Showing posts with label Mijadala. Show all posts
Showing posts with label Mijadala. Show all posts

Friday, November 19, 2010

UFAFANUZI ZAIDI TOKA KWA DR SLAA

Nadhani message ya Wabunge na ya kwangu iko very clear isipokuwa kwa mtu anayetaka tu kui spin au kuibadilisha kwa sababu anayoitaka mwenyewe. Naomb kurejea mambo ya msingi kwa wale ambao kwa bahati mbaya yamewapita na wana nia ya kuelewa ili spinning hii isiwabughudhi.

i) Mara baada ya uchaguzi, tarehe 3 November, 2010 Dr. Slaa alifanya Press Conference Makao Makuu ya Chadema kama Mgombea Urais ambaye hakuridhika na mchakato wa uchaguzi na Matokeo yaliyokuwa yakitolewa kupita Vituo vya TV na Jaji Lewis Makame, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Katika Press Conference hiyo Dr. Slaa alitaja dosari nzito katika mchakato wa uchaguzi na hasa katika hatua ya kujumlisha na kutangaza Taifa ambapo matokeo yaliyokuwa yakitangazwa na NEC yalitofautiana kwa kiwango kikubwa sana na yale yaliyotangazwa na Wasimamizi wa Uchaguzi (W) pale ambapo zoezi hilo lilifanyika. Nikatoa Mfano wa Geita. Pili, nilieleza kuwa Katika majimbo takriban 25 zoezi la majumlisho halikufanyika kama inavyotakiwa na sheria na hivyo matokeo kutangazwa na wasimamizi kwa utaratibu kinyume na sheria na kanuni za uchaguzi. Tatu, nilieleza kuwa katika maeneo mengine kama Kinondoni masanduku yapatayo 25 ambayo tunayo namba zake tunazo yalipatikana katika ghala la Shule ya Sekondari ya Biafra Jijini Dar-Es-Salaam ambayo hayajahesabiwa na matokeo yamekwisha kutolewa.Nne, Siku ya tarehe 28 October, Tume ya Taifa ya uchaguzi ilialika Wataalam wa IT wa vyama, na kuwa mbele ya Wataalam hao mfumo wa computer uliokuwa unatumika uli "collapse" na Tume kuwajulisha Wataalam kuwa wataita LapTop zote kutoka nchi nzima zirejeshwe Dar kwa matengenezo ya program husika. Ni kuwa wataitwa tena kujulishwa kama zimetengenezwa. Hawakuitwa tena. Hivyo mfumo wa Computer uliotumika kukusanya matokeo na upeleka Taarifa NEC unatia mashaka makubwa.Hata hivyo,baadaye tulipokea Barua kutoka NEC ya tarehe 28/10 ambayo ililetwa kwa Dispatch Makao Makuu Chadema tarehe 5 November, ikisema " Watalaam walikuwa na kukagua mfumo wa IT unaotumika na Tume na waliridhika" . Ni dhahiri barua hii inatia mashaka kwanini barua ya tarehe 8/10 iletwe kwa dispatch na ifike siku takriban 8 baadaye? Hali hii inatia mashaka kuwa barua hii imekuwa backdated kwa Tume kuficha ukweli wa Scandal kubwa iliyotokea katika mfumo ambao uligharimiwa kwa fedha nyingi na UNDP. Iwapo Tume inaweza kudanganya katika swala kama hili tutatukuwa na imani gani na Tume tena. Kutokana na dosari hizo kubwa (pamoja na mambo hayo yaliyojitokeza baadaye) Dr. Slaa, kama Mgombea aliitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi ifanye mambo yafuatayo:

i) Kusimamisha Zoezi la Kutangaza matokeo hadi uchunguzi kamili utakapokuwa umefanyika ili kuondoa hisia na tofauti zilizoanza kujitokeza. Ikumbukwe kuwa Tofauti hizi kimsingi ziligundulika na Wananchi wenyewe kutokana na Tarakimu alizosoma Jaji Makame kutofautiana na zile zilizotangazwa na Wasimamizi katika maeneo yao. Matokeo yake wananchi waliingia mitaani kupinga hali hiyo. Hayo yalitokea Geita, Shinyanga, Mbozi Mashariki na kadhaa. Matokeo yake wananchi hao waliokuwa wanadai haki zao walipigwa mabomu na polisi. Njia ya Busara ilikuwa kuitaka Tume kusitisha zoezi hili ili lisilete athari zaidi, japo hawakufanya hivyo. Chadema tulifanya jitihada za ziada kuwasihi wananchi wetu wasiingie mitaani kuepusha shari. ii) Kuitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kufuta uchaguzi na kutangaza upya marudio ya uchaguzi kwa kuwa Tofauti zilizoko ni kubwa sana, na nikatoa mfano wa Tarakimu za Geita CCM 17,792 CDM 3,789 ( Iliyotangazwa na RO Geita CCM 30,960 CDM 22031) Ni wazi kilichotokea hapa ni kuchakachua kwa lengo la kupunguza kabisa kura za Dr. Slaa, japo za JK nazo zimepunguzwa). Jimbo la Hai CCM 35,910 CDM 18,513 (Iliyotangazwa Hai na RO CCM 20,120 CDM 26,724 = Uchakachuaji uliofanyika hapa ni wa kumwongezea JK kwa zaidi ya kura 15,000 na kupunguza za Dr. Slaa kwa zaidi ya 8,000). Nilitoa pia mfano wa Ubungo ambapo kwa mujibu wa CCM 68,727 CDM 65,450(iliyotangazwa na RO CCM 70,472 CDM 72,252 hapa nako uchakachuaji ulioafanyika ni wa kupunguza kura za Dr. Slaa kwa Takriban 8,000 na kupunguza za CCM kwa kama 2000 hivi) Katika Jimbo la Bunda CCM 20,836 CDM 571 ( Iliyotangazwa na RO CCM 20,836 CDM 18,445 = Tarakimu za Bunda zimerekebishwa katika Taariffa ya mwisho ya NEC. Taarifa hii inaonyesha kuwa Dr. Slaa alipewa kura za Lipumba). Jimbo la Karatu ni kichekesho zaidi kwani kwa mujibu wa Taarifa ya awali ya NEC iliyonukuliwa na Mwananchi CCM 24,364 CDM 41 ( iliyotolewa na RO CCM 24,364 CDM 43,137. Taarifa ya mwisho ya NEC imerekebishwa kufanana na ya RO Karatu. Tume ilikiri kuwa imekosea Taarifa ya Geita japo hadi leo haijarekebisha Taarifa hiyo.Hadi leo hii tarehe 19/11 Tume haijatangaza matokeo ya Geita, Tumbe, Tunduru Kaskazini, na Vunjo kwenye Website yake. ( Tume ilikiri siku ya kujumlisha matokeo Taifa kuwa Vunjo kulikuwa na Taarifa mbili na ikaamua kutumia ile ambayo haikusainiwa na mawakala na kutumia ambayo haina saini ya mawakala. Ni akili ya kawaida tu kujua kuwa kuna jambo hapo.

