

19 Septemba 2007

Unabii wa kuanguka kwa CCM utatimia hivi
na
Samson Mwigamba

ITAKUWA ni mwishoni mwishoni mwa utawala wa rais wa awamu ya nne kutoka CCM. Utawala uliowapa matumaini makubwa hewa wananchi wa jamhuri hii.

Sauti zao wananchi zitapaza na kusikika kila pembe ya nchi hii kama sauti za matarumbeta yatakayopigwa na malaika watakaoambatana na Bwana Yesu wakati akirudi mara ya pili duniani kuchukua wateule, yatakavyosikika kila pembe ya dunia hata kuamsha waliolala makaburini kama inavyosimuliwa ndani ya Biblia takatifu. Wananchi watakumbuka jinsi “walivyouziwa mbuzi kwenye gunia”.

Mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2000, CCM iliunda kamati iliyoongozwa na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (wakati huo), Pius Chipanda Msekwa kwa ajili ya kupitia na kupendekeza utaratibu bora zaidi wa kupata wagombea wa chama hicho wa nafasi mbalimbali za serikali, ikiwamo urais.

Moja ya mapendekezo kadhaa ya kamati hiyo ilikuwa ni kwamba, mgombea urais kupitia CCM awe amepatikana kufikia Mei ya mwaka wa uchaguzi.

Bila shaka ni ili kujipa nafasi ya kutosha kumtambulisha mgombea wao kwa wananchi yasije yakawakumba yale ya mwaka 1995, ambako walipata tabu ya kumtambulisha mgombea asiyefahamika kwa kipindi kifupi hadi wakalazimika kumtumia Baba wa Taifa kuzunguka nchi nzima, akimnadi Benjamin Mkapa ambaye hadi leo wengi wanaamini kwamba wakati akipitishwa na chama kugombea urais, alikuwa hafahamiki kiasi cha baadhi ya watu kudhani aliyepitishwa alikuwa Kenneth Mkapa, mchezaji beki namba tatu wa timu ya Yanga wakati huo.

Hata kabla ya mwaka wa uchaguzi mkuu uliofuata, yaani 2005, pilikapilika zilikuwa zimeshaanza ndani ya chama hicho kikongwe Afrika. Kukawa na kupakana matope kwingi miongoni mwa wanachama walioonekana kuwa na nafasi na nia ya kugombea urais kupitia chama hicho.

Aghalabu kila aliyepakwa matope alisikika akisema “waliofanya hivyo ni kwa malengo ya 2005”. Ni katika wakati huu tulipoanza kuona kalamu ikitumika kwenye magazeti kuchafua baadhi ya watu na kusifia wengine. “Wenye akili” wakang’amua kuwa makusudi ya maandishi kama hayo yalikuwa ni mkakati.

Hatimaye 2005 ikawadia na muda wa kuchukua fomu za kugombea urais kupitia CCM ukawadia. Wanaume 11 waliokamilisha timu ya mpira wa miguu wakajitosa kuchukua fomu.

Wakati huu ndipo tuliposhuhudia kiwango cha juu cha kutumia magazeti kuchafuana. Katika hali ambayo binafsi sikuitarajia, mwandishi maarufu niliyemheshimu na kumpenda kwa makala zake, wa gazeti maarufu la Kiswahili ambalo nilikuwa silikosi kila Alhamisi, alitoa makala mfululizo za kumchambua kila mgombea aliyeomba kupitishwa na chama hicho kuutafuta urais.

Kama kujihami akatoa sababu ya kufanya hivyo tangu mwanzo kabisa wa makala zake, eti ilikuwa ni kwa sababu CCM ndicho chama tawala na hivyo kikipata mgombea mbovu taifa litaathirika.

Mwandishi huyo hakupima hata utetezi wake butu kwa sababu wakati huo kulikuwa na vyama vingine vipatavyo kumi na tano ambavyo vyote vilikuwa na nafasi ya kusimamisha wagombea urais.

Hivyo kama Watanzania wangeona CCM wamesimamisha mgombea mbovu, bila kujali sababu za kufanya hivyo, wangechagua mgombea wa chama kingine. Na hili ndilo lengo hasa la demokrasia ya vyama vingi.

Sasa mwandishi alijuaje kwamba lazima CCM ndiyo ishinde na nani alimwambia kwamba wajumbe wa vikao husika vya uteuzi ndani ya chama hicho hawana uwezo wa kumtambua na kumpitisha mgombea bora kati ya hao kumi na moja mpaka yeye awape wasifu wa kila mgombea?

Waandishi wa namna hii hawakuwa mmoja wala wawili, walikuwa ni wengi, tena ambao hatukuwatarajia. Jitihada zao zilizaa matunda pale ambapo mgombea wao ndiye hatimaye alipitishwa.

Siku ile alipopitishwa, hakuna atakayenibishia nikisema kwamba nchi ililipuka kwa kelele za shangwe na vifijo, maana shangwe haikuwa ndani ya Ukumbi wa Chimwaga pekee, bali kila kona nchi ilizizima, watu wakikokodolea macho kwenye TV.

Wakati Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi huo, Spika Msekwa akisimama kusoma matokeo, nilikatiza mtaa mmoja hapa Arusha na kuona watu wamerundikana kwenye pharmacy moja.

Niliposogea, ndipo nikaelewa kilichokuwa kinaendelea. Tukio hilo liliniachia mshangao na maswali mengi, hasa nikijiuliza Jakaya Kikwete alikuwa na umaarufu gani kiasi cha kushangiliwa vile kwa kuteuliwa kwake kugombea urais.

Ni kweli kwamba hakuwa hata na robo tatu ya umaarufu wa Augustine Mrema mwaka 1995. Hakukaribia hata umaarufu wa Pombe Magufuli, mjenga barabara ambaye alihifadhi kichwani mtandao wote wa barabara zilizo chini ya TANROADS nchi nzima ikiwa ni pamoja na makandarasi wanao/walio – zijenga, wafadhili wanao/walio – toa pesa na hatua zilizofikia.

Huwezi kulinganisha umaarufu wake na ule wa Dk. Salim Ahmed Salim, aliyepata kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika, Rais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na aliyeukosa Ukatibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa tundu la sindano.

Kampeni zilipoanza ndipo nikaelewa kilichofanyika, ambacho sasa ni dhahiri kwa wananchi wote. Kwamba kulikuwa na mtandao uliojumuisha wafanyabiashara, waandishi wa habari, wasanii na watendaji wakuu wa chama na serikali, ulioanza kutengenezwa tangu mwaka 1995 kwa lengo la “kumkuza” na “kumtangaza” mteule wao, hata aonekane maarufu kuliko marais wengine waliopita, isipokuwa tu Mwalimu Nyerere, ambaye ndiye aliyekuwa analinganishwa naye. Kazi hiyo ilifanywa kwa ustadi hadi akaonekana ni “chaguo la Mungu” na wengi wakaaminishwa hivyo.

Utawala wa huyu mteule ulipoanza kwa ari, kasi na nguvu ya soda, kila mtu alikubali kwamba huyu ndiye rais. Hata wanasiasa wa kambi ya upinzani walionyesha kumkubali, hata baadhi yao kufikia kusema “anafanya kazi ya upinzani”.

Watu wakamkubali kwa maneno yake na kwa baadhi ya hatua zilizochukuliwa mwanzoni mwa utawala wake. Kila kukicha kukawa na kauli mbalimbali kwenye magazeti kama; “Awamu ya nne spidi 120”, “Kasi ya Kikwete yamkumba kigogo”, “Sumaye aonja shubiri ya ari na kasi mpya”, “Lowassa hatari, asafiri Arusha – Dar – Arusha kwa siku moja, asimamisha mhandisi wa wilaya”, n.k.

Muda si muda, wananchi wakang’amua kwamba matendo hayo yote yalikuwa nguvu ya soda, walikuwa “wameuziwa mbuzi kwenye gunia”. Kumbe waliotabiri kwamba Kikwete alikuwa ni chaguo la Mungu na wale waliosema ni tumaini lililorejea, walikuwa ni manabii wa uongo. Ukweli ni kwamba alikuwa ni chaguo la wanamtandao na si tumaini lililorejea, bali ni kukata tamaa kulikorejea.

Safari za rais nje ya nchi zikatumbua zaidi ya sh bilioni 24 ndani ya mwaka mmoja wa fedha wakati nchi ikiwa gizani bila umeme, thamani ya shilingi yetu haikushuka bali iliporomoka, mfumuko wa bei ukaongezeka, akiba ya fedha za kigeni aliyoacha mzee Ben ikanywea, mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu ikakatwa kwa asilimia 40 kinyume cha sheria iliyoanzisha mikopo hiyo, rushwa na ufisadi vikaongezeka, mikataba mibovu ikazidi kusainiwa huku watuhumiwa wakifichwa na kulindwa, kodi za mafuta zikapanda na kuongeza ugumu wa maisha huku mishahara ikiongezeka kiduchu.

Lakini katikati ya shida hizo za wananchi, ofisi ya waziri mkuu ikinunua gari mbili tu kwa shilingi milioni 400, posho za wabunge zikipanda hadi sh 100,000 kwa kikao kimoja tu cha siku moja, matumizi ya serikali yenye mawaziri na manaibu wao wapatao 60 zikazidi kuliliza taifa huku kazi wanayoifanya haionekani.

Ndipo kuelekea mwishoni mwa utawala huu, wananchi watapiga kelele. Baadhi ya vyombo vya habari vilivyoupigia debe utawala huu vitajiona viliwasaliti Watanzania. Vitaungana na vyombo vya habari makini kupiga kelele itakayosikika kila kona ya nchi kwamba uhuru wa kweli na mabadiliko ya kweli bado yanahitajika.

Wanafunzi wa vyuo na sekondari watapaza sauti, watumishi wa umma na binafsi watapiga kelele kila kona wakiambiana “hakuna njia ya kuleta mabadiliko nchi hii bila kuipiga chini CCM”.

Baada ya “chaguo la Mungu” kushindwa kuleta mabadiliko, sasa itakuwa ni dhahiri kwamba hata malaika ndiye awe rais wa Tanzania kupitia CCM kwa mfumo uliopo, hakuna mabadiliko yoyote.

Kule vijijini, walimu wa shule za msingi na sekondari watageuka na kuwa walimu wa wananchi wa vijijini wasio na uelewa mpana na mwamko wa mambo ya kisiasa. Watawaelewesha kuwa mabalozi wa nyumba kumi ni viongozi wa CCM tu, na hawana haki wala uwezo wa kuwatisha wananchi hata waichague CCM bila ridhaa yao.

Watawaelimisha kwamba Tanzania itaendelea kuwa nchi ya amani tena amani ya kweli (si ya uongo) bila CCM. Wala anguko la CCM halitaifanya nchi iwe na vita kama Rwanda na Burundi.

Watawaelimisha wananchi nao watayapuuza madai hayo ya kutungwa na CCM, wasiwe na wasiwasi maana chama cha upinzani kikishinda majeshi yote yataitii serikali mpya na kama CCM wana mpango wa kushika silaha na kuingia msituni watakamatwa hata kabla hawajafika ukumbi wa Chimwaga kupanga mipango hiyo.

Ni katika wakati huo ambako walimu hawa watawaonyesha wananchi kodi zote wanazolipa wanaponunua viberiti, chumvi, sukari, sabuni, n.k kutokana na vipesa wapatavyo kwa kutembea kilometa 30 kwa miguu isiyo hata na kandambili kwenda kuuza vitu kama kuni, ndizi, viazi, mbogamboga, n.k. watagundua kwamba kumbe kodi si tu ile waliyokuwa wanalipa ikiitwa ya maendeleo iliyofutwa.

Watatambua kuwa kumbe kuna kodi za moja kwa moja (Direct – taxes) na za mlango wa nyuma (Indirect taxes), ambazo ndizo zinaathiri sana maisha yao ya kila siku.

Watagundua kwamba kumbe wao ni watu wakubwa sana na wanaopaswa kuheshimiwa ndani ya nchi hii. Maana wao ndio waajiri wa serikali.

Ndio wanaowaajiri wabunge, rais na mawaziri wake. Watatambua kuwa wao walio vijijini ndio wanapaswa kuheshimiwa zaidi maana kwa wingi wao ndio wanashikilia cheo cha juu zaidi katika ofisi ya ajira ya wabunge na rais. Wao ndio hutia saini ya mwisho ya ajira ya vigogo baada ya kupata mapendekezo toka kwa wasaidizi wao (wananchi wa mijini).

Watasema sasa tunaitumia vema sahihi yetu, kwa kuheshimu mapendekezo ya wasaidizi wetu walio mijini, na ambao ndio huwafanyia usahili viongozi kwa kupima vitendo vyao, maisha yao ya ukwasi na umaskini wa Watanzania. Wataazimia kuinyima CCM kura.

Wakati huu ndipo vyama vya upinzani vitajiona vina deni. Wananchi watavilazimisha viunganishe nguvu zao na kumsimamisha mgombea mmoja wa urais hata kama CCM haitakuwa imebadilisha sheria ya vyama vya siasa ili kuruhusu vyama kuungana.

CHADEMA, TLP, CUF, NCCR – Mageuzi, UDP na vyama vingine makini vitakaa pamoja na kumpitisha mgombea mmoja na mgombea mwenza wake wa urais. Kila jimbo la uchaguzi atakuwapo mgombea mmoja tu anayekubalika wa upinzani anayewakilisha vyama vitakavyokuwa vimesaini mkataba wa ushirikiano.

Kauli za hamasa kama “hakuna kulala mpaka kieleweke”, “haki sawa kwa wote”, “wananchi tujazwe mapesa”, “nguvu ya umma” nk, zitasikika kila mahali, wakati wa kampeni.

Viongozi wa upinzani watajigawa kila pembe ya nchi na kusambaa, huku wote wakimpigia debe mgombea mmoja tu wa urais na mgombea mmoja wa ubunge katika kila jimbo.

Tukumbuke kuwa kabla ya kampeni, vyama vilivyoamua kushirikiana vitakuwa vimekaa chini na kukubaliana juu ya sera murua za kuiongoza nchi yetu, zitakazotokana na muunganiko wa sera za vyama mbalimbali vya upinzani.

Kubwa likiwa ni kuunda katiba mpya baada ya uchaguzi na kubadili mfumo wa utawala wa nchi hii kubwa ili kuanzisha serikali za majimbo na kufuta kabisa cheo cha waziri mkuu, mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya.

Naam, wakati wa kura utawadia. Kura zitapigwa na ingawa CCM itajitahidi kuiba kura kama kawaida yake, lakini bado zitakazobaki zitatosha kuupa upinzani ushindi mzito na kuuwezesha kuunda serikali ya umoja wa kitaifa.

