Showing posts with label Toka Bungeni. Show all posts
Showing posts with label Toka Bungeni. Show all posts

Saturday, November 20, 2010

WABUNGE WA CHADEMA WALIPOSUSIA HOTUBA YA JK

Wabunge wa CHADEMA wakitoka Bungeni

Chadema 'yaitikisa' nchi :NI KUTOKANA NA WABUNGE WAKE KUSUSIA HOTUBA YA JK

source : mwananchi

Na Waandishi Wetu

HATUA ya wabunge wa Chadema kutoka nje ya ukumbi wa bunge mjini Dodoma wakati Rais Jakaya Kikwete akianza kuhutubia, imetikisa nchi kutokana na wasomi, wanasiasa, viongozi wa dini na wananchi kuibuka na maoni tofauti.

Chadema wametangaza kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais wakidai kuwa kulikuwa na kasoro nyingi kwenye zoezi zima la uchaguzi na kwamba Tume ya Uchaguzi (Nec) ilikuwa imelenga kumbeba mgombea urais kutoka chama tawala.

Chadema, ambayo safari hii imeingiza watu wengi bungeni, imeamua kutumia njia hiyo ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais kushinikiza kuundwa kwa katiba mpya kutokana na katiba ya sasa kutotoa haki ya kupinga matokeo ya urais na inataka kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi.

Katika mahojiano ambayo Mwananchi iliyafanya jana katika mikoa tofauti nchini lilibaini kuwa wapo wanaoona kitendo hicho kilikuwa halali wakieleza uamuzi huo unaweka bayana msimamo wao wa kutokubaliana na mfumo uliomweka madarakani Rais Jakaya Kikwete , huku wengine wakikosoa kwa kusema kwamba hawakustahili kufanya hivyo mbele ya rais, wakitafsiri kuwa huenda hizo ni chokochoko za kuvuruga amani na utulivu nchini.

Wasomi, wanazuoni wanaounga mkono
Mhadhri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Abdallah Safari alisema kitendo hicho nio cha ni aibu kwa serikali ya Kikwete na Nec na kutaka kitafsiriwe kuwa ni kiashirio cha udhaifu katika uchaguzi na mahitaji ya tume hiyo.

“Ni silaha ya haki kwa kila mwanasiasa, ndio maana hata katika historia wabunge waliokuwa kwenye mabunge aliyokuwa akihutubia Fidel Kastro walikuwa wakitoka nje. La kujitakia halina majuto,” alisema Profesa Safari.

Mhadhiri mwingine katika Chuo hicho, Dk Azaveli Lwaitama alisema kitendo cha Chadema cha kawaida kwa kuwa siasa huambatana na suala la kisheria na hisia.

“Wao wamesema kuwa hawamtambua, lakini tayari rais wetu ameshaapishwa, hivyo kinachowafanya waseme hivyo ni hisia tu. Wanataka kuwaonyesha Watanzania kuwa hawakubaliani na matokeo ya urais, lakini kisheria hawawezi kufanya lolote kwa kuwa sheria inawabana,” alisema Dk Lwaitama.

Mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Tumaini mkoani Kilimanjaro ambaye aliomba jina lake lisitajwe gazetini alisema hakuna kosa lolote kwa wabunge kutumia njia hiyo kuonyesha dhamira yao ya kutokubaliana na matokeo ya Urais kwa kuwa hawana njia nyingine.

“Ibara ya 41 Ibara ndogo ya 7 ya katiba yetu inakataza matokeo ya urais kuchunguzwa baada ya kutangazwa na Nec… sasa kama umemfunga mshindani wako mikono, afanyeje kukuonyesha hakubaliani nawe,” alihoji.

"Katika hali ya kawaida ni jambo lisilowezekana kukubali goli ambalo unaamini limefungwa kwa mkono na kwamba hakuna mfumo unaomlazimisha mtu kumsikiliza Rais.”

Alisema haiwezekani Tanzania kujisifu kwa maendeleo ya kidemokrasia wakati katiba inazuia watu kuhoji uhalali wa matokeo ya urais, lakini katiba hiyo inaruhusu watu kuhoji uhalali wa matokeo ya wabunge na madiwani.

“Senegal kuna mahakama ya katiba ambayo inataka baada ya matokeo ya uchaguzi wa rais kutangazwa, ni lazima yathibitishwe na Mahakama ya Kikatiba… kunakuwepo kipindi maalumu cha kushughulikia malalamiko kabla ya Rais kuapishwa,” alisema.

Harod Tairo, mhadhiri wa sheria wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema kitendo cha Chadema hakikumfurahisha kwa sababu kilijenga taswira ya mgawanyiko na machafuko bungeni.

“Mimi nashauri CCM wakae chini na Chadema wazungumze tatizo lilikuwa wapi ili kuziba mianya itakayoweza kuleta machafuko kama yaliyotokea Zanzibar,” alisema Tairo na kuongeza kuwa kama serikali inataka kukuza demokrasia, ni lazima ikubali msimamo na kitendo kilichofanywa na Chadema.

Naye mhitimu wa shahada ya sheria wa Chuo Kikuu cha Tumaini, Iringa, Clement Kihoko alisema kitendo hicho ni kabisa japokuwa wanaweza kueleweka tofauti.