Hivyo basi kutokana na Dosari hiyo kubwa mgombea yeyote anayekubali kupokea matokeo atakuwa mwendawazimu. Ndiyo maana nikakataa kutambua matokeo na kumtambua Rais aliyepatikana kwa matokeo hayo.

2:Tarehe 15 November, katika Press Conference iliyofanyika Dodoma, Dr. Slaa, alikabidhi rasmi majukumu kwa Chama kwa kuwa kazi ya Mgombea Urais imefikia mwisho wake Baada ya Rais kutangazwa kwa mujibu wa Katiba (Mbovu) ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa chombo ambacho kilikasimiwa madaraka na Kamati Kuu ya Chama ( Sekretariat) mbele ya Wabunge wa Chama. Chama kilipokea majukumu na kuelekeza utekelezaji na ufuatiliaji maazimio hayo ya kukataa matokeo na kumkataa Rais kufanyika kuanzia siku hiyo na Vyombo mbalimbali na ngazi mbalimbali za Chama, na Wabunge wa Chama. Hivyo kilichotokea Bungeni ni utekelezaji wa maamuzi ya Chama hadi pale ngazi za juu za Chama zitakapobariki au kubadilisha msimamo huo. Ni dhahiri basi, i) Wabunge wetu wala Dr. Slaa, hawakuhitaji kurudia madia ya msingi ikiwa ni pamoja na kurudia uchaguzi. Madai ya Mabadiliko ya Katiba au Katiba ya Wananchi na kudai Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kujiuzulu na Kuundwa kwa Tume ya uchunguzi ni madai yaliyotolewa katika Press Conference ya Tarehe 15/11. Hata hivyo, msisitizo wa awali ni kwa kuundwa kwa Tume ya Uchunguzi ambayo inaweza kutupelekea kwenye yote hayo. Mtu yeyote asiyemakini kufuatilia mtiririko huo anaweza kupotosha na kusababisha vurugu na uchochezi ambao Chadema, pamoja na jitihada zake za kudai haki zake na za wananchi waliochakachuliwa kura zao inapenda kufuata njia za kistaarabu na za amani. Ni vema yeyote anayetaka kufanya analysis ya hatua za Chadema kwanza akajielimisha vizuri badala ya kuweka hisia zake ( hakuna sababu ya kuandika na mate wakati wino upo), na wakati wowote Chadema tuko tayari kutoa ufafanuzi utakao hitajika, isipokuwa ule unaopaswa kupitia kwenye vyombo vyetu vya maamuzi kama chama cha kidemokrasia.

Mtizamo wa Bloga: Uamuzi wa Chadema Kususia Hotuba ya Kikwete Bungeni

Suala ambalo limetawala maongezi ya Watanzania wengi kwenye social media kwa leo ni kitendo cha wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kususia hotuba ya Rais Jakaya Kikwete wakati anazindua Bunge jipya mjini Dodoma.Kwanza niweke wazi msimamo wangu kuwa naunga mkono uamuzi huo wa Chadema.Sifanyi hivyo kwa minajiki ya kukipenda chama hicho bali ni katika kuzingatia ukweli kuwa Chadema wametumia HAKI yao ya Kikatiba na kidemokrasia kuonyesha upinzani wak kwa vitendo.Nimeandika HAKI kwa herufi kubwa kwa vile neno hilo ni muhimu katika "kuwahukumu" Chadema.

Baadhi ya wenzetu wamekishutumu vikali kitendo hicho huku wengine wakikiita "utovu wa nidhamu wa hali ya juu".Lakini wakati wenzetu hao wanatumia HAKI zao za Kikatiba na kidemokrasia kuwalaumu Chadema,hawataki kutafakari japo kidogo kuhusu HAKI kama hizo kwa chama hicho,yaani HAKI yao ku-protest kwa amani dhidi ya mwenendo mzima wa uchaguzi uliopelekea Jakaya Kikwete kuwa Rais tena.

Inawezekana tukio hilo linaonekana sio la kawaida kwa vile ni mara ya kwanza kutokea nchini.Lakini kwa wanaojishughulisha kufahamu kinachoendelea sehemu nyingine duniani watafahaku kuwa hali hiyo imeshatokea kwenye mabunge mbalimbali,kwa mfano nchini Afrika Kusini,Gambia,Sudan, India,Pakistan na Iraki,to mention only a few.

Kwa namna moja au nyingine,vipengere dhalimu vya Katiba yetu vimewaacha Chadema na alternatives chache zaidi ya hatua kama hiyo ya leo kwa vile Katiba yetu inanyima uhuru wa kupinga matokeo ya ushindi wa Rais mahakamani hata kama ushindi huo umepatikana kwa njia zisizo halali.Leo mapungufu hayo makubwa kwenye Katiba yetu yanaweza kuonekana kama jambo dogo.Lakini yayumkinika kuamini kuwa inaweza tokea tukapata Rais dikteta ambaye ameshindwa kwa mabavu lakini tukajikuta hatuna njia ya kupinga "ushindi" wake kwa vile Katiba inamlinda.

Tatizo la Katiba nyingi katika "Nchi za Dunia ya Tatu" na hususan barani Afrika ni ile tabia hatari ya katiba hizo kutumika kwa mahitaji na maslahi ya watawala walio madarakani.Na kwa vile wengi wa watawala hao ni walafi na waroho wa madaraka,na kwa vile madaraka makubwa waliyonayo yanawapa uhuru wa kufanya lolote wapendalo,katiba hizo huwekwa viraka hapa na pale sio kwa minajili ya ustawi wa taifa husika bali kikundi kidogo cha watawala.