Mara tu baada ya rais kuapishwa atalihutubia Bunge na kutangaza mchakato wa kukusanya maoni ya kuunda katiba mpya kwa kutumia tume maalum itakayoongozwa na jaji maarufu kama Robert Kissanga.

Wakati mchakato huo ukiendelea, mali zilizohodhiwa na CCM wakati zikiwa ni za wananchi wote, kama viwanja vya mpira, zitarejeshwa serikalini. Wakati huo huo nyumba zote za serikali walizojiuzia vigogo zitarudishwa serikalini.

Mikataba mibovu ya madini, IPTL, Richmond, ATCLM, TTCL n.k itapitiwa upya sambamba na kuwafikisha mawaziri wote wa zamani kama kina Nazir Karamagi na watendaji wakuu mbele ya jopo maalum la majaji ili kujieleza kwa nini walisaini mikataba isiyo na masilahi kwa taifa.

Watumishi wote wa umma watalishwa yamini kuhakikisha hakuna hata shilingi moja ya serikali inayopotea kwa njia yoyote ile bila kunufaisha Watanzania wote.

Hata hivyo kima cha chini cha mshahara kitapanda hadi sh 275,000 bila kugusa kodi za vitu ‘sensitive’ kama mafuta, ili kuepuka mfumuko wa bei na hivyo ongezeko la mshahara kumnufaisha mfanyakazi wa kawaida. Hii itakuwa motisha kwa watumishi wa umma kuachana na rushwa na ubadhirifu.

Muda si muda serikali itakuwa na pesa nyingi, kwani TRA watakusanya si chini ya sh bilioni 300 kwa mwezi, utalii na maliasili zingine zitamwaga trilioni za shilingi ndani ya hazina kufuatia udhibiti wa maliasili zetu na kurekebisha mikataba mibovu ambayo hata hivyo itasitishwa kila inapofikia mwisho wa kipindi cha mkataba.

Pesa hizi zitatumika kutoa elimu bure hadi chuo kikuu, matibabu bure, kuleta mapinduzi ya kweli ya kilimo na ujenzi wa miundombinu kama barabara za lami, viwanja vya ndege vya kisasa, umeme wa uhakika na mawasiliano.

Katiba itakapokamilika na kuruhusu uanzishwaji wa serikali za majimbo, italeta ushindani baina ya majimbo huku kila jimbo kikiongozwa na viongozi wazawa ndani ya jimbo husika, wenye uchungu na maliasili zao na nia ya kuleta maendeleo majimboni mwao kwa msaada wa karibu wa serikali kuu.

Hii itaongeza kasi ya maendeleo na ukuaji wa uchumi na hapo ndipo Tanzania itakuwa tayari KUPAA!!!

Barua kwa Rais Kikwete - Wagombea Binafsi

31 Mei 2006

Barua kwa Rais Kikwete - Wagombea Binafsi

MAAMUZI YA MAHAKAMA KUHUSU WAGOMBEA BINAFSI NA UMUHIMU WA KUBADILI MFUMO WETU WA UCHAGUZI

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Ikulu,
Dar es Salaam.


Ndugu Rais,

Kwanza naomba nikupe pongezi kwa kuchaguliwa kwako kuwa Kiongozi wa nchi yetu. Inawezekana kuwa tayari nimeshakupa hongera tulipokutana pale Dodoma siku uliyomwapisha Waziri Mkuu Ndg. Edward Lowassa au vile vile tayari umekwisha pongezwa na Mwenyekiti wangu wa chama cha CHADEMA ndg. Freeman Mbowe pale Diamond Jubilee. Hata hivyo, kwa kuwa hii ni mara yangu ya kwanza kuwasiliana na wewe kama Rais kwa barua, nimeona ni bora nikupe hongera zangu tena.

Vile vile nikutie moyo kwa kazi unayofanya. Umeanza kazi kwa kasi mpya, ari mpya na nguvu mpya ili kuleta Mabadiliko ya kweli na Uhuru wa kweli kwa jamii ya Watanzania.

Kwamba timu yako nzima ya uongozi inafanya kama wewe ni suala la mjadala mwingine. Sina shaka hata kidogo kuwa Waziri Mkuu na Spika wa Bunge letu tukufu wanaendana na ari yako. Ninaamini watakusaidia vya kutosha. Nina imani kubwa sana na viongozi hawa licha ya changamoto kadhaa ambazo ninaamini ni matatizo ya kimfumo (systematic inherent problems) tu ambayo hata sisi tungefanikiwa kupata ridhaa ya Watanzania na kuongoza taifa letu tungekutana na changamoto hizo. Nikisema sisi, ndugu Rais, nina maana CHADEMA.

Ndugu Rais, barua hii ni yangu binafsi kama kijana mwenye kulipenda taifa langu na bara langu la Afrika. Kwa kuwa nina ofisi ya kitaifa, kama Mbunge, nakuomba uchukulie barua hii kama inatoka kwa Mbunge kwenda Rais wa nchi ambae ni sehemu ya pili ya Bunge.

Barua hii ina mawazo ya kujaribu kusaidia kutokana na changamoto iliyopo mbele yetu kufuatia hukumu ya Mahakama Kuu kuhusu kuruhusu wagombea binafsi wa uongozi wa nchi yetu. Wagombea binafsi maana yake ni wagombea wasio na vyama vya siasa. Wanaweza kuwa ni wanachama wa vyama, lakini hawana dhamana ya vyama vyao wanapogombea na kisha kuchaguliwa kuwa viongozi.

Ndugu Rais, kuwa na mgombea binafsi haina maana kuwa mgombea huyu hatakuwa na udhamini wa aina fulani. Mfano, Kikundi cha Wafanya biashara wa zao fulani (mfano Tumbaku kule Urambo) wanaweza kudhamini watu kadhaa, wakagombea udiwani, wakashika “majority” ya Halmashauri ya Wilaya. Maana yake ni kuwa maamuzi yote ya Halmashauri ya Wilaya Urambo yatakuwa chini ya kundi hili. Hii inawezekana. Inawezekana pia hata kwa ngazi ya Ubunge. Sina uhakika katika ngazi ya Urais. Lakini sina haja ya kukuhadithia alichofanya Rais Bingu wa Mutharika wa Malawi.

Ndugu Rais, Vyama vya siasa vimewekewa masharti ya kuandikishwa. Kuna sheria inayopelekea vyama kusajiliwa na kuna ofisi ya Msajili wa vyama anaeratibu vyama vyote ikiwemo chama chako, CCM. Hata kama mmoja wa wajumbe wa secretariat ya chama chako alinukuliwa akisema Msajili wa vyama ni karani tu, lakini ofisi hii ina majukumu makubwa sana ya kuhakikisha taifa halimeguki kisiasa. Ingawa nina mawazo tofauti, kwamba ofisi hii ingeweza kuwekwa chini ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi badala ya muundo wa sasa. Lakini hii sio hoja kwa sasa.

Kiufupi ni kwamba vyama vinaratibiwa. Katiba zao na hata kanuni zao za uteuzi wa wagombea wa nafasi zote zipo kwa Msajili. Msajili aweza kufuatilia kuona kama chama kinafuata taratibu zake na anao uwezo wa kuonya.

Ndugu Rais, nchi haiwezi kuwa na ofisi ya kuratibu wagombea binafsi. Nidhamu yao Bungeni na hata katika Mabaraza ya madiwani haitaweza kushughulikiwa na vyama. Hawa hawana vyama!

Ndugu Rais, sio nia yangu hata kidogo kushauri kuwa tusiruhusu wagombea binafsi. Hii itakuwa ni kuzuia uhuru wa Mtanzania kushiriki katika uongozi wa nchi. Mahakama imesema ni kinyume na Katiba. Katiba ambayo sote tumeapa kuihifadhi, kuilinda na kuitetea. Kiapo tulichokula ni kikubwa sana na lazima tuheshimu kiapo. Hata hivyo, suala hili ni lazima tuliangalie kwa mapana yake.

Mara baada ya mahakama kutoa hukumu nilinukuliwa na magazeti ya hapa nyumbani na moja na Ghuba (Gulf Times) na lingine na Marekani (The Herald Tribune). Nilisema kuwa maamuzi ya mahakama yanatutaka tufanye mabadiliko makubwa ya mfumo wetu wa siasa. Maamuzi ya mahakama yanaweza kuudhoofisha mfumo wa vyama nchini kwetu.

Uzoefu wangu unaonesha kuwa Watanzania hawapendi vyama. Sio manazi wa vyama vya siasa. Hawaoni kama vyama vinawawakilisha. Wanaona vyama kama vikundi tu vya watu wenye madhumuni ya kutawala. Hawaoni vyama kama Asasi muhimu za kujenga demokrasia na kutoa sera mbadala. Ndio maana kati ya Watanzania milioni 16 waliojiandikisha kupiga kura mwaka 2005, ni Watanzania milioni tano tu ndio wanachama wa vyama. Hata wewe ndugu Rais, umechaguliwa na Watanzania milioni 9 wakati chama chako kina wanachama milioni tatu tu!

Kwa hali hii ya udhoofu wa vyama kutokukonga nyoyo za Watanzania, wagombea binafsi wanaweza kuvuruga kabisa mfumo wa vyama. Hii ni hatari ninayoiona. Ni hatari kweli kweli. Ni hatari kwa sababu, nchi inaweza kukatika kwa matamshi tu ya mtu ambae hana chombo cha kumdhibiti. Vyama vinadhibiti wanachama wake.

Ndugu Rais, mimi binafsi nina maoni yafuatayo ili kuimarisha Demokrasia katika nchi yetu kufuatia hukumu ya mahakama kuu. Mapendekezo yangu haya yanaweza kuwa sehemu ya mjadala wa kitaifa uliouahidi wakati ulipolihutubia Bunge mwishoni mwa Disemba 2005.

* Serikali ikubaliane na maamuzi ya Mahakama:

Mabadiliko ya Katiba yapelekwe Bungeni na kuondoa vizuizi vya Watanzania kugombea uongozi kwa kudhaminiwa na vyama. Sheria ya Uchaguzi ifanyiwe marekebisho na kuweka masharti kadhaa ya kufuata kwa mgombea binafsi. Mfano, mgombea mtarajiwa kupata wadhamini 50 kutoka kila kata iliyopo katika Jimbo, kama anagombea Ubunge na wadhamini 20 kutoka kila Mtaa/Kijiji katika Kata kama anagombea Udiwani. Kama anagombea Urais, apate wadhamini 1000 kutoka kila Mkoa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

* Mfumo wa Uchaguzi urekebishwe na kuruhusu mfumo mchanyato wa uwiano wa kura na mfumo wa “first-past-the-post”:

Ndugu Rais, mfumo wetu wa uchaguzi unataka Wabunge na Madiwani kupatikana kutoka katika majimbo na kata tu. Wabunge wanawake hupatikana kwa uwiano wa kura za Wabunge nchi nzima na Madiwani wa wanawake kutokana na uwiano wa viti vya udiwani ambao kila chama kimepata.

Lakini Wabunge Wanawake hawana mamlaka ya kisheria kwa eneo maalumu. Kwa sasa ni rahisi kusema kuwa wanatoka mikoani, lakini hii ni kwa sababu tuna chama kimoja kikubwa na hivyo kupata kura za kuenea mikoa yote. Huko mbele, tena na hawa wagombea binafsi, itatokea mikoa ambayo haitapata wabunge wanawake kwa sababu kura hazitotosha kwa chama kimoja kugawa wabunge kila mkoa. Umefikia wakati sasa kufanya mabadiliko makubwa ya mfumo wa uchaguzi ili kuingiza uwakilishi wa uwiano.

Napendekeza kama nchi tutafakari mambo yafuatayo yanayohusu mabadiliko ya mfumo wa kisiasa wa nchi yetu:

1. Wabunge wa kuchaguliwa moja kwa moja na wananchi watokane na Halmashauri za Wilaya za sasa. Mfano, badala ya Wilaya ya Manispaa ya Kinondoni kuwa na Wabunge watatu, iwe na Mbunge mmoja tu. Halmashauri ya Wilaya/Mji/Manispaa/Jiji ndio iwe Jimbo la Uchaguzi. Katika ngazi hii wagombea wasio na vyama waruhusiwe pamoja na wale wenye vyama.

Kwa hali ya sasa tutapata Wabunge 119 kutoka kundi hili. Idadi yao itaongezeka kutokana na kuongezeka kwa Halmashauri zitakazoundwa pindi mahitaji yanapotokea. Haitakuwa tena kazi ya Tume za Uchaguzi kuunda Majimbo ya uchaguzi bali vile vigezo vya kuunda Halmashauri (Baraza la Madiwani) vilivyopo kisheria (Local Government Authorities Acts) ndio vitatumika.

2. Wabunge 231 watokane na kura za uwiano. Vyama vya siasa vitapata viti kutokana na uwiano wa kura ambao kila chama kimepata katika Mkoa. Chama cha siasa ni lazima kiwe kimepata kwanza asilimia tano ya kura zote zilizopigwa katika Mkoa husika ili kigawiwe viti. Kwa hiyo kila chama kitatengeneza orodha ya wagombea wake kwa kila Mkoa na kuipeleka Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Orodha hii iwe katika hali ambayo kama jina la kwanza ni Mwanaume la pili awe Mwanamke, hali kadhalika kama jina la kwanza ni Mwanamke katika orodha la pili liwe la mwanaume. Mikoa itapata idadi ya Wabunge kutokana na vigezo maalumu, mfano idadi ya watu n.k. Jambo la kuzingatia tu ni kwamba idadi ya sasa ya Wabunge katika mikoa isishuke baada ya mabadiliko haya (no region shall be left worse off).

Mfano Mkoa wa Kigoma una Jumla ya Wabunge saba wa Majimbo. Iwapo tukibadili mfumo kama ninavyopendekeza hapa, kutakuwa na wabunge wanne wa kuchaguliwa, kutoka Halmashauri za Wilaya Kasulu, Kibondo na Kigoma na Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji. Hivyo wabunge watatu watagawiwa kwa vyama kutokana na uwiano wa kura ambao kila chama kitapata.

Kwa mapendekezo haya tuna uhakika wa kuwa na Wabunge wanawake zaidi ya theluthi moja katika Bunge. Lakini pia tutakuwa na uhakika kwamba kila Mkoa utakuwa na Mbunge au Wabunge wanawake.


Ndugu Rais, mabadiliko haya ya mfumo wetu wa Uchaguzi yana faida nyingi sana. Moja ya faida ni kuvigeuza vyama vyetu vya siasa kutoka katika kushindanisha watu tu, bali pia kushindanisha sera. Kwa sababu wananchi watakuwa wanapiga kura mbili. Kura moja ya chama na kura nyingine ya ama diwani au Mbunge na Rais. Kura ya chama ndio itatufanya kupata wabunge wa uwiano. Wala hatutatumia mfumo mmoja kuzalisha mfumo mwingine. Bali kila mfumo utazalisha Wabunge kuunda Bunge letu.