“Ni utaalamu wa kifalsafa na ni mambo ya kuangalia kwa umakini zaidi kwa sababu kama walivyosema awali kwamba hawamtambui Kikwete kama rais ,wangebaki kumsikiliza bungeni wangeonyesha kumuunga mkono na kumkubali,” alisema Kihoko.

Kihoko alibainisha kuwa katika tafsiri ya kifalsafa na hata falsafa ya sheria, kitendo walichokifanya chadema ni sahihi kabisa.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Morogoro (MUM), Ali Nassor alisema kitendo cha Chadema ni kuwaonyesha wananchi kwamba wako makini na wanatambua jukumu walilokabidhiwa na wananchi bungeni.
“Kwa kitendo hiki Chadema wanajiweka hadharani ili kupata wanachama wengi,” alisema Nassor.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tumaini, Dk Fairles Ilomo alielezea Chadema kuwa ni wapigania makabadiliko wachache waliojitoa kuwambwa msalabani kwa manufaa ya wananchi wengi.

Hata hivyo Dk Ilomo hakuunga mkono njia waliyotumia kupigania mabadiliko kwa kusema kuwa hawakupaswa kususia hotuba ya rais bali walipaswa kuwa wavumilivu na kutumia Bunge kufanya mabadiliko.

“Ni kitendo kilichoonyesha ujasiri kwa sababu kukiwa na viongozi ambao ni waoga watupu itachukua muda mrefu kufanya mabadiliko,” alisema Dk ILomo.

“Hayati Baba wa taifa Julias Nyerere alipoanza kupigania uhuru wakoloni walisema ni mvurugaji wa amani na kumweka rumande kwa saa kadhaa, lakini sasa tunafaidi matunda ya uhuru aliopigania. Vivyo hivyo wananchi watakuja kufaidi matunda ya mgomo Chadema."

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) walisema kitendo cha wabunge wa Chadema kinastahili kupongezwa kwa kuwa wameonyesha kwa vitendo kuwa uchaguzi ulikuwa na dosari.

Wanafunzi hao ambao wapo Jijini Tanga kwa ajili ya mazoezi walisema wabunge hao hawakutaka kuwa wanafiki mbele ya Rais Kikwete na badala yake wakaonyesha kilichokuwa mioyoni mwao.

“Walichofanya ni kupaza sauti ili dunia ielewe kwamba kulikuwa na dosari kubwa katika zoezi zima la kutangaza matokeo na hilo linaegemea kwa upande wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,” alisema Saida Hamis mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika chuo hicho.

Mawakili na Wanasheria
Mwanasheria wa Ngorongoro mkoani Arusha, Imanuel Saringe alisema: "Kisheria jambo hili halina tatizo na binafsi ninaaamini ujumbe wao umefika kwa walengwa bila vurugu au damu kumwagika."

Hata hivyo, alisema hutuba ya Rais Kikwete imekuwa ya ujumla sana na hivyo ni vigumu kuitathimini katika utekelezaji wa aliyosema.

Naye wakili mashuhuri mjini Moshi (jina limehifadhiwa) alisema kwa mtu mwenye mawazo finyu anaweza kusema kitendo cha Wabunge hao ni usanii fulani, lakini mtu upeo mpana atagundua Tanzania ina mgogoro wa kikatiba.

“Tuna tatizo la ubovu wa sheria nzima ya uchaguzi na kwa bahati nzuri sana wabunge hawa wameishia tu kutoka nje lakini tukiendelea na mfumo huu wa katiba unaokataza kuhoji matokeo ya rais, iko siku tutamwaga damu.”

Alisema: ”Tukiendelea na katiba hii tutajikuta tunakuwa na kiongozi aliyetangazwa kuwa ni rais, lakini si kiongozi aliyeshinda urais... kisheria anakuwa Ikulu, lakini kiuhalali hastahili na hapa ndipo mgogoro unapoanzia.”

Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali
Mkurugenzi mtendaji wa wanaharakati wa Agenda 2000, Moses Malaba alisema kitendo kilichofanywa na Chadema, kimefikisha ujumbe uliokusudiwa.

“Kisiasa walichofanya Chadema ni sawa; wamefanikiwa kufikisha ujumbe wa kutoridhishwa na mchakato wa uchaguzi kama walivyokusudia,” alisema Malaba lakini akaonyesha wasiwasi kama wananchi wataelewa lengo la chama hicho.

“Lakini wameenda mbali sana... wanachotaka wananchi waliowachangua ni kupata uwakilishi bungeni. Kwa sasa wanataka kujivunia kuwa na wabunge wengi.”

Mchungaji kiongozi wa Usharika wa Karanga wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Fred Njama alisema haoni kosa lolote kwa wabunge hao kufanya kitendo hicho.

“Kwa maoni yangu walichokifanya ni sahihi kwa sababu usipokubaliana na mtu huwezi kumsikiliza... ni vizuri hisia zako usizifanye ni siri ni vizuri ukazionyesha badala ya unafiki; mimi sioni tatizo hapa,” alisema.

Vyama vya siasa
Aliyekuwa mgombea urais wa TLP, Mutamwega Mugahwa alisema kitendo cha Chadema kinampasa Rais Kikwete kukaa chini na kutafakari tatizo lililopo na kulipatia ufumbuzi.