Laiti Katiba ingekuwa inaruhusu ushindi wa Rais kupingwa mahakamani basi ni dhahiri Chadema wangeshafungua kesi.Kuna wanaosema "sasa wakitoka nje ya Bunge ndio inasaidia nini?"Majibu ni mengi ila hapa nitatoa machache tu.Kwanza,ikumbukwe kuwa Chadema ndio chama kikuu cha upinzani bungeni.Pamoja na uchache wa idadi ya wabunge wao ukilinganisha na wale wa CCM,hadhi ya chama kikuu cha upinzani ni kubwa na muhimu ndani na nje ya nchi.Pamoja na mazingira na sheria kandamizi dhidi ya vyama vya upinzani,kwa nchi masikini kama Tanzania kuna kila sababu ya sote kuonekana tumeshikamana hata kama mshikamano huo ni wa kinafiki na unawanufaisha zaidi mafisadi.Ndio maana basi nchi wafadhili zilikuwa zikiwakalia kooni watawala wetu kuhusu upatikanaji wa suluhisho la kudumu huko Zanzibar,ambapo hatimaye CCM kwa shingo upande (na licha ya ngebe za akina Makamba) leo hii tunashuhudia serikali ya umoja wa kitaifa huko Zanzibar.

Of course,hali ya kutoelewana huko Zanzibar ilikuwa serious sana hasa kutokana na vurugu za uchaguzi zilizopelekea mauaji ya watu kadhaa,ukweli unabaki kuwa msimamo thabiti wa chama kikuu cha upinzani visiwani humo,yaani CUF,kutotambua matokeo ya chaguzi mbalimbali,sambamba na kelele walizopiga kwa jumuiya ya kimataifa ndivyo vilivyopeleka leo hii kuwepo serikali ya umoja wa kitaifa.

Kwahiyo wanaohoji umuhimu wa wabunge wa Chadema kususia hotuba ya Kikwete wanapaswa kuelewa kuea msimamo imara sambamba na matendo yanayothibitisha msimamo huo yanasaidia kuleta mabadiliko yanayokusudiwa.Leo pale Dodoma kulikuwa na wawakilishi wa nchi na jumuiya mbalinbali za kimataifa.Vyovyote itavyokuwa,wameguswa na tukio hilo ambalo kwa hakika limetia dola utawala wa Kikwete.Baadhi ya nchi hizo ni wafadhili ambao bila wao basi mambo yanakuwa si mambo.

Lakini jingine la muhimu ni kufikisha ujumbe kwa Kikwete na serikali yake (including vyombo vya dola na Tume ya Uchaguzi) kuwa zama za "ndiyo mzee" zimefika kikomo.Hata kama Katiba inaendelea kuhalalisha sheria dhalimu (kama hiyo inayonyima fursa ya kupinga ushindi wa rais mahakamani) mwanya mdogo wa uhuru wa kidemokrasia kupingana pasipo kupigana unawezesha Chadema kuzalisha harakati mpya za mapambano dhidi ya udhalimu lakini pasipo vurugu au umwagaji damu.Kwa tunaotaka kuona Tanzania yenye kuheshimu na kuzingatia haki na stahili za Watanzania,kitendo cha leo cha Chadema kinafungua ukurasa mpya wa matumaini.Kadhalika,kitendo hicho ni hatua kubwa na muhimu ya kukua kwa demokrasia yetu kutoka vyama vinavyokubali yaishe hata pale penye uthibitisho kuwa vimejumiwa kwenye chaguzi,kwenda kwenye zama ambapo uchakachuaji wa chaguzi unaharamishwa hadharani tena kwenye live tv.Message delivered!

Ni wazi kuwa tukio la leo limemgusa Kikwete na serikali yake kama ambavyo limewagusa Watanzania wengi na jumuiya ya kimataifa.Yayumkinika kuwa inawezekana nguvu kubwa iliyotumika kuchakachua matokeo ya uchaguzi uliopita sasa itaelekezwa katika kuihujumu Chadema ili idhoofike na hatimaye kuachana na msimamo wake wa kukataa kumtambua Kikwete.Zitafanyika jitihada za kuwqgombanisha viongozi wa chama hicho kama ilivyokuww kww NCCR-Mageuzi ya Mrema.Kuna uwezekano pia wa Dokta Wilbroad Slaa kuzushiwa zengwe zaidi ya lile ya maisha yake binafsi.Lakini hayo yanaweza kupita pasipo madhara makubwa kwani hata Baba wa Taifa na wenzake walipokuwa wanahangaikia ukombozi wa Tanzania kutoka himaya ya mkoloni walikumbana na vizingiti hivyo.Haya ni mapambano kati ya wenye uchungu na nchi yao dhidi ya wale wanaotaka kuigeuza nchi yetu kuwa "shamba la bibi" na makao makuu ya ufisadi.

Sie Wakristo tunaamini kuwa mwenye haki ataanguka saba mara sabini ( hapa simaanishi kuanguka kama kule kwa Kikwete pale Jangwani) lakini mwishowe atasimama.Kukubali uchakachuaji wa kura kutapelekea matokeo ya ain moja tu: uchakachuaji zaidi.Historia inatufundisha bayana kuwa kukubali kitu kibaya hakusaidii hata chembe kitu hicho kibaya kugeuka kizuri au athari zake kupungua.Wanaoshauri Dkt Slaa na Chadema "wakubali matokeo" hawana tofauti na wanaoweza kusema tuache mapambano dhidi ya malaria au ukimwi kwa vile magonjwa hayo yamekuwepo miaka nenda miaka rudi.

Laiti Nyerere na mashujaa wengine wa mapambano dhidi ya mkoloni wangepatwa na mawazo hayo ya "kukubali yaishe" leo hii tungeendelea kuwa chini ya mkoloni ( I know kuna watakaosema bora mkoloni kuliko fisadi.Mie nasema ukoloni na ufisadi ni mbaya kama ilivyo kwa kansa na ukimwi.Hakuna cha nafuu,wote ni maadui wanaostahili kuangamizwa).Na laiti Nyerere "angekubali yaishe pale Nduli Idi Amini alipotuvamia,basi huends leo tungekuwa sehemu ya Uganda chini ya dikteta Idi Amini au mrithi wake.