Vyama vikianza kushindanisha sera tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana kama nchi katika kuimarisha mfumo wa demokrasia na kwa kweli hatutokuwa na wasiwasi wa vyama kudhoofika kutokana na wagombea Binafsi kuruhusiwa.

Demokrasia ndani ya vyama itaimarika kwani Tume ya Taifa ya Uchaguzi itahakikisha vyama vinapata wawakilishi wake katika Orodha ya Mikoa kidemokrasia. Pia pale Bungeni uliahidi kutengenezwa kwa “code of conduct” ambazo zitakuwa binding kwa kila chama ili kuimarisha demokrasia ndani ya vyama.

Ndugu Rais, najua una majukumu mengi ya Kitaifa. Sitaki nikuchoshe na barua yangu hii.

Hata hivyo, sisi hatutokuwa wa kwanza kufuata mfumo huu wa uwiano. Ndugu zetu wa Msumbiji wanafanya hivi. Pia Afrika ya Kusini, Ujerumani, Uswidi na hata India.

Mfumo huu, pia unaweza kumaliza matatizo ya kisiasa ya Zanzibar kwani kila kura itakuwa na thamani. Wawakilishi wa Zanzibar watatokana na kura za kila chama. Kura za Wapemba walio CCM na za Waunguja walio CUF zitahesabika. Hivyo, ile hali ya Pemba yote kutoa Wawakilishi au Wabunge wa CUF tu au Unguja yote kutoa Wawakilishi au Wabunge wa CCM tu itaondoka. Hali hii pia inaweza pelekea kupatikana kwa vyama vingine vyenye wawakilishi au Wabunge kutoka Zanzibar, kwani ushindani utakuwa ni wa sera za vyama na sio watu.

Ndugu Rais, naomba utafakari mawazo yangu haya. Ninaamini kuwa ni muhimu kufanya mabadiliko ya mfumo wa siasa. Kesi ya Mtikila sio sababu pekee ya mabadiliko, bali tunakokwenda hatuwezi kukwepa mabadiliko kwa faida ya demokrasia ya nchi yetu.

Kwa leo naomba niishie hapa. Nakutakia kila la kheri katika kazi.

Kwa ruhusa yako nina nakili barua hii kwa Spika wa Bunge letu Tukufu na pia kwa wasaidizi wako muhimu. Pia nina nakili barua hii kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA ambae pia ni Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Sheria, Katiba na Utawala.

Wako mtiifu,

Zitto Z. Kabwe (Mb)
Kigoma Kaskazini.

Nakala:
Ndg. Samuel Sitta (Mb)
Spika wa Bunge.

Ndg. Edward Lowassa (Mb)
Waziri Mkuu.

Ndg. Kingunge Ngombale Mwiru (Mb)
Waziri (OR) Siasa na Uhusiano wa Jamii.

Ndg. Mary Nagu (Mb)
Waziri wa Katiba na Sheria.

Ndg. Willibrod P. Slaa (Mb)
Katibu Mkuu, CHADEMA.

Tuimarishe Demokrasia tuepuke Ufisadi

13 Machi 2008

Tuimarishe Demokrasia tuepuke Ufisadi
na
Edwin I.M. Mtei
Mwenyekiti Taifa Mwanzilishi

Mjadala uliozuka Tanzania kuhusu ufisadi hivi karibuni, ambao ulipelekea kuundwa kwa Baraza la Mawaziri upya, Mhe. Mizengo Pinda akiwa ni Waziri Mkuu, umedhihirisha umuhimu wa kutathmini kwa kina Katiba ya nchi yetu na sheria zinazohusu ubunge na vyama vya siasa. Nitajieleza kidogo.

Kwanza, licha ya kwamba mafisadi wanasiasa waliobainika ni wanachama wa Chama cha Mapinduzi na Kamati Teule ya Bunge iliyochambua ufisadi wa Richmond ilikuwa na Wana-CCM wengi, hakuna pendekezo lolote lililotolewa hadharani kwamba hawa mafisadi wafukuzwe toka chama chao cha siasa. Swali: Je CCM, kama chama, kinakumbatia mafisadi?

Hapa ni lazima nikiri kwamba nimefadhaishwa sana na tamko la Mheshimiwa Rais wetu, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM, kwamba Waziri Mkuu aliyelazimika kujiuzulu “alipatwa na ajali kazini”, katika kushughulikia kampuni ya Richmond. Siwaelewi Watanzania jinsi mnavyochukulia kama mzaha, kuporwa kwa Shilingi milioni 152 kila siku (Shilingi 55 bilioni kwa mwaka) toka kwa walipiaji wa umeme ili kufidia TANESCO wawalipe kampuni ya Richmond kwa huduma hewa. Mzaha huu umeendelea hata mtuhumiwa mkuu wa uzembe kupokewa “kifalme” aliporejea makwao! Narudia kusema kwamba nafadhaishwa na dalili hizi za kupuuza mambo yanayoathiri maslahi ya umma kwa kiwango kikubwa hivyo.

Kufadhaika kwangu kumeongezeka pale niliposoma magazetini kwamba juhudi zilifanywa na CCM Kyela kuzuiya mapokezi mazuri na wapenzi wake Mhe. Harrison Mwakyembe ambaye alijizolea sifa kitaifa kwa jinsi alivyoongoza uchambuzi wa ufisadi katika kampuni ya Richmond. Kulikoni? Ni watu gani wanafaidika na wizi na ufisadi wa Richmond unaoendelea kutunyonya fedha kulipia umeme hewa? Aidha kuhusu fedha zilizoibiwa kutoka katika akaunti ya EPA, Benki Kuu ya Tanzania, eti zinarejeshwa kimya kimya na Waziri wa Fedha ametangaza kiasi cha Shilingi 50 bilioni kati ya zile Shilingi 133 bilioni zimekwisha rejeshwa.

Swali: Mbona hawa wezi walioshirikiana na maofisa wa Benki Kuu wasitiwe mbaroni na kushtakiwa? Sijapata kusikia serikali yoyote duniani ikifumbia macho wizi wa fedha za umma na kusema eti ni siri kati yake na huyo mhalifu! Tungekuwa na Bunge jasiri linalojali maslahi ya wananchi na umma, Serikali ingepigiwa kura ya kukosa imani nayo.

Sasa nigusie Bunge na siasa za sasa. Katika Bunge letu, hususan katika ile Kamati Teule iliyochunguza Richmond, kulionekana wana-siasa ambao walionyesha kuchukizwa kwa dhati na ufisadi na kutamka dhamira yao ya kuupiga vita. Aidha kwa miezi kadhaa sasa kumekuwa na mijadala hadharani, hasa katika redio na televisheni ambapo wana-CCM mashuhuri, kwa mfano Joseph Warioba, Peter Kisumo na Joseph Butiku, wameonyesha kukerwa na jinsi Chama tawala na Serikali, wanavyoshughulikia rushwa na ufisadi. Wana-siasa wa upinzani wanaoamini kwamba ufisadi ndio kiini cha umaskini na kukosekana kwa maendeleo kunakoikumba Tanzania wanafarijika kwa dalili hizi za kubadilika kwa baadhi ya wanachama wa chama tawala.

Mimi kama mwana-Mageuzi, nimepata kushauri baadhi ya hawa wana-CMM ambao tumefahamiana kwa miaka mingi, wakihame chama chao na kujiunga na chama kama Chadema ambacho kimedhihirisha kwamba kinakubaliana na msimamo wao wa kupinga rushwa na kiliibua mjadala huu. Baadhi yao wamenieleza kwamba kuna misimamo mingine ya CCM ambayo inawavutia, na suala la rushwa peke yake haliwezi kuwafanya wakihame chama.

Labda lao hilo ni jibu sahihi, ingawa kwa kweli nakiri sijui mvuto wa CCM kwa Mtanzania mzalendo thabiti kwa sasa ni nini. Labda wanadhani wanaweza kubadilisha mwenendo wa chama hicho wakibaki ndani.

Ukitafakari kwa kina siasa za Tanzania na hali za wana-siasa, utaweza kubaini kwamba Katiba na Sheria ya Uchaguzi zinawabana wawakilishi, wakiwepo wabunge, kuendelea na chama chao hata pale chama na uongozi wake wanakiuka misimamo ya awali, wanashindwa kutekeleza ahadi na/au wanatenda mbambo kinyume na maslahi ya taifa na dhamiri (conscience) njema. Katika nchi zinazozingatia demokrasia ya kweli, chama kama hicho kinaachia ngazi kutokana na Bunge kupitisha azimio la kukosa imani na uongozi au chama. Lakini hapa kwetu jambo kama hilo halifanyiki; sio kutokana na kwamba chama hakikiuki maadili, bali kutokana na Katiba, sheria na taratibu mbovu.

Kwa hiyo pendekezo langu la kwanza ni kwamba Katiba, sheria na taratibu zirekebishwe ili umma kupitia wawakilishi wao, yaani Bunge, kuweza kuiondoa madarakani Serikali yoyote wakati wowote inapodhihirika imekiuka maadili, ahadi na maslahi ya taifa kama ilivyotokea kuhusu Richmond, ulipaji wa fedha za EPA katika Benki Kuu na kukubali mikataba mibovu mingine inayowaumiza na kuwaathiri wananchi sana. Isiwe ni lazima kungojea mpaka miaka mitano ipite.

Ningetaka kusisitiza kwamba Mbunge au Diwani anachaguliwa na umma. Hapa ninamaanisha kwamba wanachama wa vyama vya siasa katika jimbo/kata ni wachache sana kulingana na idadi ya wananchi wapigao kura. Wengi wa wabunge au madiwani huchaguliwa kutokana na haiba na mahusiano yao na umma na jinsi wanavyoweza kutatua matatizo ya kijamii. Licha ya ukweli huu, Mbunge akiamua kujiuzulu kutoka chama kilichomsimamisha, anapoteza ubunge wake. Vivyo hivyo kama diwani akifanya hivyo, anapoteza udiwani wake. Hii inamaanisha kwamba hawa wawakilishi kila wakati wanahofia kujiuzulu ili kujiunga na kambi ya kutetea maslahi ya umma kwa vile wanatambua ni vigumu kupinga chama tawala na kurudia katika nyadhifa zao mara tu baada ya kukihama.

Kwa hiyo pendekezo langu la pili ni kwamba Katiba yetu na Sheria ya Uchaguzi virekebishwe kuruhusu Mbunge au Diwani kujiuzulu toka chama chake bila kupoteza uwakilishi wake. Naamini hatua hii itaimarisha uhuru wa wawakilishi na demokrasia thabiti katika nchi yetu. Bunge likiimarika, Serikali itatekeleza majukumu yake kwa uadilifu, uzembe utapungua na maendeleo na huduma za kijamii zitanoga kwa manufaa ya wote. Narudia kwamba Katiba yetu inayotamka kwamba Bunge ndicho chombo kikuu kitakachokuwa na madaraka, kwa niaba ya wananchi, kusimamia na kushauri Serikali, itatekelezwa kwa ukamilifu zaidi endapo wabunge hawatawekewa vizingiti na vikwazo katika kukosoa Serikali.

Kama tunadhamiria kwa dhati kusimika demokrasia ya kweli hapa nchini, ni lazima wabunge wawe na uhuru wa kweli kuchangia na kutoa mawazo kulingana na dhamiri yao (conscience), na wakiona ni lazima, basi wahame toka chama chao hasa ikiwa, kwa maoni yao, chama kinakwenda kinyume na maslahi ya umma na taifa. Viongozi wa chama chochote tawala, wakidhihirisha ni waroho wa madaraka na wanatumia nyadhifa zao kujinufaisha binafsi, ni lazima wanachama wazalendo wa kweli wapinge mwenendo huo na wawaondoe katika uongozi huo. La sivyo, basi hao wazalendo wawaachie chama chao hao viongozi mafisadi, wahamie kingine au waunde chama kipya, bila hofu ya kufukuzwa Bungeni.

Hata hivyo, natambua kwamba kama maamuzi ya Mahakama Kuu ya hivi karibuni kuhusu mgombea wa kujitegemea yatazingatiwa na kuingizwa katika Katiba ya nchi na Sheria ya Uchaguzi, basi hata kipengele kinachotaka Mbunge au Diwani aachie uwakilishi wake pale anapojiuzulu kutoka chama chake cha awali, utakuwa hauna mantiki. Kuingia Bungeni hakutategemea tena ulazima wa kuteuliwa na chama cha siasa.

Hapa nieleweke pia kwamba ni lazima vyama vya siasa viwepo na viwe ni vyama imara kama tunataka kuimarisha michango ya mawazo na uchambuzi wa kina katika miswada iletwayo Bungeni na Serikali. Hii haipingani na msimamo kuwa demokrasia ya kweli na uhuru kamili unaweza kuwepo tu pale wanasiasa kibinafsi wanapokuwa huru kwa dhati kutoa maoni yao kwa ujasiri na uzalendo kwa manufaa ya umma.

CHADEMA imekonga mioyo ya Watanzania

Barnabas Lugwisha

HAKUNA ubishi kwamba Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetokea kuwa kipenzi cha wananchi, maana mioyo ya Watanzania wengi imevutiwa na umakini wa viongozi wa chama hicho.

Ukitaka kuhakikisha hilo, rejea siku ile ya kutangazwa kwa matokeo ya awali ya kura za udiwani, ubunge na urais kwa kuyaangalia matokeo kwenye kata za vigogo ambazo baadhi yake ni Oysterbay, Masaki na Mbezi Beach.

Huko ni kwa waliofaidi matunda ya nchi hii na hata kufikia hatua ya kugawana nyumba za serikali. Lakini wote hao wameungana na walalahoi kwa kuipa kura CHADEMA.

Binafsi nasema, vigogo walioiunga mkono CHADEMA, hongereni sana kwani kwa mara ya kwanza mioyo yetu imeunganishwa na sera makini za CHADEMA.

Hata hivyo kwa bahati mbaya, kule kwetu Kiwalani, ndani ya Jimbo la Segerea alikoshinda Dk. Makongoro Mahanga, kura zetu zilipotea.

Katika vituo 37 tulikotumbukiza kura zetu, ilikuwa ni hasara tupu, kwani ofisa mtendaji wetu (jina tunalihifadhi), alitutangazia kuwa kura zetu zimepotea. Tulinyamaza kwa kuwa viongozi wetu walituasa tudumishe amani.

Mpendazoe umo mioyoni mwetu kwa kuwa tulikupa kura zetu, ila wajanja wamezichakachua. Inshallah siku moja utatinga mjengoni!