“Ningekuwa mimi ndio nimesusiwa Bunge, kiukweli nisingeweza kuchukulia kirahisi; lazima ningekaa na wahusika na kujua tatizo lililopo na kutafuta njia ya kulitatua kwa mujibu wa sheria za nchi,” alisema Mugahwa.
Alisema kwa mujibu wa katiba mtu ana uhuru wa kusikiliza na kutosikiliza ili mradi tu katika maamuzi yake asiingilie uhuru wa mtu mwingine.

Muasisi wa Chadema, Edwin Mtei alisema kitendo hicho binafsi kimempa faraja na kwamba huo ni mwendelezo wa kupinga katiba na kutaka ibadilishwe.

Mtei ambaye pia aliwahi kuwa gavana wa Benki Kuu nchini pia alimuunga mkono mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini, Jaji Amir Manento kuwa sasa ni muda wa kulilia katiba mpya.

Wananchi na makundi mengine
Mkoa wa Iringa
Baadhi ya wananchi wamewapongeza wabunge wa Chadema kwa hatua yao wakieleza kuwa msimamo huo unaweza kumfanya rais ajue kwamba wapo Watanzania wengi ambao hawana imani na utendaji kazi wa Nec.

Walisema Chadema wangeweza kuitisha maandamano na kufanya fujo kama ilivyowahi kutokea nchini Kenya, lakini kwa busara wametumia njia ya kususia hotuba kuonyesha kuwa hawamtambui rais kama alivyotamka katibu mkuu wa Chadema, Dr Willibrod Slaa.

Enock Mwasondole ambaye ni mkazi wa Mtwivila alisema umefika wakati ambao Nec inapaswa kuwa huru ili malalamiko yatokanayo na uchaguzi yapungue.

“Ni bora kususia kuliko wangeitisha mgomo na maandamano makubwa kama yaliyotokea Kenya. Rais asipuuzie hali ile badala yake anapaswa kuhakikisha Tume ya Uchaguzi inakuwa huru na kutenda haki,” alisema Mwasondole.

Mkazi mwingine wa Gangiolonga, Anania Mlelwa alisema huu ni wakati wa Tanzania kubadilisha katiba ambayo Iliandaliwa wakati wa chama kimoja na hivyo kusababisha tume hiyo kuwa mikononi mwa rais ambaye ni mwanachama wa chama kimoja.

“Katiba ndiyo tatizo kubwa; kama katiba ingelingana na wakati wa vyama vingi, tume isingekuwa ikilalamikiwa kwa kuwa isingekuwa chini ya rais,” alisema.

Naye rais wa Muungano wa Vyama vya Waandishi wa Habari, Keneth Simbaya alisema suala hilo ni la kiitikadi zaidi la kwamba wabunge hao wanapaswa kusikilizwa kwa kuwa yawezekana wana madai sahihi,

"Mara nyingi tuhuma za wanasiasa zinatakiwa kuangaliwa pande mbili kwa kuwa upande mmoja inaweza kuwa ni kweli na kwa upande wa pili inaweza kuwa si kweli, hivyo wabunge hao wasikilizwe ili kubaini wanachokilalamikia," alisema mwanahabari huyo.

Mkoa wa Mwanza
Uamuzi wa Chadema pia uliungwa mkono mkoani Mwanza ambako walisema unalenga kurejesha thamani ya kura.
Yohana Kagenzi, mkazi wa jijini Mwanza, alisema Chadema wameanzisha njia ya amani na ya kiungwana ya kudai katiba na tume huru ya uchaguzi ambayo haiwezi kusababisha umwagaji wa damu na kuzusha vurugu.

“Walisema kuwa hawayatambui matokeo, lakini serikali iliona ni jambo la kawaida nadhani njia hii sasa itamkera rais na kuamua kuwasikiliza. Kama hakuchakachua kura kwa nini asisikilize malalamiko yao,” alihoji Kagenzi.

Mkazi mwingine, Saida Mbwana alisema kitendo hicho kisipuuzwe kwa kuwa kinaweza kuwa na athari kubwa.
"Kama hawamtambua Rais Kikwete, basi hata serikali atakayoiunda hawataitambua, jambo ambalo litawakosesha maendeleo katika majimbo," alisema.

Mkoa wa Arusha
Arnold Kamde, Gervas Mgonja pamoja na Prosper Mfinanga ambao ni wakazi wa Arusha walidai ya kuwa kitendo hicho si tu kwamba kimeonyesha dalili za kukua kwa demokrasia nchini, bali pia kinatoa ujumbe kwa serikali ya Rais Kikwete kuwa Chadema hawakubaliani na matokeo ya urais kwa kuwa yalichakachuliwa.

"Sheria ya nchi inasema kuwa mara matokeo ya urais yakishatangazwa, hakuna mtu wa kuyapinga mahakamani. Sasa hiki kitendo si tu kwamba kinaonyesha kukua kwa hali ya demokrasia nchini bali pia ni ujumbe tosha kwa serikali ya Kikwete," alisema Mgonja.

Mfanyabiashara John Lyimo wa soko kuu la Arusha alipongeza wapinzani kwa kuonyesha hasira zao za kupinga matokeo na pia alimpongeza Rais Kikwete kwa kutoa hutuba nzuri.

"Mimi sina chama ila naona Chadema wamefanya vizuri tu na wamefanikiwa kufikisha ujumbe... rais aliongea vizuri na ameonyesha ameupata ujumbe," alisema Lyimo.