Giving up is not an alternative.Mapambano ya kudai haki (kwa amani) lazima yaendelee.Waingereza wana msemo kwamba kukubali kitu pungufu kwa minajili ya bora liende hatimaye hupelekea kupata kilicho pungufu zaidi ya kilichostahili kupatikana.Kadhalika,hatua zote za mabadiliko huanza kwa hatua chache na pengine ndogo lakini zenye impact na hatimaye kutengenrza mazingita mazuri kwa hatua kubwa zenye impact kubwa zaidi na pengine zenye kuweza kuandika historia mpya.Vilevile,actions speak louder than words.Na hiyo imethibitka leo kwani japo Chadema walishatangaza kuwa hawatomtambua Kikwete uzito wa tamko hilo haukuwagusa wengi kulinganisha na tukio la leo la kususia hotuba ya Kikwete.

And by the way,hotuba hiyo ilikuwa na tofauti gani na hotuba lukuki alizotoa wakati wa utawala wake 2005-2010?Hivyo vipaumbele sijui 13 (or were they 19) tulishavisikia kwenye kampeni za 2005 na zikarudufiwa kwenye kampeni za mwaka huu.Kama kuna yeyote aliyechukulia vimpaumbele hivyo seriously all I can say asubiri muda si mtefu atabaini "imekula kwake" as they say in the streets.

KULIKONI UGHAIBUNI: Uamuzi wa Chadema Kususia Hotuba ya Kikwete Bungeni Dodoma

Thursday, November 18, 2010

WABUNGE WA CHADEMA NA KUAPISHWA MIZENGO PINDA.

CHADEMA hawatahudhuria hafla ya kumwapisha Mh. Pinda na pia hawatahudhuria hotuba ya Jakaya Kikwete.

Ufafanuzi zaidi umetolewa kuwa CHADEMA haijatamka kuwa haimtambui Kikwete kama Rais wa Tanzania bali HAWAYATAMBUI MATOKEO YA UCHAGUZI YALIYOMPA KIKWETE MAMLAKA YA KUWA RAIS. Kwa tafsiri rahisi ni kuwa Kikwete hana tofauti na wale marais wanaotumia mbinu mbalimbali kuupata urais bila ridhaa ya wananchi wanaowaongeza, amewekwa madarakani na tume ya uchaguzi lakini siyo wapiga kura.

CHADEMA haiongelei matokeo ya kura za ubunge kwa vile sheria inaruhusu kuhoji matokeo ya ubunge kwenye vyombo vya kisheria, kwa hiyo CHADEMA inategemea kuhoji matokeo ya kura za ubunge katika majimbo kadhaa. Kwa upande wa Urais ni tofauti kwa vile sheria hairuhusu kuhoji matokeo ya Urais mara tume ya uchaguzi ikishayatangaza. Kwa hiyo jitihada pekee inayoweza kutumika ni ya kisiasa.

CHADEMA hawatahudhuria matukio yote mawili kama njia mojawapo ya kuonesha kutokuridhika na kile kilichofanywa na tume ya uchaguzi ya kuhujumu demokrasia.

WABUNGE WA CHADEMA NA KUAPISHWA MIZENGO PINDA.

Thursday, October 28, 2010

Namuunga Mkono DR Slaa Asema Prof Lipumba wa CUF

Mgombea Uraisi kwa tiketi ya chama cha wananchi CUF amesema anamuunga mkono
yule wa CHADEMA DR W P SLAA , Kwahiyo amewasihi wananchi wampigie kura dr
slaa kama wasipompa yeye ila kasema yeye ni kama Mlima wakati DR SLAA ni
Kichuguu ameyasema hayo katika Mdahalo maalumu unaorushwa na ITV Moja kwa
moja sasa hivi

Gonga hapa kufuatilia Mjadala Huu
Namuunga Mkono DR Slaa Asema Prof Lipumba wa CUF

Monday, October 25, 2010

NUKUU ZA DR WP SLAA


  1. Monduli wanaishi maisha magumu.
  2. Tanzania bila CCM inawezekana, na kuendelea kukaa na CCM ni maafa makubwa.
  3. Kama ningesema uongo kuhusu ufisadi wa JK na waswaiba wake, mbona sichukuliwi hatua?
  4. Ukitukanwa, angalia, puuzia na uondoke. Ukipigwa kofi, mgeuzie na la pili...!
  5. Sipendi kwenda ikulu huku damu zikimwagwa, au kuwaacha watanzania wakiwa vilema kwa ajili yangu...!
  6. Nipo tayari kula mihogo ikulu, ili mtoto wa tanzania asome...!
  7. Siendi kuwa raisi wa Afrika Mashariki, bali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...!
  8. Kodi ya saruji kutoka Tanzania ni 18%, Kenya 15% na Uganda 16%....! Eti ndio makubaliano yaliyowekeana kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki...!
  9. Ninazo nyaraka kuwa serikali ya Tanzania imefanya partial payments huko Canada kwa ajili ya mabango ya CCM...!
  10. Sikatai kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki, lakini lazima tufanye maandalizi kuwapatia watanzania elimu itakayowawezesha kuingia kwenye ushindani...!

Sikiliza Mdahalo wa DR W P SLAA ITV

Mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA, Dr. Slaa, amefanya mdahalo ITV, kama ilivyotangazwa kwa siku kadhaa. Mimi kama mwalimu naiheshimu sana midahalo, kwani ni njia madhubuti ya kuelimishana, na katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi, ni njia madhubuti ya kuwaelewa wagombea. Namsifu Dr. Slaa kwa kujitokeza mbele ya umma namna hii, na nawashutumu wale wote ambao wamekataa kushiriki midahalo. Sikiliza mdahalo huu wa ITV na Dr. Slaa hapa:

GONGA HAPA KUSIKILIZA

Saturday, October 23, 2010

MDAHALO WA DR SLAA MOVEN PICK LIVE

Nipo ukumbini hapa DR SLAA na Mbowe wameshaingia Hotelini pamoja na viongozi wengine wa chadema kama kitila mkumbo na mabele marando maandalizi yanaenda vizuri kwa walinzi kukagua vitu kadhaa vya kiusalama , mafundi wa ITV wakijaribu mitambo yao pamoja na maongezi ya hapa na pale - hapo nje kuna tsh za dr slaa , ilani ya chadema pamoja na vitabu kadhaa vilivyoandikwa na vijana vinavyohusu maisha ya dr slaa pamoja na kingine kinachojaribu kumfananisha dr slaa na nyerere kutokana na matukio na matendo