Turejee kwenye mada, Je, chama hiki kimekuwa mwandani wetu kirahisi? Jibu ni hapana:

Hadi kukonga nyonyo za Watanzania viongozi wakuu wa chama hiki wakiongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe, walihenyeka, wamezunguka huku na kule, kuanzia Mwanza hadi Mtwara, kote huko wamekuwa wakitoa elimu ya uraia sanjari na sera za chama chao.

Nakumbuka ni katikati ya mwaka 2003 nikiwa mwandishi wa gazeti la Mtanzania na The African, naambiwa na mabosi wangu niambatane na CHADEMA katika ziara ya mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, niliambatana na Waheshimiwa mzee Philemon Ndesamburo, Freeman Mbowe, Dk. Willibrod Slaa na Grace Kiwelu, ambao wote hao walikuwa ni wabunge katika majimbo, Kiwelu alikuwa ni Mbunge wa Viti Maalumu.

Narejea nyuma kutokana na mafanikio makubwa sana ambayo chama hicho kimeyapata achilia mbali uchakachuaji wa hali ya juu wa kura za chama hicho uliotokea kufuatia uchaguzi mkuu uliomalizika hivi karibuni.

Katika ziara hiyo ambayo ilikuwa ni ya kukitangaza chama na kutoa elimu ya uraia nilijifunza mengi na nikiyaakisi kwa sasa unatimia msemo wa ‘ukitaka cha uvunguni sharti uiname.’

Tulifika Iringa, Mbeya na kwingineko, leo ni mabadiliko makubwa ambayo nimeyaona kutoka kitambo, CHADEMA imepata mbunge Iringa mjini ambako kulikuwa na wana CCM watiifu mno.

Jambo lililonishanganza ni kwamba katika ziara hiyo, eneo hilo lilikuwa gumu kwa chama hicho, kiasi cha kuwakatisha tamaa viongozi wa CHADEMA katika mikutano yao ya Iringa mjini.

Mathalani, Iringa mjini, ulifanyika mkutano wa hadhara maeneo ya stendi pale, jina la uwanja silikumbuki, katika mkutano huo wananchi wengi walijitokeza lakini cha ajabu kila walipokuwa wakisalimiwa na kiongozi aliye hutubia kwa kauli mbiu ya CHADEMA, wananchi hao walikuwa kimya ama waliitikia kwa mashaka, ni dhahiri walionyesha utii kwa chama tawala.

“People’s power, People’s Power, People’s Power (kimya).” “Aisee hawa watu ni wagumu sana,” alisikika akisema mzee Ndesamburo aliyekuwa akiwasalimia wananchi hao.

Aisee hawa watu ni wagumu sana, kumbe mzee huyu hakugundua kwamba miaka saba baadaye chama chake kitaaminika kiasi cha kupata mbunge katikati ya watu hao wagumu.

Narejea nyuma kidogo kwa sababu ninapenda niwakumbushe Watanzania wenzagu kwamba maisha unavyoyapanga na unavyotaka yawe ndivyo yanavyokuwa.

Hakuna muujiza katika maisha kwamba utapata maziwa na asali bila kufanya kazi, haiwezekani! Viongozi hawa wa CHADEMA wamemenyeka sana, walitembea nchi nzima kwa gharama zao kuwaelewesha Watanzania sera za chama hicho, kuna walio waona wanapoteza muda, lakini kuna waliowaona kama wakombozi wa baadaye wa taifa hili.

Kuna mahali tulipita katika ziara hiyo tukielekea Tarafa ya Makongorosi, nje kidogo ya Jiji la Mbeya, eneo tajiri kwa madini ya dhahabu, lakini lililotopea katika lindi la umaskini.

Nakumbuka ilinibidi kupanda juu ya mti ili nipate mtandao wa simu.

Tukiwa njiani kuelekea eneo hilo, tulikutana na bibi mmoja wa makamo, Mbowe alimuuliza maswali mbalimbali, moja ya maswali hayo nalikumbuka, lilikuwa ni jina la rais wa Tanzania kwa wakati huo (2003).

“Jina la rais ni Nyerere (alikuwa ni Rais Mkapa), alijibu bibi huyo.” Mbowe alitikisa kichwa na kusema, ‘kazi ipo.’

Kazi ipo, kwani mbali na kuwaeleza ukweli juu ya umuhimu wa mabadiliko, imekichukua chama hicho takiriban miaka 18 tangu kuanzishwa kwake kukubalika, hasa kwa Watanzania, na kuwa chama kikubwa rasmi cha upinzani ndani ya mioyo ya Watanzania.

Tukirejea Iringa na Mbeya, sehemu ambayo kila mara baada ya mikutano ya elimu kwa umma viongozi wa CHADEMA walikuwa wakiitwa polisi na kukumbushwa kuzingatia mambo fulani fulani, ilimradi tu kuwabana, leo hii imekuwa ni vituo vikuu vya upinzani katika njia kuu hiyo ya mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

Leo hii ni faraja kubwa sana kutambua kwamba nguvu, rasilimali na elimu ya uraia waliyoitoa viongozi hawa wa CHADEMA havikupotea bure.

Havikupotea bure, kwa sababu ilihitaji ujasiri wa hali ya juu kujitolea kusafiri nchi nzima katika safari zilizopewa majina mbalimbali kama ‘Operesheni Sangara’ ilimradi kuwaelezea Watanzania umuhimu wa mabadiliko katika taifa letu.

Dk. Slaa alitumia muda mwingi kuwaelezea namna ambavyo wana Karatu wanafaidi matunda ya jasho lao, kwa maana ya maendeleo, baada ya kuichagua CHADEMA na hatimaye kuunda halmashauri. Zilikuwa ni hadithi nyingi za kuwaomba Watanzania wabadilike.

Leo hii, Watanzania wameusikia mwangwi kutoka Karatu, Moshi, Kigoma, Mbeya, Iringa, Mwanza na Arusha.

Madonda ya uchaguzi yawe tiba 2015

Christopher Nyenyembe

BAADA ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu uliofanyika, Oktoba 31 mwaka huu huku kila sehemu matokeo yakitangazwa kwa muda na nyakati tofauti, kuliamsha furaha kwa wale walioshinda na kilio kwa walioshindwa.

Jambo la msingi ambalo linaweza kuwa fundisho kubwa sio kujua nani kashinda na nani kashindwa na kushinda au kushindwa hakumaanishi sana kuwepo kwa uzito wa kura haramu na halali isipokuwa matokeo yote yaliyopatikana yanahitaji utayari wa kujuuliza ni wapi kila mmoja alipokosea.

Kwa maana ya kuwa na ushindani wa nguvu kati ya chama tawala CCM na vyama vingine vya siasa kutoka kambi ya upinzani kulipimwa zaidi kwa uwezo wa wagombea kuliko picha waliyokuwa nayo wagombea wengi kuwa pesa zinaweza kuteka maamuzi ya watu.

Watu wamejionea jinsi ambavyo wagombea wenye pesa na mamlaka walivyoweza kuangushwa na pesa zao,wapiga kura wametumia haki yao ya kuchagua mtu waliyemtaka bila kujali pesa, umri, utajiri au umaarufu wa yule aliyedhani atapita kutokana na vigezo hivyo.

Kimsingi uchaguzi huu umeweza kutoa fundisho kubwa na la aina yake kwa wanasiasa, wapiga kura na watazamaji wa kimataifa kuwa nguvu za umma ni imara zaidi kuliko pesa, wapo waliotumia pesa nyingi wamejikuta wakimwagwa na wapo waliotumia pesa nyingi zikaliwa na watu wasiowajua.

Hayo naweza kuyaita kuwa ni madonda ya uchaguzi mkuu na ipo haja ya kutambua kuwa kitendo cha kutoa rushwa kwa wapiga kura ili wakupe kura na huo unakuwa ndio mwanzo wa kilio na kusaga meno kwa watu waliotumia pesa kwa ajili ya kupata madaraka.

Madonda ya uchaguzi mkuu hayatapona kama kila mtu aliyetumia pesa ili kuupatq, udiwani,ubunge au urais atakuwa amekosa nafasi hiyo kwa kigezo cha pesa au yule aliyeshinda naye ameshinda kwa ajili ya kutumia pesa, basi kwa njia hiyo wanapaswa kujua kuwa madonda hayo hayatapona hadi mwaka 2015.

Kutokupona kwa vidonda hivyo kwa namna yoyote ile pia kutasababishwa na namna kila mmoja alikoweza kuzipata fedha hizo, nikimaanisha kuwa wapo walioamua kwenda kukopa kwenye mabenki ili kupata fedha za kuwahonga wapiga kura.

Wapo wale walioamua kwenda kuazima kwa ndugu zao, kukopa kwa riba mitaani na wengine kudiriki hata kutumia fedha walizopewa na wahisani kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo katika maeneo yao, zimetumika kwenye uchaguzi kwa ahadi ya kuzirudisha baada ya ushindi kupatikana.

Wale walioshinda wanajua watapata wapi fedha za kulipia madeni hayo na wale walioshindwa unakuwa ndio mwanzo wa kuwakimbia wadai wao, kuziacha familia zao na kujikuta hakuna mahali pa kukalika, kila sehemu moto, nyumbani moto, mitaani nako moto unawaka.

Lakini kuna jambo muhimu la kujiuliza kuwa ni ujasiri gani wanaoupata watu wanaotaka uongozi wa kufikiria kuwa fedha wanazozitoa zinaweza kuwafikia wapiga kura wote kwenye, kata, jambo au nchi, nadhani hayo tunaweza kuyaita kuwa ni mawazo ya kitoto.

Mtindo huo umeweza kuibua kundi mbaya na la hatari katika uwanja mzima wa demokrasia, hawa madalali wa siasa, wapiga debe au tunaweza kuwaita kuwa wapambe wa wagombea wanajinufaisha kwa kupewa fedha nyingi ili ziweze kuwafikia wapiga kura.

Ukweli ni kwamba fedha hizo haziwafikii walengwa na kama zinafika huko ni tofauti kabisa na matarajio ya mtu aliyewapa fedha hizo kwa ajili ya kuwahoga wapiga kura ambao kadri elimu ya uraia inavyozidi kukua watu wengi sasa hawahongeki.

Madhara ya kufanya biashara bila utafiti ndio hayo na kwa ujumla wake watu wamejionea namna wapendwa wao walivyoweza kubwagwa vibaya pamoja na ujasiri wao wa kutumia pesa bila kukamatwa na TAKUKURU, wamehukumiwa na wananchi.

Mtindo huo wa kuupata uongozi kwa kutegemea pesa unaweza kuwa ukoma wa kisiasa unaowatafuna watu bila kujua faida ya baadaye kuwa kigezo cha kuwa na kiongozi bora sio pesa isipokuwa ni sifa za mtu.

Hata kama kiongozi fulani atafanikiwa kuingia madarakani kwa ajili ya pesa hawezi kupona madonda na huyo anaweza kuwa na maumivu zaidi kwa sababu hana mashiko ya uongozi kutoka moyoni.

Kiongozi wa aina hiyo ni yule mwenye kinyongo, kisasi, hasira na mnyanyasaji akiamini kuwa uongozi alioupata haukuja kwa nguvu za wananchi isipokuwa umetokana na fedha zake nyingi alizozimwaga kila sehemu.

Najua fika kuwa baada ya watu kushinda na wengine kushindwa huu sasa unapaswa kuwa mwanzo wa kutibu vidonda vya ufisadi, kujitakasa na kuamini kuwa pesa ni sehemu ndogo sana ya mafanikio ya mtu katika uongozi wake.

Kujua kuwa fedha zikitumiwa kama silaha ya kuupata uongozi haziwezi kuleta tija kwa wananchi kwa kuwa hata wao hukosa mashiko na upendo kwa kiongozi wa aina hiyo wakijua wazi kuwa hawakumchagua, isipokuwa alijichagua kwa fedha zake.

Kiongozi aliyejiweka madarakani kwa fedha zake, akaweza kuwanunua wapiga kura masikini au akafanya kila njama na hila ya kuwa mgombea aliyepita bila kupingwa huo ndio mwanzo wa kuua demokrasia.

Naamini kabisa kuwa kiongozi anaweza kupita bila kupingwa kwa kukosa mshindani wake lakini hana sifa za kupita bila kupingwa kwa wapiga kura 100,000 waliopo kwenye jimbo lake, ipo haja kiongozi akapimwa na wananchi wenyewe na sio wagombea wenzake.

Hayo yote yanaweza kuwa madonda ambayo tiba yake lazima ipatiwe ufumbuzi kabla ya mwaka 2015 nikiamini kila mmoja atakuwa amejifunza na kushuhudia namna uchaguzi ulivyofanyika mwaka huu.

Kuteteleka kwa nguvu za CCM katika uchaguzi huu na kuruhusu kupoteza majimbo mengi kisiwe kigezo cha upinzani kubweteka, kazi ndio imeanza na ni wazi kuwa CCM nao watajipanga upya kutibu madonda waliyoyapata.

Ili madonda hayo yaweze kutibiwa jibu ni moja tu sasa wananchi wanataka kuona ahadi zilizoahidiwa zinaanza kutekelezwa mara moja bila visingizio wala sababu za kupanda au kushuka kwa thamani ya shilingi.

Wananchi wanataka kuona meli mpya ikielea Ziwa Nyasa, wanataka kuona mv Bukoba mpya ikizaliwa, wanataka kuona mv Liemba mpya ikipiga nanga katika Ziwa Tanganyika na kuwa na babaraba ya juu inayovuka kwenda Kigamboni.

Wanataka kuona viwanja vya ndege vya kisasa vikijengwa kwenye nchi isiyokuwa na shirika makini la ndege, kuwa na barabara zisizokwenda kwenye maeneo ya uzalishaji na wanataka kuona hospitali zikipandishwa hadhi bila ya kuwepo kwa madaktari na wauguzi wa kutosha.

Lengo la wananchi sasa ni kuziona ahadi hizo zinatekelezwa, zitekelezwe bila kujali kuwa maeneo hayo walioshinda ni wapinzani kwa kuwa Rais aliyeshinda alipita kila sehemu akiahidi bila kujua kama chama chake kuna maeneo kitaangushwa.

Kwa kuwa ahadi nyingi zimeahidiwa na rais aliyeshinda, akumbuke kuwa sio rais wa CCM isipokuwa Watanzania wanaye rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyeapa kulitumikia taifa hili na kiapo chake ndio ndoa aliyoifunga na Watanzania wote bila kujali itikadi zao kwa miaka mitano.

Najua madonda ya uchaguzi yamemgusa kila mtu na huo uwe mwanzo wa kujipima, kujirekebisha na kuamua sasa kuwatumikia wananchi bila kinyongo, vinginevyo madonda hayo hayatatibika na tiba yake sio rushwa ni nguvu ya umma.