Mkoa wa Mbeya
Watu wengi walioongea na Mwananchi mkoani Mbeya waliunga mkono kitendo cha Chadema wakisema ujumbe waliotaka kumfikishia rais ulifika.

“Chadema wana ujumbe ambao wamewasilisha kwa serikali ya Rais Kikwete na ni haki yao kufanya hivyo,” alisema Jeremiah Osward ambaye ni mkazi wa Vwawa wilayani Mbozi.

"Kutokana na tamko lao la kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais, isingekuwa ni rahisi kwao kumsikiliza."

Mkazi wa Mwanjelwa, Zawadi Pangani alisema wabunge hao walikuwa sahihi kwa kuwa wanajua wanachokifanya ni kwa ajili ya maslahi ya wananchi na kwamba bila kufanya hivyo, haki haitaweza kupatikana.

Alisema inawezekana Chadema wana uhakika kuwa mgombea wao wa urais, Dk Slaa alishinda, lakini matokeo yakatangazwa kuwa ameshindwa, hivyo wana haki ya haki yao kufanya hivyo.

Mkoa wa Morogoro
Mmoja wa wakazi wa Morogoro, Anthony Chalamila alisema tukio hilo lilitarajiwa kwa sababu mgombea wao alitamka wazi kuwa hakubaliani na matokeo yaliyomtangaza Kikwete kuwa rais kwa madai yana walakin.

“Ni lazmima wasimamie na kuyatetea maamuzi yao, hivyo haingewezekani mtu ambaye walisema hawamtambui, wakae kumsikiliza,” alisema.

"Kama wangekubali kukaa na kumsikiliza rais akihutubia, ingeonyesha wazi kuwa hawana msimamo."
Mkazi mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Naye Simon alisema ni haki yao kufanya hivyo kwa kuwa walishatoa sababu za msingi za kutomtambua rais.

Wanaopinga kitendo cha Chadema
Wasomi na wanazuoni
Mbali na wengi kuunga mkono kitendo hicho, wapo ambao wanakipinga wakiongozwa na kiongozi wa zamani wa waasi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Profesa Ernest Wamba dia Wamba ambaye alisema si cha kiungwana.

Akizungumza katika mkutano wa wanafalsafa ulioandaliwa na Chama wa Falsafa Tanzania (Phata) uliofanyika jijini Dar es Salaam, Wamba alisema ni vizuri kama chama hicho kingekubaliana na matokeo hayo.

“Kawaida katika siasa changamoto ni jambo la kawaida, lakini kwa jinsi ulivyoniuliza kuhusu uchaguzi wa hapa Tanzania ni kweli umefanyika na mshindi kapatikana, lakini ingekuwa vizuri kama walioshindwa wangekubali tu matokeo,” alisema Profesa Wamba.

“Wabunge wameshakula kiapo, lakini wanasema hawatambui ushindi wa rais. Wana haki ya kuzungumza kwa kuwa hiyo ndio maana ya falsafa, lakini kwa hili la kiapo litawabana. Wangekubaliana na matokeo.”

Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali......

Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) limeelezea kutofurahshwa na kitendo kilichofanywa na Chadema na kukitaka kutafuta njia mbadala ya kutoa dukuduku lao.

Katibu wa TEC, Padri Antony Mkunde alisema vyama vya siasa na Watanzania kwa ujumla wanapaswa kutambua kuwa amani iliyopo haikushuka kutoka mahali popote bali ni mshikamano na busara katika uongozi.

"Mahali penye vurugu hata viongozi wa dini hawawezi kuhubiri; kinachotakiwa ni busara za viongozi wa nchi katika kuhakikisha amani na utulivu vinakuwapo," alisema Makunde.

Kwa upande wake Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania (MISATAN) imekielezea kitendo cha Chadema kuwa ni utovu wa nidhamu.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Rose Haji alisema viongozi wa Chadema ni kati ya viongozi waliokula kiapo walipoapishwa hivyo wasingepaswa kususia hotuba ya rais.

"Chadema wanatakiwa kumheshimu rais kama baba mzazi kwa sababu baba anapokosea huwezi kumdhalilisha mbele ya kadamnasi hivyo heshima inatakiwa pia katika suala la uongozi," alisema Haji.

Naye mwenyekiti wa taasisi ya kiislamu ya Imam Bukhary, Sheikh Khaliha Khamis alisema uamuzi wa Chadema utasababisha chuki dhidi ya chama hicho na wananchi waliowachagua.

Alisema kitendo hicho kinaonyesha dhahiri kuwa chama hicho hakiko tayari kukubali misingi ya demokrasia nchini na kuwatumikia wananchi.

Vyama vya siasa....

CCM imewataka wabunge wote waliokiri kutomtambua rais kujitoa haraka bungeni vinginevyo wataondolewa na azimio la bunge hadi watakapotambua uwepo wa rais.

Katibu wa kamati kuu ya CCM, John Chiligati alisema kuwa kila mbunge amekula kiapo cha kutii na kulinda katiba na kitendo cha kutomtambua rais ni uvunjaji wa katiba na hivyo wabunge hao wanatakiwa kujiondoa bungeni.

Chiligati alisema kitendo cha Chadema kuruhusu wabunge na madiwani wake kuendelea na kazi wakati hawamtambui rais na serikali ni unafiki wa hali ya juu.