GONGA HAPA KUFUATILIA
MDAHALO WA DR SLAA MOVEN PICK LIVE

Thursday, October 21, 2010

DR W P Slaa Kujibu Maswali Live ITV

Jumamosi ijayo, yaani Oktoba 23 ni siku muhimu kwa sababu Mgombea Urais wa
Chadema, Dk. Willibrod Slaa atajibu maswali ya wananchi moja kwa moja (live)
kupitia ITV Televisheni, kuanzia saa moja jioni hadi tatu usiku. Mwambie
rafiki yako na wadau wote wa uchaguzi wasiokuwa kwenye mtandao huu, kwa njia
ya simu au ujumbe mfupi wa maandishi, ni wakati murua wa kumuuliza maswali
na kumbana kujua anataka kuifanyia nini hasa nchi hii, maana midahalo ndio
kama hiyo ya urais hatuoni kama itakuwapo tena.
Kila la heri wote, na nawatakia kazi njema.

FUATILIA HABARI HII HAPA
DR W P Slaa Kujibu Maswali Live ITV

Sunday, October 17, 2010

SLAA ATISHA KAHAMA LEO JIONI

Slaa alikuwa kahama leo jioni atisha, watu waliminika kwa walee ambao ni
wakristo ungesema yesu amerudi.alijaribu kuwatuliza watu wamsikilze kwanza kabla
ya ushabiki kwani ushabiki huishia hapa uwanjani.kama kawaida yake alianza na
secta ya madini jinsi ufisadi ulivyoathiri secta hii.
ni mara ya ya kwanza kumwona slaa hadharani ila watu walivyomiminika uwanjani
pale na wakipiga kura atashinda kwa kishindo.

SLAA ATISHA KAHAMA LEO JIONI

Saturday, October 16, 2010

MGOMBEA URAISI WA CHADEMA DR W P SLAA ALIPOFIKA TABORA LEO

Dr Slaa ameingia Tabora mjini saa 11:50 jioni,
amepokelewa kwa bashasha kubwa na wananchi wa Tabora...
Mshehereshaji ajapoteza muda, na kumkaribisha Dr Slaa Jukwaani..
Dr anaanza kwa kuomba samahani kwa kuchelewa kufika akitokea Urambo, na wananchi kuridhia kumsamehe...
Huku akiwa anaonekana anaharaka sana, anaanza kwa kumwaga sera moja kwa moja..
Ameanza kwa kutoa ahadi ya kupunguza kodi ya vifaa vya ujenzi, na kufafanua kwa kina.. Ila muda ndo hautoshi..
Huku akionekana ni mwenye afya tele..
Anaelezea pia anaufahamu sana mji wa Tabora, amesomea hapa, seminari ya Itaga, na Kipalapala, anashangaa kuona mji aliouacha umezidi kudidimia kiuchumi, na kimaendeleo...
Anaendelea na sera ya ahadi ya kutoa elimu ya bure kwa kila mtoto anaeenda shule..
Anaendelea kuvuta hisia za watu wa hali ya chini, kwa kutoa pia ahadi ya kutetea wanyonge na mali zao...
Muda unazidi kwenda kasi, huku giza likianza ingia, wananchi nao wanaendelea kua wavumilivu kumsikiliza...
Anamwita Mgombea ubunge jimbo la Tabora Mjini, na kumtambulisha ndugu Gwikima, na watu kumhaidi kua watampa kura zao...
Baada ya hapo anamwita mke wake Bi josephine na kumtambulisha mbele ya wananchi na kumpa kipaza sauti ajitambulishe mwenyewe.. Wananchi...
Huku akionekana mwenye haraka, anamponda mgombea wa CCM, kwa kukiuka muda, na kuwaomba wananchi waendelee kumsikiliza hata mpaka saa 5 usiku, huku akionekana jasiri, anasema yupo tayari kujibu kwa tume..
Anamaliza kwa kuwapa wananchi somo la uraia na wasifanye makosa octoba 31..
Huwezi amini, wananchi wanasukuma gari la Dr Slaa , gari likiwa limezimwa, hakika wananchi ni Wengi sana..
Mkutano unaisha muda huu..

GONGA HAPA KWA HABARI ZAIDI

Tuesday, October 12, 2010

CHAGUA JOSEPH MBILINYI CHAGUA CHADEMA MBEYA

Mr II atia fora mdahalo wa uchaguzi mkuu Mbeya
Sehemu ya wakaazi wa jiji la Mbeya wakisikiliza mdahalo huo
Mgombea ubunge wa jimbo la Mbeya mjini kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) Joseph Mbilinyi a.k.a MR.II akiingia ndani ya ukumbi wa Mkapa jijini Mbeya kwa ajili ya kushiriki mdahalo ulioandaliwa na asasi za kiraia mkoa wa Mbeya (MBENGONET) kwa ufadhili wa asasi za kiraia Tanzania,huku akishangiliwa kwa nguvu sana
Mratibu wa midahalo mikoa ya nyanda za juu kusini kutoka asasi za kiraia Tanzania Bw Sisila Ngalemwa (Kulia) akijaribu kuwatuliza wananchi waliofurika katika ukumbi wa Mkapa Mbeya kumsikiliza mgombea ubunge wa Chadema Joseph Mbilinyi a.k.a MR II katika mdahalo huo ulioandaliwa na asasi za kiraia mkoa wa Mbeya (MBENGONET) Vijana wakijitolea kumtoa nje ya ukumbi wa mdahalo mmoja kati ya mashaiki wa msanii Joseph Mbilinyi a.k.a MR II aliyeshindwa kujizuia kushangilia kwa staili ya kutaka kumshika mkono msanii huyo wakati akijinadi mbele ya wananchi katika mdahalo wa wagombea ubunge jimbo la Mbeya mjini. MR.II (chadema)ni mmoja kati ya wagombea watano wa ubunge jimbo hilo.
Wapenzi na mashabiki wa msanii Joseph Mbilinyi a.k.a MR II na wale wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) jijini Mbeya wakiwa wamemzunguka msanii huyu nje ya ukumbi wa Mkapa baada ya kutoka kushiriki mdahalo wa wagombea ubunge jimbo la Mbeya mjini
Picha zote na Francis Godwin