Sunday, November 14, 2010

Viongozi wenye kashfa wajiuzulu

Mhariri,
NI ombi kwa wanasiasa kwamba katika maisha yao ni vizuri wakawa na kawaida ya kuachana na madaraka hasa pale wanapokuwa na kashfa kwani kujiuzuru kwao kunaweza kusaidia kuwaimarisha kisiasa kuliko kung’ang’ania kama ambavyo wengi wanafanya.

Kwa mfano sijafurahishwa kabisa na namna ambavyo Andrew Chenge alivyomtupia maneno aliyekuwa spika, Samuel Sitta kwamba ameharibu bunge na vitu kama hivi.

Ikiwa kama yeye alilenga kugombea nafasi ya uspika hakuwa na sababu ya kumnenea mabaya Sitta, kwani kati ya yeye na Sitta, ni nani ambaye katika jamii anaonekana wazi kulalamikiwa zaidi na jamii.

Sisi wananchi sio wajinga, mbunge huyu anakabiliwa na kesi mauaji ambayo bado haijatolewa hukumu. Kwanini CCM wasingeacha kwanza mahakama ikamwachia huru na ndipo aruhusiwe kugombea ubunge? Je haki iko wapi mtu ambaye analalamikiwa au ana kesi kama hivi, anamtangaza mwingine kwamba ni mbaya na hafai kuliongoza tena bunge.

Amegombea wananchi tumekaa kimya, haya kapita anaanza kuleta malumbano na wengine ambao hata hawakuwa na matatizo, kisa alimhukumu na kutomtetea alipohusishwa na ufisadi.

Wananchi tulichokisoma hapa ni tatizo la kuwa na ugomvi wao wawili na ugomvi huo ameupeleka katika maslahi ya nchi, hili ni kosa kubwa. Ndio maana wananchi sasa wanafahamu kuwa sheria, miiko na taratibu za kazi/uongozi zipo kwa ajili ya makapuku tu.

Lakini si kwa viongozi wateule. Kwani kosa la kuua iwe kwa bahati mbaya au vinginevyo si swala dogo la kulichukulia juujuu, kana kwamba ni kesi ya wizi wa kuku wa jirani.

Viongozi wenye mamlaka ya kusimamia maadili ya ki utu ya kawaida, wanapo shindwa au kufumbia macho kutoa maamuzi ya kusimamia utawala bora, basi ujue hao viongozi ni kinyume ya viongozi waadilifu, waung wana, wastaarabu .

kwani hawa watakuwa wamejaa kiburi, umimi, uzandiki, unafiki na ni vigumu kufanya kitendo cha kistaarabu kama kujiuzulu. Au kutoshiriki katika uongozi kwani tayari miiko, maadili anayotakiwa kuwa nayo kiongozi hawanayo tena.

Masanja,
Dar es Salaam.

Thursday, October 28, 2010

Tusikubali miaka mitano mingine ipotee

Evarist Chahali

MWAKA 2005 nilikuwa miongoni mwa waliokuwa na shaka juu ya uteuzi wa Jakaya Kikwete kuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Lakini baada ya ushindi wake wa kishindo, nilianza kuwa na imani naye, hasa kutokana na kauli zake za kuleta matumaini mapya.

Baada ya miaka 20 ya tawala za Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa, nchi yetu ilihitaji mtu mwingine mwenye kuelewa kwa nini inazidi kuwa masikini wa kutupwa licha ya utajiri lukuki, mtu mwenye dhamira ya dhati ya kupambana na rushwa kwa vitendo, si maneno matupu (kwa mfano kutangaza kuwa anawafahamu wala rushwa ila anawapa muda wa kijirekebisha).

Awali, sikuamini kuwa Kikwete angeweza kuipatia Tanzania kiongozi wanayemuhitaji kwa vile hukuwa na rekodi hiyo. Licha ya kwamba urais si taaluma inayosomewa, lakini uongozi bora unaweza kubashiriwa kutokana na rekodi ya nyuma ya kiongozi mtarajiwa hasa kwa vile kabla ya kuwa rais wetu, Kikwete alikwisha kushika nyadhifa kadhaa lakini pasipo rekodi ya kujivunia.

Hofu yangu kuhusu Kikwete ilianza kuyeyuka baada ya kusikia kauli yake wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 ya Maisha Bora kwa Kila Mtanzania ingekuwa kipaumbele chake kikuu pindi akichaguliwa, sambamba na kibwagizo cha Kasi Mpya, Nguvu Mpya na Ari Mpya.

Hotuba yake wakati anazindua Bunge, Dodoma, ilileta msisimko mpya, matumaini na imani kwamba hatimaye sasa tumepata kiongozi wa kuifikisha Tanzania inakopaswa kuelekea. Na hata alipotangaza baraza kubwa la mawaziri (lililojumuisha sura zenye utata), nado niliendelea kuwa na matumaini naye na kukubaliana na utetezi wake kwamba ili afanikiwe kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania angehitaji timu kubwa.

Matumaini yangu yalianza kufifia pale ulipotoa hotuba na kutamka kwamba “nawafahamu wala rushwa kwa majina lakini nawapa muda wa kujirekebisha”. Nilivunjwa moyo na kauli hiyo kwa sababu sijawahi kusikia mahala ambako rushwa ilikoma baada ya kiongozi kutoa muda kwa wala rushwa kujirekebisha. Na labda hapa niulize, hivi ile deadline aliyotoa mwaka 2006 kwa wala rushwa (aliodai kuwafahamu kwa majina) kujirekebisha bado haijaisha? Au ilikuwa indefinite deadline (isiyo na ukomo)?

Baadaye alirejea kauli kama hiyo alipofanya ziara ya ghafla Bandari ya Dar es Salaam alikotamka bayana kwamba anawafahamu wala rushwa katika sehemu hiyo na kilichobaki ni kuwaumbua tu (nadhani alimaanisha kilichobaki ni kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria). Inasikitisha kuona hadi leo hakuna aliyewajibishwa huku mamlaka husika zikirejesha mpira huo kwake kwa maelezo ya “waulizeni Ikulu maana wao ndio walidai wana orodha ya wala rushwa hapa”.

Tuwe wakweli, hivi kama aliahidi kuwasilisha majina ya mafisadi wa bandarini lakini hajatimiza ahadi hiyo maana yake ni nini? Je, tunastahili kuendelea naye kama ahadi alizotoa ni zisizotekelezwa? Kama anashindwa kutekeleza ahadi anazotoa mwenyewe pasipo kulazamishwa ataweza vipi kutekeleza mambo muhimu ambayo japo hajaahidi ni lazima ayatekeleze?

Ni kweli kwamba kiongozi wa nchi lazima afanye safari za kujitambulisha nje, lakini hicho hakiwezi kuwa ndiyo kipaumbele kwa kiongozi mwenye dhamira ya dhati ya kurekebisha hali ya nchi masikini kama yetu. Hata Barack Obama na David Cameron, viongozi wa mataifa tajiri kabisa duniani, wametuthibitishia kwamba kwenda nje ya nchi kujitambulisha si kipaumbele kwa kiongozi mpya.

Lakini pengine eneo tata zaidi ni la mafisadi. Kusita kupambana na kundi hili kumezua tafsiri nyingi katika vichwa vya watu, nyingi za hizo, hazimsemi vizuri Rais Kikwete kwa vile imejikita imani kwamba kuwaacha mafisadi waendelee ndiko kulikokwamisha “Maisha Bora kwa Kila Mtanzania”.

Ni siri ya wazi kuwa aliingia madarakani kwa nguvu na jitihada za wanamtandao, wengi wao wakiwa watu wenye rekodi zisizopendeza. Kosa kubwa alilofanya ni kutotumia nafasi yake kama Rais kuwadhibiti, matokeo yake wameishia kuutumia urais wake kujinufaisha wao wenyewe.

Matukio mawili ambayo hayatafutika katika historia ya Urais wa Kikwete ni ujambazi wa fedha za EPA na utapeli wa kampuni ya Richmond na ‘binamu’ yake Dowans.

Kuhusu suala la EPA, wengi wetu tunaamini kwamba bado kuna maswali mengi kuliko majibu. Japo inapendeza kuwaona baadhi ya watuhumiwa wakifikishwa mahakamani, bado haieleweki kwa nini hadi muda huu wamiliki wa kampuni iliyokwiba fedha nyingi zaidi, Kagoda, wameendelea kuhifadhiwa.

Ni kweli safari hii pana ushindani wa kutosha kwenye kiti cha urais. Ni kweli pia kwamba kama akipita, Kikwete atakuwa, kwa mujibu wa Katiba, akitumikia kwa muhula wake wa mwisho. Ninachojiuliza ni kama amemudu kufumbia uoza wote huu katika kipindi muhula wake wa kwanza huku akijua fika kuwa baada ya miaka mitano angepaswa kuomba tena ridhaa ya kupigiwa kura, hali itakuwaje katika muhula wake wa mwisho ambao hatahitaji tena kura zetu?



Barua-pepe:
epgc2@yahoo.co.uk

Monday, October 25, 2010

NUKUU ZA DR WP SLAA


  1. Monduli wanaishi maisha magumu.
  2. Tanzania bila CCM inawezekana, na kuendelea kukaa na CCM ni maafa makubwa.
  3. Kama ningesema uongo kuhusu ufisadi wa JK na waswaiba wake, mbona sichukuliwi hatua?
  4. Ukitukanwa, angalia, puuzia na uondoke. Ukipigwa kofi, mgeuzie na la pili...!
  5. Sipendi kwenda ikulu huku damu zikimwagwa, au kuwaacha watanzania wakiwa vilema kwa ajili yangu...!
  6. Nipo tayari kula mihogo ikulu, ili mtoto wa tanzania asome...!
  7. Siendi kuwa raisi wa Afrika Mashariki, bali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...!
  8. Kodi ya saruji kutoka Tanzania ni 18%, Kenya 15% na Uganda 16%....! Eti ndio makubaliano yaliyowekeana kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki...!
  9. Ninazo nyaraka kuwa serikali ya Tanzania imefanya partial payments huko Canada kwa ajili ya mabango ya CCM...!
  10. Sikatai kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki, lakini lazima tufanye maandalizi kuwapatia watanzania elimu itakayowawezesha kuingia kwenye ushindani...!

Ewe Mpiga Kura Nakusihi Usipoteze Nafasi Hii Adimu Jumapili Ijayo



Siku moja nilikuwa na mazungumzo na babu mmoja wa Kiskotish.Kwa vile ilikuwa ni safari ya masaa kadhaa kwenye treni kutoka mji mkuu wa Uingereza,London kuelekea mji wa kaskazini mashariki mwa Scotland,Aberdeen,tulipata wasaa wa kuongea mengi.Babu huyo ameshawahi kukaa Tanzania,na anajua maneno mawili matatu ya Kiswahili.Swali moja aliloniuliza,na ambalo limeendelea kuumiza kichwa changu hadi leo ni kwanini Tanzania ni masikini licha ya utajiri mwingi ilionao na watu wakarimu,wapenda amani na wenye kiu ya maendeleo.Sio siri,nilijiumauma kutoa jibu la kueleweka.

Uzuri kuhusu hawa wenzetu ni kwamba hawajui kumwonea mtu aibu.Babu huyo alinieleza waziwazi kuwa nimeshindwa kumpa jibu la kuridhisha sio kwa vile sifahamu kwanini Tanzania ni masikini bali nimeona aibu tu ya kutoa jibu sahihi.Na huo ni ukweli.Nilijua nikimwambia kwamba tatizo kubwa kwa maendeleo ya Tanzania ni uongozi,angeweza kuniuliza "kwani viongozi hao ni wakoloni au Watanzania wenzenu?"

Katika maongezi yetu babu huyo alinipa fundisho moja muhimu ambalo nadhani sote tunapaswa kulitilia maanani.Alinieleza kuwa zamani hizo wakati Uingereza inajengwa,Waingereza hawakuwa wanafikiria kuhusu mahitaji yao tu bali pia mahitaji ya vizazi vijavyo.Alifafanua kuwa kadri anavyoelewa,Waingereza wengi wanajibidiisha sio tu kwa ajili ya leo bali hata miaka 200 ijayo.Akanipa mfano wa namna walivyojenga treni za chini ya ardhi,hospitali zao kuubwa kama kijiji kizima,vyuo vilivyotapakaa sehemu kubwa za miji na maendeleo mengineyo.

Akatanabaisha kuwa wengi wa walioshiriki katika ujenzi huo wa Uingereza ya leo kwa sasa ni marehemu.Na akanikumbusha kuwa japo wakati wanajituma kujenga nchi yao walikuwa wanafahamun kuwa watafaidi matunda ya jitihada zao kwa muda mfupi tu kabla Mungu hajawachukua lakini hiyo haikuwakatisha tamaa kwa vile walifahamu kuwa vizazi vijavyo vingetaraji waliowatangulia wangetumia nafasi zilizokuwepo muda huo kuwaandalia mazingira mazuri ya kuishi.

Nifupishe stori.Jumapili ijayo tuna Uchaguzi Mkuu ambao binafsi nauona kama tukio muhimu kabisa kwa historia ya nchi yetu.Takriban miaka 50 baada ya uhuru kuna wenzetu wengi tu ambao wanaishi katika mazingira mabovu kuliko kabla ya ujio wa mkoloni.Lakini pia,kuna wachache ambao angalau wanamudu mahitaji ya msingi ya kila siku.Ni kundi hili ambalo ningependa kuelekeza rai yangu kwao.

Hebu tutafakari stori za huyo babu niliyekutana nae kwenye treni.Laiti kizazi chao kingeridhika na hali waliyokuwa nayo wakati huo basi huenda Uingereza ya leo isingekuwa imepiga hatua kama ilivyo sasa.Laiti wangekuwa wabinafsi wa kufikiria maslahi yao tu wasingejihangaisha na mipango ya maendeleo ambayo matunda yake yangeonekana baada ya vifo vyao.Lakini kwa vile waliweka mbele maslahi ya jamii badala ya maslahi binafsi,hawakusita kujenga msingi wa jamii ya Uingereza kwa wakati huo na karne kadhaa baadaye.

Tunaweza kuendelea kuwalaumu wakoloni kwa kukwaza maendeleo yetu.Lakini wakoloni walishaondoka takriban miaka 50 iliyopita.Sasa badala ya kupiga hatua,kuna nyakati tunajikuta tunarudi nyuma zaidi ya wakati wakoloni wanaondoka.

Na japo siwatetei wakoloni,lakini angalau wao walikuwa na excuse.Hawakuwa Watanzania wenzetu.Hawakuwa na uchungu na nchi yetu wala vizazi vijavyo.Vipi kuhusu viongozi wetu wa sasa?Hivi sio hawa waliosomeshwa bure buleshi lakini leo wanakataa katakata kuwa elimu ya bure haiwezekani?Kama iliwezekana wakati huo ambapo hatukuwa na maendeleo ya kutosha,kwanini ishindikane wakati huu ambapo tumeweza kugundua vyanzo mbalimbali vya mapato?