Chiligati aliwataka wananchi kukataa tabia za viongozi wanaokataa matokeo kwa kuwa ni tabia inayoweza kusababisha matatizo na kuchochea vurugu nchini.

Katibu mwenezi wa NCCR-Mageuzi, David Kafulila alisema kitendo hicho hakikuwa cha kiungwana huku akikielezea kuwa ni sanaa ya maigizo.

Wananchi na makundi mengine
Mkoa wa Kagera
Aliyewahi kuwa waziri kwa nyakati tofauti katika awamu ya kwanza na pili Balozi Joseph Rwegasira amewaponda wabunge wa Chadema kwa kususia hotuba hiyo.

Mwanasiasa huyo alisema kitendo hicho kilikosa hekima kwa madai kuwa hawakujua sheria na taratibu.

Balozi Rwegasira, ambaye pia aliwahi kuwa mbunge wa Jimbo la Nkenge, alisema rais hawezi kususiwa na wabunge kwa kuwa kwa mujibu wa taratibu hata yeye ni sehemu ya Bunge na kuhoji iweje wasisusie Bunge zima.

Mkoa wa Kilimanjaro
Mwenyekiti wa Umoja wa Wafanyabiashar Wenye Viwanda na Kilimo (TCCIA) mkoani Kilimanjaro, Patrick Boisafi alisema kilichofanywa na wabunge hao wa Chadema hakikuwa cha uungwana na si mfano mzuri wa kuigwa.

“Kama hawataki kutambua matokeo yaliyompa Kikwete urais ina maana kwa miaka yote mitano hakuna siku watashiriki kutunga sheria Bungeni kwa sababu ni lazima mwisho wa siku iidhinishwe na Rais wanayemkataa,” alisema.

Alisema anachokiona ni ubinafsi wa Chadema kwamba kionekane ndicho chama kikuu cha upinzani nchini kama ilivyo CUF kwa Zanzibar ili siku za usoni wapate nafasi ya kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Bendera Isinika, ambaye mkazi wa Kaloleni anayefanya kazi ya uchoraji, alipinga kitendo cha wabunge wa Chadema kususia hotoba ya Rais Kikwete kwa madai kuwa hawakuwatendea haki wananchi waliowachagua kwa kuwa walipaswa kuwashirikisha kwanza kabla ya kufanya tukio hilo.

"Kama kuna tatizo la uchakachuaji wa kura wao walipaswa kutumia njia bora na sio kususia hotuba ya Rais Kikwete kwa kuwa wao tumewachagua sisi hivyo wangetuambia kwanza kama wanataka kutoka nje ya Bunge na si kuchukua maamuzi yao," alisema Isinika.

Mkoa wa Mbeya
Mkazi wa wilayani Mbozi, Imelda Ngarawa alisema kuwa hayo ndiyo matokeo ya upinzani kwa kuwa wanafikiri bungeni ni mahali pa kufanya sanaa, hivyo wameenda huko si kwa ajili ya kuwatetea wananchi bali kufanya sanaa.

Naye mkazi wa Tukuyu wilayani Rungwe, Fadhili Sikumoja alisema kuwa wabunge hao hawajafanya vizuri kwani rais Kikwetye bado ni rais wao kwani yupo madarakani na kwamba ilikuwa vizuri wangemsikiliza hotuba yake na kama wanahopja za msingi wangewasilisha wakati wa bunge lijalo.

Mkoa wa Morogoro
Mkazi wa Morogoro Leonard Mtete alisema kuwa hatua iliyoonyeshwa na wabunge wa chama cha Chadema haikuwa nzuri kwa vile inaweza kuwashushia umaarufu ulioanza kujijenga katika chama hicho.

Alisema kuwa hali hiyo pia inaweza kuionyesha jamii kuwa chama hicho ni chama cha washari na wagomvi tofauti na jinsi ambavyo watu walinavyokichukulia kuwa mapambano yake ni kidemokrasia na ya amani.

“Mimi nafikiri wabunge wa chadema wangetumia fursa waliyonayo bungeni kupambana kwa hoja na siyo kutoka kama walivyofanya wao” alisema mkazi huyo wa Morogoro.

Mkoa wa Iringa
Mkazi wa Iringa, Fanuel Kagambo alisema haoni kama msimamo huo unaweza kuwa na manufaa zaidi ya kuwaumiza Chadema na akawashauri kuanzisha njia nyingine ya kudai madai yao kwa vile kumkataa rais na kushiriki kupiga kura za kumthibitisha waziri mkuu aliyeteuliwa naye kuonaonyesha kumtambua.

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe anasemaje...
Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu jana, Mbowe alisema wanaowapinga au kuwa na mawazo tofauti na uamuzi huo, wasilitazame suala hilo juu juu na badala yake waangalia hoja wanazozitoa.

Alisema Chadema haikuamka tu na kutangaza kutomtambua rais, bali inazo sababu za msingi ambazo imeziweka bayana na imekuwa ikizieleza kila kukicha na kulaumu vyombo vya habari vinavyoshindwa kuainisha malalamiko au hoja zao kwa wananchi.

Mbowe alisema, msingi wa madai na malalamiko ya Chadema ni kutaka mazingira mazuri katika chaguzi zijazo wananchi wapate viongozi waliowachagua.