Saturday, October 2, 2010

UJUMBE KWA WAPIGA KURA WOTE

Watanzania wasiotaka mabadiliko na maendeleo kwa nchi yao wataichagua CCM, lakini ikumbukwe kuwa ni hiyohiyo CCM iliyotufikisha hapa kwenye umasikini huu mkubwa tulionao. Ni hawahawa walioshindwa kudhibiti mfumuko wa bei. Ndio hawahawa wanaotuletea uchungu na shida katika nchi yetu wenyewe. Wakoloni Weusi, ndugu zetu,jamaa na rafiki zetu wa tangu udogoni.Wananchitwendeni tukapige Kura kisha tuzilinde kura hizo dhidi ya madhalimu. Tusikae jirani ya vituo vya kupigia kura ila mbali na eneo la kupigia kura na kuchukua tahadhari kwa yeyote atakayekwenda eneo la kuhesabia kura baada ya muda wa mwisho wa kupiga kura hasa kipindi cha kuhesabu kura hizo. Najua Polisi watamwagwa kuhakikisha mmerudi majumbani nafasi ambayo wataitaka sana, jigaweni katika zamu zenu kulinda haki yenu mpaka kieleweke, msiamini mawakala pekee nao ni binadamu, kila mmoja awe mlinzi wa kura yake. Je wataweza kutuhonga sote?

Kama kuumia kwa miaka mingine mitano tutaumia sote na kizazi chetu. Tusifanye makosa tena

Tuesday, September 14, 2010

Ahadi za DR W P Slaa Kwa Watanzania

1.Kujenga nchi isiyo na ufisadi

2.Kufufua Tanganyika ili irejee mezani kujadili muungano na Zanzibar

3.Kufufua uchumi wa nchi kwa kutumia rasilimali zilizopo

4.Kukata asilimia 20 ya mshahara wa rais

5.Kupunguza mishahara ya wabunge kwa asilimia 15

6. Kuweka Mwenge wa Uhuru Jumba la Makumbusho

7. Kutoa huduma bora za afya bure

8. kufuta kodi ya vifaa vya ujenzi

Fuatilia zaidi hapa

Ahadi za DR W P Slaa Kwa Watanzania

Monday, September 13, 2010

TUNAHITAJI MDAHALO KABLA YA UCHAGUZI MKUU 2010

Nalileta kwenye jukwaa suala la mdahalo wa viongozi wa vyama vya siasa katika ngazi ya rais kwa mwaka huu wa uchaguzi. Tuliona mara ya mwisho mwaka 2000 wakati BBC walipoanda mdahalo kati ya maalim seif wa CUF na Mheshimiwa Karume (CCM).

Mdahalo unawapa fursa wananchi kusikia moja kwa moja toka kwa wagombea katika kunadi sera zao lakini pia kujibu maswali ya wananchi moja kwa moja, tofauti na ziara za viongozi hawa mikoani ambako huwa hawamfikii kila mlengwa ama kukata kiu ya wananchi ambao ndio wapiga kura wakubwa.

Wananchi wakati mwingine hawapati hata nafasi ya kuwaona ama kuwasikia viongozi na wagombea katika nafasi mbali mbali za uchaguzi zaidi ya wawakilishi wao ambao mara nyingi wanakwenda kwa minajiri ya kuwashawishi kuwapigia kura bila kuwaeleza ni namna gani watatua matatizo ya taifa ama wamefanikiwa kwa kiasi gani katika mipango iliyopo.

Mdahalo ni njia mbadala ya kuongea na wananchi kwa kujibu mawali yao na kuwapa nafasi ya kupima sera za vyama vyote kupitia mahojiano ya moja kwa moja. Ni njia pia ya kuwakosoa viongozi moja kwa moja pale wanapotoa ahadi ambazo hazitekelezeki.

Naomba tuchangie hili na namna gani tunaweza kuinfluence lifanyike kwa mwaka huu. Kumbuka kuwa mwaka 2005 Hamza Kasongo akishirikiana na Channel Ten waliamndaa mdahalo ambao ulikuwa ufanyike Agosti 27, 2005 ambapo CUF, TLP, CHADEMA, na NCCR-Mageuzi walikuwa wamekubali kushiriki lakini CCM walikataa kushiriki na hivyo kufanya mdahalo huo kuota mbawa.

Kama kuna chama kinakataa ama kitakataa kushiriki mdahalo huu basi kitatoa nafasi kwa wananchi kuamua kutokana na sababu zitakazokuwa zimetolewa.

NAWAKILISHA

TUNAHITAJI MDAHALO KABLA YA UCHAGUZI MKUU 2010

Sunday, September 5, 2010

Mambo Kumi Muhimu Kuhusu Dk Willibrod Peter Slaa

Mambo Kumi Muhimu Kuhusu Dk Willibrod Peter Slaa

Dk Willibrod Peter SLAA

1. Anachokisimamia

• Dk Slaa anasimamia maadili, uadilifu, uamakini na uwajibikaji katika uongozi wa nchi na utendaji serikalini.

• Dk. Slaa anaamini kuwa Watanzania wanaweza kuleta mabadiliko wanayoyataka wakipata uongozi bora na thabiti.

2. Kuzaliwa, elimu ya msingi na sekondari

Dk Slaa alizaliwa tarehe 29 Oktoba 1948 katika Wilaya ya Karatu. Alipata elimu ya msingi katika shule za Karatu na Kwermusi (Mbulu) kati ya mwaka 1958 na 1965. Alisoma elimu ya sekondari katika Shule za Dung’unyi Seminari na Itega Seminari kati ya mwaka 1966 na 1971.

3. Mafanikio ya Dk Slaa Kielimu na Kitaaluma

Dk Slaa ana shahada na stashahada zifuatazo

• Shahada ya Uzamivu (PhD ) katika Sheria ya kanisa kutoka Chuo Kikuu cha St. Urban, Rome

• Stashahada ya Theolojia kutoka Kipalapala Seminari

• Stashahada ya falsafa kutoka Kibosho Seminari

• Stashahada ya Afya ya Macho kutoka Kituo cha Kimataifa cha Macho

4. Mafanikio ya Dk Slaa Kikazi na Kitaalamu

Dk Slaa amefanya kazi katika maeneo na sehemu mbalimbali. Baadhi ya nyadhifa alizoshika na kazi alizofanya ni hizi zifuatazo:

• Mkurugenzi Mtendaji, Chama cha Wasioona Tanzania, 1992-1998

• Katibu Mkuu, Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), 1985-1991

• Mkurugenzi wa Maendeleo (Jimbo Katoliki la Mbulu), 1977-1979 na 1982-1985.