Tukiridhika na mishahara inayotuwezesha kwenda Twanga Pepeta kial wikiendi,au vikao vya bia kila jioni kisha tukasahau kuwa kuna wenzetu (na wengi wao ni ndugu zetu kabisa) huko vijijini hawana uhakika wa kifungua kinywa,wamesahau ladha ya chumvi kwenye mlo kwa vile chumvi imegeuka anasa japo iko kibwena huko Uvinza,sukari imegeuka muujiza hata huko Kilombero ambako wana kiwanda cha sukari na miwa inayozalisha sukari inaozeana mashambani.Kuna wenzetu ambao wali nyama au ugali nyama ni milo inayowezekana kwenye sherehe,misiba au wanapobahatika mara moja kwa mwaka kupelekwa hotelini licha ya maelfu kwa maelfu ya ng'ombe,mbuzi,kondoo na wanyama pori lukuki,sambamba na mchele,mahindi,mihogo,mtama,nk.

Sasa hali hii itaendelea hadi lini?Tunaweza kupuuza shida za wenzetu hawa ambao ni wengi kuliko sie lakini ni dhahiri kuwa ndani kabisa ya nafsi zetu tunateseka tunapokumbuka kuwa punje za wali tunazosafisha kwa minajili ya kuzitupa zinahitajika kwa udi na uvumba katika nyumba moja au nyingine.Hivi kama hawa "wazungu" na ubinafsi wao (hawa familia ni baba,mama na watoto.Habari za shangazi,binamu,mjomba,babu,bibi ni kama kachumbari kwenye mlo: inapendeza lakini sio muhimu). waliweza kuvikumbuka vizazi vijavyo na hivyo kujenga nchi zao hadi kufikia zilipo leo,wakni sie ambao familia ni zaidi ya mume,mke na watoto?

Kuna wenzetu wanaokumbatia mafisadi kwa vile tu wanahofia kuwa mafisadi hao wakiondoka basi nao hawatakuwa na namna ya kumudu maisha yao.Hiyo si kweli kwani hata nyakati za mkoloni kuna waliokuwa wanatumikia wakoloni na kuwakandamiza waafrika wenzao,lakini watu hao waliendelea kuwa hai,huru na kumudu maisha yao...tena kwa njia halali pasipo hofu ya kuonekana wasaliti.

Kura utakayopiga Jumapili ijayo ni zaidi ya kura yako binafsi.Ni kura kwa ajili ya memba wote wa ukoo wako (ambao katika mazingira ya kawaida kuna wengi tu wenye kuhangaika na maisha ya kila siku),rafiki zako wa zamani ambao baada ya kukosa nafasi ya kuendelea na masomo wakajaribu bahati zao kwenye kilimo lakini jitihada zao zinakwazwa na vyama vya ushirika vinavyojua kukopa zaidi kuliko kuuza mazao.Ni pamoja na wale ambao waliamua kufany kazi za wito kama ualimu au uuguzi lakini sasa wanajiuliza kama "wanafanya kazi ya Kanisa" kwani licha ya mshahara kuwa kijungujiko lakini pia hauna uhakika wa kufika katika muda stahili.Kuna wale jamaa zako walioamua kujiari lakini wanaandamwa na polisi na kubambikiwa kesi za bangi,uzururaji,nk kila wanaposhindwa kutoa rushwa kwa askari au mgambo.

Wafikirie hawa wakati unapiga kura.Weka kando mafanikio yako binafsi.

Na kwa wale wanaoteseka kwa vile watawala wamekuwa bize zaidi na kuongeza idadi ya magari yao ya kifahari,kuongeza idadi ya mahekalu yao,kuongeza idadi ya nyumba ndogo zao,na matumizi mengine ya anasa kama hayo,huu ndio wakati wenu wa kulipa kisasi.Kama mlibebwa kwa malori kwenda kwenye mkutano wa Kikwete au mgombea mwingine wa CCM,well,hakuwaomba bali walijipendekeza wenyewe.Hivi hamsangai ukarimu huu wa ghafla umetoka wapi?Hamjiulizi kuwa wakati mnahangaika kupeleka wagonjwa na akina mama wajawazito hospitalini kwa vile hakuna magari ya vimulimuli wao walikuwa wantembelea magari ya thamani huku wakiwatimulia vumbi,lakini ghafla leo wanawabeba kwenye malori mkawasikilize.MSIDANGANYIKE.Mkishawapa kura,hamtawaona tena mpaka mwaka 2015.

Japo nimesema kuwa uchaguzi huu una umuhimu wa kipekee,lakini ni muhimu kukumbuka kuwa tulikuwa na chaguzi kama hizi huko nyuma,na wa karibu zaidi ni wa mwaka 2005.Hivi hamkupata matumaini Kikwete alipoahidi maisha bora kwa kila mmoja wenu.Je mmeshayaona maisha hayo bora?Kama bado,kwanini mnataka kumwamwini tena safari hii japo amekaa madarakani miaka mitano na ameshindwa kutimiza ahadi aliyoweka mwenyewe bila kushikiwa mtutu wa bunduki (hakulazimishwa)?

Na yule mbunge aliyeahidi miujiza lakini akaishia kuongeza kitambi chake na idadi ya watoto kupitia hawara zake,kwanini umpe tena kura?Unataka aendelee kukusanifu?Maana ulifanya makosa mwaka 2005 ukiamini kuwa ahadi zake zilionyesha anakujali.Lakini miaka hii mitano iliyopita inatosha kukuthibitishia kuwa huyo ni tapeli wa kisiasa,na hakuna tapeli anayeaminika.Lakini sio yeye tu bali hata chama chake.

Hesabu umri wako.Halafu jiulize lini ulianza kuisikia CCM.Kumbuka magapi wameahidi katika miaka yote hiyo uliyokuwa unawafahamu.Linganisha maendeleo yako na hao wenye CCM halisi.Kwanini bado unaendelea kukiamini chama hiki?Kama waliahidi 1995 hawakufanya,lakini wakarejea tena kuahidi mwaka 2000,na hawakufanya.Na bila aibu wakarejea tena mwaka 2005,na safari hii wakiahidi kuwa wanajua matatizo yako na ya familia yako.Wakaahidi pia kuwa maisha yako yatakuwa bora kwa vile hilo linawezekana.Na wakaonyesha namna watakavyowezesha maisha bora kwa kila Mtanzania.Je wametimiza?

Lakini pengine wameshindwa kutimiza kwa sababu za kibinadamu.Sasa kwanini badala ya kukuomba msamaha na kueleza kwanini wameshindwa kukuletea maisha bora,wanakufanya mjinga kwa kukuahidi yaleyale waliyoahidi mwaka 2005 na kutoyatekeleza?Kumbuka: ukiwachagua tena hutokuwa na sababu ya kuwalaumu kwani wameshakuthibitishia kwa miaka kadhaa kuwa hawawezi kukusaidia lakini ukaendelea kuwaamini.Sasa,japo inakera kuona unaendela kuwaamini matapeli hawa,ni muhimu kukumbushana pale tunapokosea.Kufanya kosa si kosa bali kurejea kosa.Na umesharejea makosa hayo mara kadhaa.Sasa umefika wakati wa kusema IMETOSHA.

Nimalizie kwa kukumbusha kuwa katika uchaguzi huu tumebahatika kumpata Nyerere wa pili.Huyu ni Dokta Wilbroad Slaa.Kama ambavyo Nyerere alijitoa mhanga kuhakikisha mkoloni anaondoka,Dokta Slaa amethibitisha kuwa ni mzalendo mwadilifu ambaye ameamua kupambana na mafisadi hadi watokomee.Kama aliweza kuwakalia kooni mafisadi alipokuwa mbunge tu,jiulize atakayofanya atapokabidhiwa urais.Wakati akiwa mbunge silaha yake pekee ilikuwa ni maneno,lakini tukimkabidhi dola atakuwa na nyenzo mbalimbali za kuipeleka nchi yetu inapostahili kwenda.

Usihadaishwe na wasiwasi kuhusu wizi wa kura.Kuiba wataiba lakini ili waweze kuiba za kutosha kuwabakiza mafisadi madarakani itategemea zaidi idadi ya kura tutakazompa Dokta Slaa.Ni rahisi kuiba kura chache lakini ni vigumu kuiba maelfu au mamilioni ya kura.Wingi wa kura kwa Dokta Slaa utakuwa silaha muhimu ya kuwatia aibu mafisadi katika kujaribu kuchakachua kura au matokeo ya uchaguzi huo.

INAWEZEKANA.TIMIZA WAJIBU WAKO

Sunday, October 24, 2010

Ni maafa kuichagua CCM – Dk. Slaa

MGOMBEA urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk. Willibrod Slaa, amesema kuwa ni maafa kwa Watanzania iwapo watakichagua Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 31, mwaka huu.

Kauli hiyo aliitoa jana jijini Dar es Salaam alipokuwa kwenye mdahalo uliokuwa ukirushwa moja kwa moja na Televisheni ya ITV, ambapo alisema kuwa chama hicho kimewafanya Watanzania wawe maskini, kimeendekeza ufisadi na kimeshindwa kutumia rasilimali za nchi kwa manufaa ya walio wengi.

Dk. Slaa alisema hakuna sababu ya wananchi kuwa waoga wa kuwachagua viongozi wapya kutoka upinzani, kwa kuwa hakuna chuo kinachofundisha urais bali kinachoangaliwa ni busara, hekima, kuwashirikisha wananchi na kuweka mbele masilahi ya taifa.

“Kuichagua CCM ni kutafuta maafa zaidi ya haya tuliyonayo, tuache woga wa kuwachagua viongozi wapya, bila CCM Tanzania inawezekana, hata Mwalimu Nyerere alikuwa mpya wakati huo, lakini tulimpa uongozi kwa sababu tulimuamini atatuongoza vizuri,” alisema.

Dk. Slaa alimtupia lawama Rais Kikwete, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM kwa vijana wa chama hicho kufanya fujo kwenye mikutano ya kampeni ya wagombea wa CHADEMA.

Alisema vijana hao wa CCM maarufu kama Green Guard wamekuwa wakipata mafunzo ya kijeshi, kinyume cha Katiba na sheria za nchi na baadaye huenda kufanya vurugu katika mikutano ya CHADEMA pasipo askari kuwachukulia hatua zozote.

Alisema Rais Kikwete ana jukumu kubwa la kukomesha kundi hilo la vijana kwa sababu yeye ni Amiri Jeshi Mkuu na Mwenyekiti wa CCM, ambayo inawalea na kuwapa mafunzo vijana hao.

Dk. Slaa alisema wananchi wasidanganywe kuwa vyama vya upinzani vinaweza kuyumbisha au kuleta machafuko hapa nchini, bali hali hiyo itaweza kuletwa na chama tawala, ambacho kinakuwa kimeshikilia serikali na vyombo vya ulinzi na usalama.

“Mimi sitaki kwenda Ikulu huku damu ya wananchi wangu ikiwa imemwagika au wengine wakiwa na vilema, nataka niende Ikulu kwa amani na furaha ya wananchi wangu walioshiriki kwenye kampeni na uchaguzi uliokuwa na mazingira bora,” alisema Dk. Slaa

Ufisadi

Alibainisha Rais Kikwete na CCM, wameshindwa kuwashughulikia mafisadi kwa sababu wametokana na zao hilo, kwani hata fedha zilizotumika kumuingiza Ikulu zilipatika kwa wizi uliofanyika katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).

Alisema ana ushahidi wa nyaraka wa Kampuni ya Kagoda ambayo ilikwapua zaidi ya sh bilioni 40 na benki zilizohusika katika malipo hayo zinajulikana, lakini mpaka sasa wahusika hawajafikishwa mahakamani.

Alibainisha kuwa Rais Kikwete anahusika na wizi huo, ndiyo maana mpaka sasa hajaweza kumfikisha mahakamani yeye (Dk. Slaa) ambaye alitaja hadharani orodha ya watuhumiwa wa ufisadi akiwamo Rais Kikwete.

“Ninachokisema mimi huwa nina uhakika nacho, kwa sababu nyaraka ninakuwa nazo, mpaka leo hii nadunda mitaani kwa sababu najua Kikwete hawezi kunifikisha mahakamani,” alisema.

Alibainisha kuwa Rais Kikwete hana ubavu wa kupambana na ufisadi kwa sababu hata wale wanaotuhumiwa kushiriki vitendo hivyo huku wengine kesi zao zikiwa mahakamani amewanadi katika mikutano yake ya kampeni kwa kuwaeleza wananchi wawachague kwa madai ni wachapa kazi.

Alisema ni jambo la kusikitisha serikali iliyopo madarakani inabariki wizi wa sh bilioni 155 kupitia Kampuni ya Meremeta ambayo inadaiwa kuwa ilikuwa ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Alisema Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisimama bungeni kutetea wizi huo kuwa fedha hizo zilitumika kwa masuala ya jeshi, ilhali jambo hilo si la kweli, bali zililiwa na wajanja wachache, ambapo fedha hizo zilipitia benki moja ya Afrika Kusini.

Katika hatua nyingine, Dk. Slaa alisema elimu bure kwa Watanzania ni jambo linalowezekana, kwa sababu serikali inazo rasilimali za kutosha lakini kutokana na kutozigawanya inavyotakiwa, jambo hilo limeshindikana.

Alisema Tanzania kamwe haitaweza kujikwamua katika lindi la umaskini kama wananchi wake hawatapata elimu bora kama wanayoipata watoto wa vigogo au wa nchi za Uganda na Kenya.

Alibainisha kuwa hivi sasa hapa nchini kuna matabaka matatu katika sekta ya elimu, ambapo tabaka la kwanza lina uwezo wa kuwasomesha watoto wao nje ya nchi huku lile la pili likiweza kuwasomesha katika shule za kata zilizojengwa hivi sasa.

Tabaka la tatu ni lile ambalo halina uwezo wa kusomesha watoto wao hata katika shule za kata.

Mikataba ya madini

Alisema iwapo atapewa fursa ya kuwa rais ataipitia mikataba yote ya madini na kuirekebisha, ili iweze kuwanufaisha zaidi wananchi kama ilivyo kwa wenzao wa Botswana.

Aliongeza kuwa alikwisha kufanya mazungumzo na watu kutoka nchi za nje ambao walimwambia ni jambo la ajabu kwa Tanzania kupata mrabaha wa asilimia tatu katika sekta ya madini wakati wawekezaji wakipata asilimia 97.

Mabadiliko ya Katiba

Alibainisha kuwa katika miaka yake mitano ya mwanzo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali atahakikisha anaifanyia mabadiliko Katiba ya nchi ili kumpunguzia madaraka rais, ambaye amekuwa akiteua watendaji wengi.