“Harakati ni kitu endelevu, michakato huzaa tunda la haki, miaka 19 sasa tangu siasa za vyama vingi ziruhusiwe, kumekuwa na vilio vingi toka kambi ya upinzani na kwa wananchi, lakini wenzetu walioko madarakani hawaonekani kusikia, tunatafuta lugha mbadala baada ya lugha ya upole kusikia” alisema.

Alisema, jambo wanalopigia kelele sio kilio cha Chadema pekee, bali ni kilio cha watanzania wote na akasema wanachofanya ni kutengeneza mazingira mazuri ya uchaguzi wa mwaka 2015.

“Yapo matatizo ya msingi na ni lazima yafanyike mabadiliko ya haraka na ya msingi, kwanza ni suala la katiba, tutahitaji kuangalia katiba kama chombo muhimu kinachoweza kumkomboa mtanzania na kupunguza vilio vya watu wengi” anasema.

Akizungumza kwanini wanayakubali matokeo ya wabunge na kuyakataa yale ya rais, Mbowe anasema, “Hili ni muhimu likawa wazi, sheria iko wazi kabisa, kwamba Rais akishatangazwa na Tume ya Uchaguzi hakuna anayeweza kubadilisha wala kwenda mahakamani, lakini ukiwa huridhiki na ushindi kwa wabunge au madiwani, sheria inaruhusu kwenda mahakamani kupinga” anasema.

Anasema, kutokana na sheria hizo ambazo anasema ni miongoni mwa mambo wanayoyapigia kelele wameamua kutumia njia hiyo ya kutomtambua rais ikiwa ni katika hatarakati za kutaka marekebisho katika sheria kandamizi kama hiyo ya kutokuwa na haki ya kupinga endapo wagombea wengine watakuwa hawajaridhishwa na ushindi wa mgombea mwingine.

Hata hivyo Mbowe alisema, Chadema inatambua kuwa kwa kufanya hivyo hakuwezi kubadilisha matokeo na hakuwezi kuzuia Kikwete kuwa rais au kuongoza serikali isipokuwa kwa kufanya hivyo kutafikisha ujumbe wao kwake Kikwete na serikali yake pamoja na dunia nzima.

Habari hii imeandaliwa na Joyce Mmasi, Nora Damian, Tumsifu Sanga, Fidelis Butahe, Hussein Kauli, Minael Msuya, Fredy Azzah, Michael Matemanga, Petro Tumaini, Hussein Issa, Aziza Masoud, Hidaya omary, Burhani Yakub,Tanga, Daniel Mjema, Moshi, Moses Mashalla na Mussa Juma,Arusha, Brandy Nelson, Mbeya, Tumaini Msowoya na Habel Chidawali,Iringa,Venance George, Morogoro, Phinias Bashaya,Bukoba, Geroda Mabumo na Masoud Masasi Dodoma na Frederick Katulanda, Mwanza.

Friday, November 19, 2010

Tanzania opposition says to push for electoral reform

Fri Nov 19, 2010

By Fumbuka Ng'wanakilala

DAR ES SALAAM (Reuters) - Tanzania's main opposition party said on Friday it would push for reforms of the country's electoral system after walking out of parliament during the president's speech to protest disputed elections.

The opposition said the October 31 vote was heavily rigged in favour of the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) party and want an independent electoral commission and constitutional amendments to allow presidential election results challenged in court.

President Jakaya Kikwete, who won re-election for a second and final term in office by 61 percent, delayed his speech for a few minutes on Thursday as lawmakers from Chadema party, which makes up the official opposition camp, marched out.

"The decision to walk out was made in line with our decision not to recognise results of the presidential election," Chadema's parliamentary chief whip, Tundu Lissu, told Reuters.

"We have reasons to believe that the results of the presidential vote were heavily rigged in favour of the incumbent president."

Chadema, whose presidential candidate Willibrod Slaa garnered 26 percent of the vote, said it would snub meetings officiated by the president.

Under the constitution, parliamentary and local council results can be challenged in the courts but final presidential results as announced by the National Electoral Commission cannot be challenged.

"The only legal recourse left is to register our displeasure and walk out. We know our action may not have any legal consequences, but we will not give legitimacy to the deeply flawed election process," Lissu said.

"We will hit the road and streets of Tanzania. We will explain to the people of Tanzania what happened."

ELECTORAL REFORM

Independent election observers said the electoral commission and government officials openly favoured the ruling party during the election process.

Lawmakers from the ruling CCM party, which has a two-third majority in the 335-seat parliament, heckled Chadema legislators as they walked out of parliament.

Members of parliament from other opposition parties did not join Chadema in the walk out.

One analyst said Tanzania's constitution, which was written more than three decades ago when the east African country was under one-party rule, had become obsolete.

"I think the need for a new constitution is more scaled up now than at any other time in the country's history," political commentator Deus Kibamba said in a phone interview with Reuters.

"To avoid a political crisis, the government should start the process of writing a new constitution that will take into consideration all the major changes that have occurred in Tanzania, including the introduction of multi-party politics in 1992."

In his speech on Thursday, Kikwete urged political leaders to work together to heal wounds that emerged after the election.

He outlined priorities of his government in the next five years, which include boosting economic growth, investing in agriculture, infrastructure and improving access to social services such as education, water and electricity.

He said his government would add 640 MW of electricity to the national power grid by 2015.