• Padri wa Kanisa ikatoliki kuanzia 1977 hadi 1991.

5. Vitabu alivyoandika

• Utimilifu wa Msichana (1977)

• Utimilifu wa Mvulana (1977)

• Expediency and exigency Liturgical Legislation (1981)


6. Ufasaha katika lugha nane (8)

Dk Slaa anajua kuzungumza na kuandika lugha nane za kimataifa zifuatazo: Kiswahili, Kiingereza, Kilatini, Kiitaliano, Kijerumani, Kihispania, Kireno na Kifaransa.

7. Uzoefu wa Dk Slaa Kisiasa

Dk Slaa ana uzoefu wa muda mrefu katika shughuli za kisiasa. Baadhi ya nyadhifa alizoshika ni hizi zifuatazo:

• Mbunge wa Karatu kwa miaka 15, kutoka 1995 hadi 2010

• Katibu Mkuu wa CHADEMA, 2002 hadi sasa

• Makamu Mwenyekiti Taifa wa CHADEMA, 1998-2002

• Mjumbe wa Kamati Kuu na Baraza Kuu wa CHADEMA kutoka 1995 hadi sasa

8. Uzoefu wa Dk Slaa Kitaifa na Kimataifa

Dk Slaa ana uzoefu mbalimbali kitaifa na kimataifa kama ifuatavyo

• Mjumbe wa kuwakilisha Bunge la Tanzania katika Bunge la Afrika, Carribean na Pacific-EU (ACP-EUC Joint Assembly), 1996-2000

• Mjumbe Kamati ya Uongozi (ACP-EU Joint Assembly)

• Mjumbe katika Bunge la SADC kutoka 1998 hadi 2010

• Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge la SADC (Inter Parliamentary Cooperation and Capacity Building Committee) kutoka 1998 hadi 2010

• Naibu Kiongozi wa Kamati ya Upinzani Bungeni, 2006-2010

• Mwenyekiti, Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, Bunge la Tanzania, 2008-2010

9. Mafanikio kisiasa na kiutendaji

• Dk Slaa amekuwa mbunge wa Karatu kwa miaka 15 mfululizo. Karatu ni moja ya wilaya hapa nchini zenye mafanikio makubwa ikiwemo miundo mbinu bora, maji na huduma nyingine za kijamii. Dr. Slaa anataka kutumia uzoefu wake wa miaka

15 ya ubunge wa Karatu kwa ajili ya taifa zima.

• Ndiye Katibu Mkuu aliyefanikiwa zaidi kuijenga CHADEMA. Kwa kushirikiana na viongozi wengine ameweza kuipitisha CHADEMA katika changamoto mbalimbali na kukifanya kuwa chama kilicho tayari kushika uongozi wa taifa.

• Bila kujali vitisho vya watawala aliibua rasmi kashfa za ufisadi mbaya kuliko zote zilizowahi kutokea hapa nchini zikihusisha wizi wa fedha za umma katika Benki Kuu. Madai yake mazito Bungeni yalimlazimisha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu nchini kutoroka nchini.


10. Baadhi ya vipaumbele vya Serikali itakayoundwa na Dk Slaa

• Kuanzisha mchakato wa kuandika upya Katiba ndani ya siku 100 baada ya kuunda serikali

• Kupambana na kuwashughulia mafisadi katika nafasi zote, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha fedha zote zilizoibwa zinarejeshwa na wahusika wanashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

• Kuhakikisha kuwa kilimo chetu kiwe bora na cha kisasa, chenye faida na kinachofikia viwango vya kimataifa katika kuvuna, kuhifadhi, kusafirisha na kuuza mazao mbalimbali.

• Kuhakikisha kuwa kila mtoto wa kitanzania anapata elimu bora katika ngazi zote.

• Kuanzisha utaratibu wa kuwalipa pensheni wazee wote wenye umri wa miaka 60 na kuendelea nchi nzima na kurekebisha mfumo wa malipo ya pensheni kwa wastaafu

• Kuanzisha utaratibu mpya wa upandaji mishahara kwa watumishi wa umma na wa sekta binafsi utakaohakikisha kuwa mishahara inapanda kadri gharama za maisha na mfumuko wa bei unavyopanda.

Chagua Mabadiliko,

Mchague Dk Slaa ili arudishe tunu za taifa letu: Uzalendo, Maadili, Uadilifu na Umakini.

BE AN ACTIVE FORCE TO CHANGE TANZANIA

Blame Tanzanians for their problems, not their leaders. Awkward? This might not be true as an ontological universal truth. However, it is a fact. As long as heaven and earth exists, the Tanzanian leaders would never change Tanzania for good. The people (of Tanzania) will. Leaders are a minority. The people are the majority. Until we the people constitute an active forces of change and ‘disturb’ the world as we have always inherited it, Tanzania will continue to remain worst. The word ‘disturb’ is necessary as a revolutionary catalyst. Disturbance is a stimulus to change. All throughout history a constituted cabal of few people (minority) had often impressed their wills on the rest of mankind. Until when ‘the people’ are willing to say ‘enough is enough’.

This is the mathematics of change: knowledge (existential understanding), plus rising-up (revolution) equals change. But how can a people change their lot when they do not even understand it? If the masses of Tanzania have come to the full knowledge of the existential corruption, oppression, dehumanization and neglect they endure from the few minority who have constituted leadership, the country would have had great mass uprising for change long ago.

A case in point is this: FISADI is under investigation for corruption. He was declared wanted and aught to be arrested. But the youths has taken to his defense, attempting to shield him from facing questions about his acts. Do these people even understand what they are doing to themselves. Whose money, if he did loot, has FISADI stolen. It is the people’s money. The same people that tend to prevent his arrest. Do they even get the fact that it is for their own interest that he should answer questions to the court? Perhaps not! We are often in denial of the corrupt action of politicians because they are from our village towns, from my tribes or Region .