Alisema haoni kazi za manaibu mawaziri, hivyo akiingia madarakani atahakikisha hawateuwi na fedha zilizokuwa zikitumika kuwahudumia zitapelekwa kusaidia ujenzi wa shule, zahanati, barabara na huduma nyingine za kijamii.

Utegemezi wa bajeti

Alisema serikali yake itajitegemea katika matumizi ya kawaida, ikiwemo kulipana mishahara na shughuli nyingine, lakini itaendelea kushirikiana na wafadhili na wahisani ili wasaidie miradi mikubwa.

Aliongeza kuwa serikali yake haitakuwa na kisasi na mtu yeyote, lakini pia haitakuwa na huruma na wanaotumia rasilimali za taifa kwa masilahi binafsi.

Masilahi ya wafanyakazi, wazee

Alisema ataboresha masilahi ya wafanyakazi kwa kupandisha mishahara kulinga na taratibu watakazoziweka lakini pia atashusha gharama za sementi (saruji) na bati, ili wafanyakazi waweze kujenga nyumba.

Kuhusu suala la wazee, alisema ataanzisha utaratibu wa kutoa pensheni bila kujali kama walifanya kazi au la, kwani jambo hilo lilifanyiwa utafiti na watu wa Help Age International Tanzania na likaonekana linawezekana.

Kukubali matokeo ya uchaguzi

Alisema atawaandaa wanachama wake kukubali matokeo iwapo mazingira ya kufanyika kwa uchaguzi yatakuwa huru na haki lakini hawezi kufanya hivyo ikiwa hujuma zitafanyika.

Alisema kocha yeyote ambaye atasema kabla ya kuanza kwa mchezo kuwa timu yake itatoka sare au atayakubali matokeo, atakuwa na matatizo, kwani inawezekana akiingia uwanjani refarii akaipendelea timu pinzani.

Kulinda kura

Alisema jukumu kubwa la kulinda kura ni la mwananchi mwenyewe, kwa sababu kura yake ndiyo maji, barabara na huduma nyinginezo, hivyo ni vema kila mmoja akazilinda kama wakazi wa Kigoma, Karatu, Mpanda Kati, Moshi Mjini na kwingineko.

Aionya NEC

Alisema anashangazwa na majibu ya Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Rajabu Kiravu, kuwa yeye (Slaa) ni muongo, kwa kumpa tuhuma za kuwapo kwa kontena la kura lililokamatwa Tunduma likiwa na kura za mgombea wa CCM.

Alisema alichopaswa kufanya Kiravu ni uchunguzi, si kukurupuka, lakini ni vema akaelewa kuwa Watanzania wa mwaka 2000 si wa sasa, mambo yamebadilika
Alibainisha kuwa Kiravu alipaswa awaeleze wananchi imekuwaje karatasi hizo zichapwe nje ya nchi wakati Waziri anayeshughulikia masuala ya Uratibu na Bunge, Philip Marmo, alisema zitachapishwa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali, lakini hivi sasa zinachapishwa Uingereza.

Dk Slaa: Jukumu la amani si la wapinzani pekee

Mussa Juma, Karatu
MGOMBEA wa urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa amesema kuwa jukumu la kuhakikisha amani inatawala wakati wa uchaguzi mkuu si la wapinzani pekee, bali vyama vyote vinavyoshiriki.
Dk Slaa alikuwa akizungumzia kauli za mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete ambaye amekuwa akidai kuwa kuna vyama vinahubiri vurugu na uchochezi na kuwataka viongozi wa vyama hivyo kuacha na badala yake wanadi sera zao.

Jana, Dk Slaa aligeuka mbogo na kusema kuwa damu imeshaanza kumwagiza kwenye baadhi ya maeneo kutokana na vurugu za CCM, lakini hadi sasa Kikwete amekuwa kimya.


“Jakaya Kikwete hatapona katika hili... damu za Watanzania zimeanza kumwagika Mwanza, Musoma, Hai, Mbeya, Iringa, Arusha na maeneo mengine na yeye yupo kimya kwa kuwa wanaomwaga ni CCM,” alisema Dk Slaa.
Alisema tangu ameanza ziara amejionea jinsi Watanzania wengi walivyokubali mabadiliko hivyo, kama ikitokea kura zao zikaibwa, wa kulaumiwa haitakuwa Chadema wala wapinzani, bali ni CCM.


“Jukumu la amani halipo kwa wapinzani pekee... tumeona damu inamwagika maeneo mengi na Kikwete yupo kimya; sasa naonya kama kweli hali hii ikiendelea na ajue amani inaweza kuondoka kwa kuwa haki ya wananchi inaporwa,” alisema Dk Slaa.
Dk Slaa pia alisema kuwa hagombei urais kwa lengo la kuwa afisa miradi anayeahidi kujenga barabara na zahanati, bali anataka kuongoza nchi.
Mbunge huyo wa zamani wa Karatu, ambaye amekuwa akieleza makombora yake kwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete, aliuambia mkutano wa hadhara uliofurika kwenye Uwanja wa Bwawani, Karatu mkoani Arusha kuwa anataka kuwapatia Watanzania ukombozi wa kweli wa maisha yao.


“Mimi si afisa miradi au mipango wa kusema mkinichagua nitajenga zahanati, nitajenga, barabara nitanunua Bajaj," alisema Dk Slaa akionekana kumlenga mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete ambaye amekuwa akitoa ahadi za kujenga barabara, hospitali na kununua pikipiki za magurudumu matatu ili zitumike kubeba wagonjwa.
"Hiyo siyo kazi yangu (rais) kwa kuwa yote hayo yapo katika mipango ya serikali na mgombea yoyote atakayeshinda atatekeleza,” alisema Dk Slaa.


Alisema ahadi nyingi ambazo zinatolewa sasa na Kikwete tayari zilipangwa na serikali na Bunge lililopita hivyo kuahidi kuzitekeleza sasa ni kuwadanganya wananchi.
“Mpango wa ununuzi wa meli mpya kwenye Ziwa Victoria ulikuwepo, miradi hiyo ya Bajaj ilikuwepo na hata hili la elimu ya sekondari si mpango wa CCM uliigwa na serikali,” alisema Dk Slaa.


Katibu huyo mkuu wa Chadema aliwataka wananchi kupuuza matokeo ya tafiti za kura zilizofanywa na Redet akisema kuwa ukweli halisi unajulikana na utaonekana siku ya kupiga kura Oktoba 31.
Katika mkutano huo. Dk Slaa aliwaomba wakazi wa Karatu kumchagua mgombea wa ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya Chadema, Mchungaji Israel Natse na wagombea wote wa udiwani huku wakihakikisha wanalinda kura zao.


“Mwaka 2005 waliniibia kura na nyie mnajua na hata mahakama ilikiri hivyo naomba mwaka huu mlinde kura wasiibe tena,” alisema Dk Slaa.
Mgombea huyo kesho atakuwa na mikutano kwenye miji ya Monduli mkoani Arusha, Hai, Moshi na mkoani Tanga.

Monday, October 18, 2010

PEMBETATU YA USHINDI: KUELEKEA MABADILIKO

Na. M. M. Mwanakijiji

Njia ya Dr. Slaa kuingia Ikulu inapitia moja kwa moja katika migongo na mabega ya Zitto Kabwe na Freeman Mbowe. Na pamoja nayo inapitia katika pembetatu ya watu hawa watatu kuongoza shambulizi la mwisho katika wiki hizi mbili zilizosalia kabla ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 31, 2010.

Kama kuna kiongozi ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema anayeamini kuwa ipo nafasi nyingine ya kugombania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kushinda nje ya nafasi hii ya 2010 basi mtu huyo anajidanganya. Kama wapo wanachama na mashabiki ambao wanaamini kuwa wakati wa kugombea Urais na kushinda siyo sasa na hivyo wasubiri hadi 2015 au 2010 watu hao vile vile wanajizuga wao wenyewe. Endapo viongozi, wanachama na mashabiki wa Chama hicho maarufu cha upinzani nchini hawatafanya yote wanayopaswa na wanayoweza kufanya katika wiki hizi mbili za mwisho za kampeni basi ndoto ya kuupata Urais itatoweka kama umande wa alfajiri.

Nalazimika kuandika hili kama kuwatia shime wale wote ambao wanataka kweli mabadiliko nchini kupitia chama hicho kuondoa vizuizi vyote vya kihisia na kiakili na kutumia nafasi hii ya kihistoria kuweza kuigombania ipasavyo nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano.

Mkakati wowote wa kutaka kupata wabunge wengi zaidi na siyo kupata Urais wa Jamhuri ya Muungano ni mkakati uliokubali nafasi ya kudumu ya upinzani. Kama viongozi na mashabiki wa Chadema wanapita na kuhamisha watu wawachague wabunge ili kuwe na wabunge zaidi Bungeni ili kwa kufanya hivyo waanze kusikilizwa zaidi na CCM basi watu hao wanakuwa wamekubali nafasi ya upinzani na hawako tayari kuwa watawala. Mkakati wa kupata wabunge wengi ni mkakati mzuri isipokuwa pale tu unapoendana na lengo zima la kutaka nafasi ya urais vile vile.

Ninasema hili kwa sababu kuwa na wabunge wengi wenye kuzungumza zaidi na wenye kufumua mambo mengi Bungeni wakati bado Rais ni wa chama tawala ni kuongeza kelele zaidi Bungeni na “wapiganaji” zaidi lakini ikiangaliwa kwa ukaribu itaonekana ni kujaribu kuwa na miaka mitano iliyopita tena Bungeni. Namna pekee ya kuwa na wabunge wengi bila ya kuwa na Rais inaweza kufaa kama lengo ni kuwa na wingi zaidi ya wabunge kuliko CCM au chama kingine chochote na hivyo kuwa katika uwezekano wa kumtoa Waziri Mkuu, japo siyo lazima kwani kunaweza kuwa na mbunge mwingine anayeonekana kuungwa mkono na wabunge wengi.

Lakini kama lengo ni kuwa na wabunge wengi tu ili kuongeza idadi na hivyo kuwa na “sauti zaidi” basi lengo hili ni zuri kwa kiasi fulani tu na ni kiasi kile kwamba wingi mkubwa wa wabunge wa CCM (super majority) ukiondolewa basi CCM haitoweza tena kubadili Katiba kama ipendavyo au kupitisha mijadala kirahisi rahisi. Katika mazingira hayo vyama vilivyoko Bungeni vitalazimika kujadiliana na kukubaliana na kujifunza kuachiliana vile vile ili mambo yaende. Hili likifanikiwa basi ni jambo kubwa na jema.

Hata hivyo, chama cha siasa chenye kuona tuzo wanayostahili kwa kazi ngumu ni Bunge zaidi na Ikulu wako tayari mwingine aendelee kuishikilia kinajiwekea kizuizi kisicho cha lazima. Chama cha siasa lengo lake ni kuchukua Bunge na Urais ili kwa kufanya hivyo kiweze chenyewe kutekeleza ajenda zake na ilani yake ya uchaguzi. CCM inapopita kuomba kura na kupiga kampeni hakimpigii kampeni Rais tu bali pamoja na wabunge na madiwani wake. Ni katika kutambua hili CCM inaweza kuwa na uhakika wa kutekeleza sera zake na ilani yake. Vivyo hivyo Chadema kama kinajiamini kuwa kimekomaa na kiko tayari kushika madaraka ya juu kabisa ya utawala ni lazima viongozi wake wote, wanachama na mashabiki wake wawe na lengo hilo wazi kabisa katika fikra zao yaani ni lazima wagombea wa ubunge wa Chadema wachaguliwe, wagombea wa Udiwani nao wachaguliwe na yule wa Urais naye achaguliwe. Kusisitiza kuchagua wabunge na madiwani tu bila kusisitiza kuchaguliwa kwa Rais ili chama kiunde serikali siyo mkakati mzuri.

Katika kufikia lengo hilo kwa upande wa Chadema ninaamin nafasi ya watu hawa wawili haiwezi kukwepeka. Mgombea wa Chadema na mbunge maarufu Bw. Zitto Kabwe ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu ana nafasi ya pekee kumletea Dr. Slaa ushindi. Ukiondoa tofauti zao za ndani ya chama na migongano ambayo kama nilivyowahi kusema huko nyuma ni muhimu kwa afya ya Chama Zitto amekomaa zaidi kisiasa na kwa yeyote ambaye amemfuatilia kwenye kampeni zake na za kuwanadi wagombea wengine kwa hakika amevutiwa na utayari wake. Hata hivyo, bado Zitto hajajionesha kuwa anampigia Dr. Slaa debe ili achaguliwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Zitto ni lazima atoke na aseme wazi na pasipo utata kuwa anamuunga mkono Dr. Slaa na anamuombea kura katika kila mikutano yake. Asionekane kusita hata kidogo.

Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema Bw. Freeman Mbowe naye ana nafasi ya pekee katika kumletea ushindi wa kihistoria Dr. Slaa. Hadi hivi sasa ameshafanya makosa makubwa mawili ya kimkakati na ninaamini historia itamhukumu vibaya kama atafanya kosa la tatu na la nne. Kosa la kwanza ni kuamua kugombea Hai tena kitu ambacho kimemlazimu kutumia muda mrefu jimboni humo na kama nilivyosema kwenye Chadema: Kutoka Hapa mpaka Kule CCM wataweka msukumo mkubwa Hai ili kuhakikisha Mbowe arudi Dar au haingii kwenye kampeni za Kitaifa za kumnadi Dr. Slaa. Hili hadi hivi sasa limefanikiwa na asipoweza kujinasua basi atakigharimu sana chama chake kitaifa. Kosa la pili linatokana na hilo la kwanza, kama habari kuwa “Mbowe ana wakati mgumu Hai” zina ukweli kutokana na vyanzo vyangu mbalimbali ninaamini wakati huu “mgumu” hautaisha hadi siku ya kura. Hivyo, Mbowe imemlazimu kufuatilia sana kampeni yake yeye mwenyewe kule Hai na kutokuwa msaada mkubwa kwenye kampeni ya kitaifa na CCM wataendelea kuweka presha zaidi Hai ili kuhakikisha kuwa wanamuangusha. Kumuangusha mtu anayejinadi kuwa ni Kamanda kwenye uwanja wake wa nyumbani itakuwa ni pigo kubwa la binafsi kwa Mbowe.