East Africa's second largest economy has energy demand close to 900 MW capacity, but produces less than 800 MW. Only 14 percent of its 40 million people are hooked to the grid, while demand grows by 10 to 15 percent annually.

Source: Tanzania opposition says to push for electoral reform | Top News | Reuters

Thursday, November 18, 2010

Kwanini wabunge wetu wamesusia hotuba ya Mwenyekiti wa CCM Dr. Jakaya Kikwete

SOURCE : http://www.facebook.com/WilbrodSlaa

Wabunge wetu wamechukua uamuzi mgumu sana, uamuzi ambao unataka ujasiri na uthubutu wa vitendo. Ni lazima tuelewe kuwa mgogoro uliopo siyo na Kikwete kama Kikwete, la hasha bali na mfumo uliomuingiza madarakani safari hii, mfumo ambao tunautuhumu kuwa haukuwa huru na wa haki. Uamuzi huu haukuwa wa chuki binafsi au kisirani dhidi ya Kikwete kama Kikwete, bali dhidi ya mfumo ulioundwa na kulelewa na CCM na ambao umetuonesha kuwa hauwezi na haupaswi kulelewa kwa muda mwingine wowote ujao.

Kuanzia wakati wa kutangaza matokeo tulitoa malalamiko yetu kwa Tume ya Uchaguzi ili waweze kuyafanyia kazi ili mshindi apatikane katika mazingira ya haki na uwazi. Tume haikusikiliza na ikaendelea na mfumo wake mbovu wa kutangaza matokeo bila kujali malalamiko yetu. Tukazungumza hadharani juu ya kutopatana kwa matokeo ya uchaguzi yanayotangazwa na tume na yale yaliyoko majimboni na kuomba tume wasitishe ili waangalie ushahidi tulio nao, tume haikusikiliza na matokeo yake wakamtangaza Kikwete kuwa Rais licha ya kwamba matokeo majimboni yalikuwa yanaashiria vinginevyo.


Ni muhimu kutambua kuwa ni rahisi kukubali matokeo ya Ubunge kwa sababu yanarasimishwa majimboni na yanaweza kupingwa mahakamani. Katika urais kimsingi ukiangalia Katiba utaona kuwa haijalishi nani kashinda kwenye kura, bali nani katangazwa mshindi. Tunachotuhumu sisi ni kuwa matokeo ya Uchaguzi yangetangazwa kama ilivyoahidiwa na Tume mwezi Machi yangeonesha wazi mshindi ni tofauti na yule aliyetangazwa. Lakini wao tume wakijua kuwa mara wakishatangaza hakuna mahakama inayoweza kuhoji wakafanya hila na haraka ya kutangaza matokeo ya Urais kwa kumtangaza Kikwete kuwa ni Rais.

Kama toka siku ya kwanza tulitoa malalamiko na zikapita siku tano bila kujibiwa wala kusikilizwa na baadaye tunatakiwa tukubali tu kwa vile "keshatangazwa" katika dhamira safi tunaweza vipi kufanya hivyo? Ugomvi wetu wa kisiasa (na siyo chuki wala uhasama binafsi) hauko zaidi na Kikwete bali natume iliyomtangaza. Na kwa vile yeye mwenyewe haoni matatizo katika tume au mfumo wetu wa uchaguzi tunaona kuwa aidha alitoa baraka zake au alikubali kunufaishwa na mfumo huo mbovu.

Hivyo, wabunge wetu kutoka nje ni kutuma ishara mbili: Kwanza, tunapinga mfumo wa kichakachuaji wa tume ya Uchaguzi uliomtangaza Kikwete kuwa Rais, na pili kwa vile Tume imeshindwa kutuonesha uwazi wa ushindi wa Kikwete tunashindwa kukubali kama ni mshindi halali. Ni mpaka pale uchunguzi huru wa kura utakapoonesha kuwa Kikwete kashinda kihalali ndipo tutakuwa tayari kumtambua ukiondoa uwezekano mwingine wa kuelewana.

Tukumbuke kuwa, kama uchaguzi huu ungeendeshwa katika hali ya uwazi, haki na ufanisi tusingefika hapa. CHADEMA siyo wa kulaumiwa katika hili wala wabunge wetu wasibebeshwe mzigo kwa hili; watu waliotufikisha hapa ni Serikali ya CCM na vyombo vyake ikiwemo Tume ya Uchaguzi. Wangeonesha weledi na kutokupendelea kwa wazi tusingefikia mahali pa kutulazimisha kuchukua hatua hizi ambazo kwa kila kipimo ni za wastani sana ukilinganisha na hatua ambazo tungeweza kuzichukua.

Nawasihi tuwaunge mkono wabunge wetu na uongozi wetu kwa kuwatia moyo kwani uamuzi waliouchukua ni uamuzi wa kijasiri lakini ulioweka historia katika Tanzania kuwa hatuwezi tena kusukumwa na kuburuzwa kwa kutumia nguvu ya taasisi au cheo cha mtu. Tuwatie shime na tusimame nao katika wakati huu wa kihistoria.

CHADEMA kumsusa Kikwete

Mbowe akataa kuzungumzia msimamo wao

na Mwandishi wetu

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), leo kinatarajiwa kutohudhuria sherehe za kuapishwa kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, pamoja na uzinduzi wa Bunge la 10 utakaofanywa na Rais Jakaya Kikwete.