The consciousness of Tanzanians and indeed so many African nations are yet to ‘awaken’ to the new world of liberation, freedom and development. While the entire humanity and history is converging and harmonizing by the process of globalization, our nation is still blinded by tribalism and its bigotries, a force that retards our nationhood. Only a handful of the people of Tanzania actually grasp the degrading state of socio-political and economic life the country had fallen in. The masses feel it, but they do not understand it. Hardships, fear, oppression and years of hopelessness have made Tanzanians seemingly unaware that there could be something rightfully better. Few people actually understood the existential problem of police brutality and corruption. People are beaten and shot extra-judicially and nothing happens. It is a way of life. How many Tanzanians understood what it means that their human rights are protected by the law court. What does law court stand for the millions of common Tanzanians? Absolutely nothing.

We need a new kind of thinking in Tanzania. We need brave people who are morally ready to challenge the statues quo. It is only by challenging the oppressive establishments that the masses of Tanzanians would for the first time begin to see that they could actually have a different and better life. If Martin Lurther King Jr. did not dare racial oppression and segregation, there were so many blacks in America that never even understood that they were living suppressed life. After all that was how it has always been from time immemorial. The people of Tanzania need a different king thinking and mentality.

Throughout the ages, men and women who think differently change the world. In a world that often conform to socially accepted behaviors, lifestyles and cultures, to think different means being odd or strange. And those who are perceived to be ‘strange’ within this description are often ostracized, rejected or even killed. This is why it is not surprising that most of the world’s greatest minds were treated badly when they were alive. But after their death, the same world that condemned them might begin to see the light of the truth of what actually they stood for.

No one can positively change the world without being a radical of a sort. Socrates, Mahatma Gandhi, Martin Lurther King Jr, Mandela are few examples. These folks were adjudged radically dangerous by the world they lived in. Radical in the sense that they challenged the very essence of the social, racial, political and economic order of their times. These aforementioned orders had always existed before them as unchallengeable norms no matter how oppressive or unjust they were.

Challenging an existing social order is one of the most fearsome endeavor any human could embark on. We all know that the world is build on systems of injustice, oppression, lies and inequalities. And the powers that be are terminally toxic to new ideas, new creation, new innovations and most especially new world orders. In 5th/6th BC, Thales of Miletus tried to explain the world in the language of cosmology and physics. This did not go well to the world of his time. The Greek had always understood and explain the world in terms of myth and superstition. I could imagine what he went through trying to inform the people that lightning and thunders and sea waves could be explained with physics and not mythology. Similar to this is Galileo Galilei. He introduced a new scientific world view of the universe. This this not go well with the old ecclesiastical kerugmatik conception. Thus Galileo was seen as not just introducing something new to the old order but dangerous and was killed.

Socrates is known in history as one of the wisest men ever to live, he was a great moral thinker. His advocacy for justice, fairness and equality brought him down. He was seen as a thorn on the flesh of the Athenian political establishment--the statues quo--and for this reason he died by deadly poison called hemlock. How about Christ, he too challenged the statues quo. He stood for the poor and the oppressed and took the heat. He called those who maintain the oppressive statues quo: “You brood of Vipers”. And because of his open critiques of systemic ills, he was executed. Mahatma Gandhi single handedly stood up against the almighty imperial British empire. He was too daring, he was seen as a dangerous rebel and hunted down as one. The British wanted to keep the world at it was, Gandhi wanted the world to change. And this two forces clashed. Although Gandhi changed the world, he paid with his life.

Marin Lurther Kind Jr. did not want a world where racism and economic deprivation of obtains. He wanted a world where people are “judged by the content of their character and not by the color of their skins”. The old establishment felt challenged. Their feathers were being ruffled. Lurther was the enemy. His ‘dream’ was not welcomed. He was shot. But he changed the world order as it always existed even before his time. Nelson Mandela challenged apartheid. The apartheid system was among the most brutal and dangerous to dare. Mandela was ready. No jail term nor death treats could debar him from attempting to change a world that was build on structural injustice.

The point is this, it takes morally upright persons who are ready to die to change structural injustice. Anything less than that is a share noise and waste time. Why do men and woman in history try to change the world (ills) instead of leave it the way it has always been. It is because as humans, we are endowed with the capacity for moral reasoning. We have the sense of universal right and wrong. Some believe this moral sense in endowed by a moral divine being(God) and others believe it is just a share product of societal upbringing and education. As human, we have moral consciousness. This obliges us to act not just in our own interest but in consideration of others around me or even the generation not yet born. This is one of the cardinal factors that separates humans from other lower creatures in a very unique way.

Tanzanians need to vibrantly ‘disturb’ the old establishment. This can happen by the way of individual commitment to act as a moral agent of goodness and human progress. But it takes a heart to say stand for goodness and humanity when the gun of the old oppressive order in pointed at your head.

Thursday, August 19, 2010

Maswali na Majibu – Mgombea Uraisi Dr W Slaa ( CHADEMA )

Wanabidii Karibuni tena kwenye Mjadala wa Maswali na Majibu Kwa mara
ya Kwanza Tutaanza kufanya mahojiani na Wagombea Uraisi Leo tunaye Dr
W Slaa wa CHADEMA – CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO tukipata
Mawasiliano ya Vyama zaidi Itapendeza .
Kama kawaida ntaanza .

1 – Mh Dr Slaa Naomba kujua Historia yako kwa kifupi na kwanini
unafikiri CHADEMA imefanya chaguo Nzuri kwa kukupa wewe Jukumu la
Kuwashawishi wapiga Kura wakupigie wewe Mwezi Oktoba .

2 – Kama ukishindwa Katika Uchaguzi wa Mwaka huu uko tayari kukubali
matokeo na kumpongeza Mshindani wako ? Je Uko Tayari Kwa Kushindwa
Uchaguzi hata kwa asilimia ndogo ?

FUATILIA MJADALA HUU HAPA Maswali na Majibu – Mgombea Uraisi Dr W Slaa ...

KAULI MBIU YA DR SLAA

My guess ni kuwa kampeni hazijaanza so sidhani kama hiyo ni issue kwa sasa.
I thought it was said earlier kuwa hili jukwaa sio la chama kimoja au?
Naona at times tunajisahau na kuandika as if hapa ni pa mlengo mmoja tu. I
hope hii ni kutokana na positive munkari ambao baadhi yetu tunao ktk kutaka
kuleta maendeleo ya kweli NA sio ile michezo ya kisanii na kujifanya tupo
huku kumbe timevaa zile ngozi za nanii..

Gonga KAULI MBIU YA DR SLAA Kujadili