Lakini pamoja na ukweli wa hali halisi inayoendelea huko Hai ambako katika kampeni za CCM kumetazamwa kama “special case” Mbowe ni lazima anasuke. Ni lazima awe tayari kuitoa kafara Hai ili Dr. Slaa ashinde. Yeye naye anahitajika kuonekana katika mikutano nje ya Hai na sehemu nyingine (kama anvyofanya Zitto sasa) kuanza kuwapigia debe wagombea wengine wa Ubunge na Udiwani pamoja na Dr. Slaa. Hili ni kweli kwani kama kabla ya wiki mbili za uchaguzi Mbowe hana uhakika wa ushindi Hai basi ushindi kwake utakuwa ni mgumu mno. Kamanda mzuri vitani ni yule anayejua ni kita kipi cha kupigana na kipi cha kukiacha. Hivyo, kuna wakati wa vita basi majemedari huamua kupigana katika maeneo mbalimbali lakini maadui zao wakati mwingine hutengeneza kita mahali ili kuwavuta wapiganaji huko huku wao wenyewe wanaendeleza mapambano kwingine. CCM ilijua Mbowe atagombea Hai na walihakikisha kuwa akija hata pingamizi lolote hawaweki lakini watahakikisha wanamtoa katika mtandao wa kampeni ya Dr. Slaa. Bahati mbaya Mbowe ameingia kwenye mtego huu na ni vigumu kujinasua bila kwanza kuwa tayari kutoa kafara Jimbo la Hai. Mimi ninaamini kabisa Mbowe jimbo la Hai atashinda bila hata ya kutumia nguvu nyingi kwani anachokiona kuwa ni presha ya CCM si lolote zaidi ya kile kinachoitwa “drawing the enemy” yaani “kumvuta adui aje”. Mbowe apumzike siasa za Hai na mara moja aende maeneo mengine ya nchi kuwauza wagombea wa Chadema na kumwombea Dr. Slaa kura zaidi.

Ndugu zangu, ushindi wa uchaguzi mkubwa wa kisiasa kwenye nchi mara nyingi hauamuliwi siku ya kwanza ya kujiandikisha kupiga kura au wiki za mwanzo za kampeni. Utafiki wa kisayansi ya siasa unaonesha kuwa wapiga kura wengi hufanya uamuzi wao wiki mbili za mwisho za uchaguzi. Hadi hivi sasa matokeo yote ya kura za maoni yatakuwa na nguvu katika wiki hizi mbili zijazo na siyo yale ya Septemba au Machi. Wiki hizi mbili za mwisho ndizo zitaamua nani anashinda. Ni kutokana na ukweli huo ninaamini kile ambacho Chadema watafanya wiki hizi mbili ndicho hasa kitaamua kama wanaanguka au wanasimama.

Nimesema kuwa kile ambacho “chadema watafanya”. Maanake ni kwamba, ushindi wa Dr. Slaa na wagombea ubunge na udiwani wa Chadema hautaletwa na CCM, TLP au CUF. Hautaletwa na vyombo vya habari na hautaletwa na watu wanaokuja kuwashangilia kwenye mikutano; utaletwa na Chadema wenyewe. Ushindi hautaletwa kama zawadi bali unatakiwa kutafutwa, kupatikana na kuchukuliwa kama lulu iliyopotea. Na ushindi huo hautazuiliwa na CCM.

Kwa uhakika mkubwa naweza kusema kwamba hakuna jambo lolote ambalo CCM na makada wake na hata serikali yake wanaweza kufanya ambalo litaamua kama Chadema inashinda au la. Siamini kabisa kabisa kama Rais Kikwete, Bw. Kinana na Bw. Makamba wanaweza kufanya lolote kuzuia ushindi wa Chadema kama Chadema wanautaka na wanaenda kuuchukua. Kitu pekee CCM inaweza kufanya ni kupunguza makali yake.

Hii ina maana ya kwamba kushindwa au kushinda kwa Chadema kumo mikononi mwao wao peke yao kwa asilimia 1000. Mengine yote yatafuata yenyewe. Lakini ushindi huo utategemea moja kwa moja Pembetatu ya Ushindi (Triangle of Victory) yaani Dr.
Slaa, Freeman Mbowe na Zitto Kabwe. Hawa watatu katika mabega yao wamejibebesha mzigo wa kuiletea Chadema ushindi; naam ule “ushindi wa heshima” kama anavyoita Bw. Kabwe.

Hadi hivi sasa nikiri kuwa Dr. Slaa amefanya zaidi ya vile ambavyo wengi tulitarajia. Kwa kila kipimo Dr. Slaa amejionesha kuwa ni mwanasiasa aliyekomaa na ambaye anaweza kuhimili mikiki ya uchaguzi. Binafsi nikiri kuwa kwa mwanasiasa ambaye ameshambuliwa hadharani maisha yake binafsi (kuacha upadre), maisha yake ya chumbani (kuwa na Bi. Josephine) na kuhimili maumivu ya mkono uliovunjika na kukampeni na vijana wengi akihutubia mikutano mingi kila siku ni wazi kuwa Dr. Slaa ameshajiweka kwenye kaliba nyingine kabisa na kama mgombea sidhani kama wangeweza kumwomba afanye lolote zaidi. Katika wiki hizi mbili za mwisho ni hawa wengine ndio sasa wanaitwa na historia pamoja na wagombea wengine ambao bado wametingwa katika majimbo yao kufanya kile ambacho Umsolopagas alikiita ni “pigo takatifu”.

Ndugu zangu, kama ingekuwa ni ulingoni basi hii ni raundi ya kumi katika pambano la raundi kumi na mbili. Tayari tumeona CCM ikirusha masumbwi yake na Chadema wakirudisha. Hadi hivi sasa watazamaji wanaamini Chadema imeshenda kwa pointi. Na watu wanaamini kuwa ikiendelea hivi hivi katika raundi zilizobakia basi watashinda kwa pointi nyingi tu. Na kama viongozi wa Chadema wataendelea na mbinu zile zile na hotuba zile zile wakiamini kuwa zitawapa ushindi wajiandae kwa mshangao.

Katika mapambano ya ngumi usimdharau bondia mzoefu. CCM ni chama cha siasa na kinajua jinsi ya kufanya siasa (how to do politics). Chadema ni chama cha siasa lakini bado hakijamudu sana jinsi ya kufanya siasa. Ninaamini sasa hivi CCM inachofanya ni kumkumbatia tu huyu bondia mwingine huku ikimvuta muda kumfikisha raundi ya mwisho ambapo itaangusha ngumi kama mvua ili kuhakikisha inamtoa kwa KO. Hivyo, hata kama mnaiona CCM imeshikilia kamba inahema au inaruka ruka kwa mbali msidhani imeshashindwa. CCM bado ni chama chenye nguvu na chenye mbinu za hali ya juu za kisiasa. Yeyote anayewadharau ati kwa vile Chadema inaonekana kushinda asije kujikuta anapigwa na butwaa. Kwani ni mara ngapi tumewahi kuwaona mabondia wanaoongoza mapambano lakini dakika za mwisho wanajikuta hawana ubavu hata wa kurusha ngumi ya ushindi?

Chadema, mashabiki wake na wagombea wake wote wanazo wiki mbili kufikiria ni ngumi ipi na ilenge wapi ili kuhakikisha kuwa CCM ikinyukwa inapata kizunguzungu na kuanza kuona nyota za fedha za EPA zikiyeyuka hewani! Lakini kujiamini kuwa ati Chadema itashinda kwa vile watu wanaishangilia ni kutokujua siasa. Ni matumaini yangu Chadema na viongozi wake watabadilisha mbinu zao za vita, watamshangaza adui na zaidi sana watafanya kile ambacho CCM hata kuwaza kuwa Chadema inaweza kufanya haijawaza. Lakini wakiendelea na mtindo ule ule na mbinu zile zile ambazo CCM inazijua kwa muda mrefu, tusije kujikuta tunashangazwa na kuaza kulia “CCM wameiba kura”. CCM haina haja ya kuiba kura ili ishinde, CCM inahitaji kuchezea wapiga kura kisiasa tu ili ishinde, na nani atawalaumu hiyo ndiyo “siasa”. Chadema wajifunze kujua jinsi ya kufanya siasa dakika hizi za mwisho vinginevyo wasije kujikuta dakika za mwisho wanapatwa kwikwi.

Tayari wana ujumbe wenye kuungwa mkono na watu wengi, tayari wana wagombea viongozi wenye kukubalika na tayari wameshachochea nyoyo za Watanzania kutamani kitu tofauti nje ya CCM. Ndani ya miaka mitano wameikuta ardhi kavu, wameilowesha, wamepende mbegu, mazao yamekua na sasa wakati wa mavuno, Chadema ihakikishe inavuna kiuhakika. Isiionee huruma CCM, viongozi wake wasimuonee huruma Kikwete na CCM bali watoe na wawe tayari kutumia mbinu zote za kisiasa kwenda kupata ushindi. Isije baadaye watu wakaanza kusema “kwanini hamkufanya vile au hivi” na wao wakaanza kutafuta visingizio vya kuhalalisha kushindwa kwao, visingizio ambavyo vitakuwa ni vile vya nje ya chama. Ninaamini kuna mambo kama matatu au manne ambayo Chadema wakiamua kweli kuyafanya siyo tu kwamba watashika hatamu ya uongozi lakini wataonekana kwa haki kabisa wamestahili kufanya hivyo na hakuna mtu atakayeweza kuamua vinginevyo.

Ninachosema ni kuwa Chadema ushindi ni wao kupoteza na Urais ni wao kuukosa. CCM inaombea tu Chadema wasifanye wanachopaswa. Hata ningekuwa mimi, ningeombea Chadema wasipigane kama mashujaa siku ya ushindi. Kwani harufu ya “siku ya ushindi” inanukia kwa mbali. Chadema watafanya kweli? Tuna wiki mbili kuona kwani wananchi wanaweza kufanya yote wanayotakiwa kufanya lakini mwisho wa siku Pembetatu ya Ushindi itasimama pamoja majukwaani?

Naamini tunapoanza kuelekea katika malango ya CCM kuyatikisha na hata kuyafungua kwa nguvu ili hewa mpya ya mabadiliko ipite, hakuna njia nyingine isipokuwa kuona makamanda wa mapambano haya wakinyanyua bendera juu na wakipiga yowe la “ushindi” bila kuona huruma, woga, haya au kusita. Nje ya hapo ushindi wa CCM hautaepukika.

Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com

Saturday, October 16, 2010

Who amongst us fits into the shoes of Nyerere?

By MAKWAIA WA KUHENGA, 14th October 2010 @ 12:00, Total Comments: 4, Hits: 379

ON Thursday was the eleventh anniversary of the death of the Father of this Nation, Founder President Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Going by African tradition, one does not mark the death of a dear one by any festivities such as going on holiday!

It is always a somber and not festive moment. For African animists, they have their own mode of prayers, normally invoking on the spirits of the ancestors of the deceased to either keep well the departed loved one or invoking on them, including the spirit of the departed one, to bless those left behind.

As for the religious ones of today’s major religions, they either say special mass for the deceased or invoke special prayers - du’a or hitma. One is not sure how we marked the 11th anniversary of the departure of the Father of this Nation yesterday, which was a public holiday.

Coming into the midst of campaigns towards elections, the anniversary was certainly low key with only presentations by activists at the University of Dar es Salaam and publishing of bumper editions by the major dailies like this newspaper, which published special editions. But as I have had occasion to point out in this column in the past, it may be appropriate in the future to commemorate Mwalimu’s birthday and death anniversaries separately in compliance with African culture and tradition.

So we could have April 13th every year to celebrate posthumously his birthday anniversary and October 14th his death anniversary. For Mwalimu Nyerere deserves such commemoration because he lives with us and indeed, is a living comprehensive textbook in terms of personal conduct, leadership and vision for this country and the wider world. For today, let us address the question constituting the theme of this subject: Who amongst us fits into his shoes?

Well, if I have included you, the reader of these lines into trying his shoes to see whether we fit into them is for a good reason. As everybody may agree, Nyerere offers a good example for emulation, even by ordinary individuals if one was to take his personal conduct at private level in terms of humility and integrity.

These virtues of humility, especially integrity, makes one stand tall and distinguishes one from others in the pack, isn’t it? But these two virtues can make a huge difference, wouldn’t they, if they are seen in a leader of a nation, especially of poor people like us. Those who saw him in his lifetime may remember that Mwalimu always scorned pomposity in his life style.

He could have opted for top of the market western suits especially tailored for him directly from France or Italy. But he didn’t. He preferred simple suits, easily affordable, the type of suits we called those days ‘Kaunda’ or ‘Chou En Lai’ suits. Such was his life-style – simplicity couched in humility.

A graduate of Edinburgh University, where he earned his Masters Degree, many a reputable universities across the globe had honoured him with honorary doctorate degrees. When people began addressing him, ‘Dr Nyerere’, Nyerere cut them short by these words: “….Oh! No! I will have none of this stuff… I am a teacher (Mwalimu) by profession anyway.

So please just call me Mwalimu…’ In power, Mwalimu never allowed his family to run for political office or run Non-Governmental Organisations (NGOs), least of all his wife and children. If they did, it was only when he had formally retired as Head of State. He also never allowed himself to be overpowered by the trappings of power like awarding himself tenders or businesses.

Seeing the poor condition of his simple house at his home village as he moved closer to retirement, some public institution offered to rebuild and renovate the house for him! One can go on and on in one’s memory lane in so far as Mwalimu’s humility and integrity is concerned. Today, what ordinary people can say without blinking is that Mwalimu Nyerere was not personally a thief.

This explains why even after his retirement he continued to wield unprecedented moral clout and power. He spoke what he himself practised and people believed him because they had empirical evidence in his person! But there is one aspect in his person that made a huge difference and which literally put this country on international map. He knew exactly where to draw the line between personal likes and dislikes and matters of leadership in ethics and national principles.

For the two things, ethics and principles are the ones, which transcend one given leader – they also embody a given nation because they literally translate for a given nation’s self respect. Your memory lane and mine would remember that Tanzania was principled on the question of liberation of other countries in Africa and the principle of relationships with other nations based on sovereignty and genuine independence based on equality and not appendage.

On the latter, Tanzania was taken seriously in all international forums as ‘Africa’s moral voice of conscience.’ The super powers of this world knew the stand of this country, much earlier and they dared not push this country to their line of thinking! At home, everybody knew there was no “friendship” with the president on matters of ethics and national principles and bad leaders knew their place.

The questions to ask ourselves apart from whether we would ever fit into the shoes of Mwalimu Nyerere is what of the many aspects of the qualities of Mwalimu as a human person and a leader have we been able to emulate 11 years on after his death. Of course, there will and there can be only one Mwalimu Nyerere. But surely we have to try, at all levels, to emulate even one aspect of his many virtues, isn’t it?

As Prime Minister Mizengo Pinda asked the other day, does it make sense for a leader or an agricultural field officer to visit peasants at their small farms clad in a three-piece suit or top of the market blazer while the peasants he is visiting are clad in tatters or clothes which have not seen soap for six months?

Makwaia wa KUHENGA is a Columnist for this newspaper. E-mail: makwaia@bol.co.tz