Sababu za CHADEMA kutohudhuria uzinduzi wa Bunge na kuapishwa kwa Pinda, kunatokana na msimamo wao walioutangaza wiki iliyopita kuwa hawamtambui kiongozi huyo kwa sababu matokeo yaliyompa ushindi yalichakachuliwa.

Habari ambazo zilizagaa maeneo mbalimbali mkoani hapa zilibainisha kuwa CHADEMA hawatohudhuria uzinduzi huo wa Bunge, ili kushibisha hoja yao ya kutomtambua Rais Kikwete ambaye alipata ushindi kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka huu.

Tanzania Daima, limedokezwa kuwa msimamo huo wa CHADEMA, unamaanisha kuwa chama hicho hakitahudhuria shughuli zozote ambazo Rais Kikwete atakuwa mgeni rasmi.

Msimamo kama huo uliwahi kutolewa na Chama cha Wananchi (CUF), ambacho kiliwahi kutoyatambua matokeo yaliyowaingiza madarakani waliokuwa marais wa Zanzibar, Dk. Salmin Amour na Dk. Amani Abeid Karume.

CUF ilikataa kuhudhuria mikutano ya Baraza la Wawakilishi pamoja na ile ya Bunge sambamba na kutoshiriki kwenye shughuli mbalimbali za kitaifa zilizokuwa zikiongozwa na marais hao.

Tofauti na CUF, CHADEMA imetoa msimamo wa kutomtambua Rais Kikwete, lakini kimeweka wazi kuwa wawakilishi wake wataendelea kuwatumikia wananchi kulingana na sheria na Katiba za nchi.

Tanzania Daima, lilizungumza na msemaji wa kambi ya upinzani bungeni ambaye pia ni Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, kuhusu tetesi hizo na kusema hayuko tayari kuzungumzia tetesi bali aliwataka wananchi wavute subira, ili waone kama watahudhuria au hawatohudhuria.

Alibainisha kuwa hawezi kuzuia mawazo ya watu au maneno yao, lakini ukweli utajulikana wakati ukifika kama wabunge wa CHADEMA wataingia bungeni wakati Rais Kikwete akilizindua na kulihutubia Bunge.

“Taarifa za CHADEMA kutohudhuria sherehe hizo umezipata wapi?....mimi naomba uvute subira ili kujua ukweli wa tetesi hizo, wanaozieneza wanajua walikozipata...muda utaamua,” alisema Mbowe.

Tanzania Daima, lilidokezwa na watu walio karibu na wabunge wa CHADEMA kuwa msimamo wao ni kutohudhuria sherehe hizo, kwani wakifanya hivyo ni sawa na kwenda kinyume na msimamo wao walioutoa mwanzoni mwa wiki hii wa kukataa kumtambua Rais Kikwete.

CHADEMA inadai kuwa Kikwete alipata madaraka kwa sababu ya uchakachuaji wa kura uliofanywa na Usalama wa Taifa kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ili kumuwezesha Kikwete kuibuka na ushindi.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, leo asubuhi katika viwanja vya Ikulu Ndogo ya Chamwino, anatarajia kuapishwa kushika wadhifa huo baada ya kuidhinishwa na Bunge juzi.

CHADEMA yamwadhiri Ndugai

Yamtuhumu kumbeba Sophia Simba

na Salehe Mohamed, Dodoma

NAIBU Spika wa Bunge, Job Ndugai, juzi alianza kuonja machungu ya kiti chake baada ya kukaliwa kooni na wabunge wa CHADEMA kwa madai anakipendelea Chama cha Mapinduzi (CCM).

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, na John Mnyika wa Ubungo, walipinga kitendo cha mbunge wa viti maalum kupitishwa bila kupingwa kuwakilisha Tanzania katika Bunge la nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara (SADC).

Mnyika aliomba mwongozo wa Naibu Spika kuhoji ni kanuni ipi iliyotumika kumpitisha Simba ilhali wenzake walijieleza kwa lugha ya Kiingereza na baadaye kupigiwa kura.

Alisema kanuni za uchaguzi wa wabunge wanaokwenda kwenye vyombo vingine vya uwakilishi kifungu cha 5(2)c kinasema mgombea mmoja wa nafasi inayohusika wabunge watampigia kura za ndiyo au hapana.

“Mimi napinga Sophia Simba, kutoitwa kujieleza, kuulizwa maswali na kupigiwa kura, kinyume na kanuni ametangazwa na amepita bila kupigwa,” alisema Mnyika.

Akitoa mwangozo, juu ya jambo hilo Naibu Spika Ndugai, alisema Mnyika yuko sahihi, lakini alichelewa kutoa hoja na Spika wa Bunge, Anne Makinda ndiye aliyeanza mchakato wa uchaguzi kabla ya kumuachia kiti hicho.

Jibu hilo lilimfanya Zitto na Mnyika kupinga hoja hiyo na kuzua mjadala ambao ulimfanya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Federick Werema kuingilia kati.

Werema, alisema hoja iliyotolewa na Mnyika ni sahihi lakini haitoweza kujadiliwa au kubadili utaratibu uliofanyika kwa sababu ilichelewa kutolewa.

Alisema kuwa makundi mengine yalishafanya uchaguzi huo hivyo haitokuwa rahisi kwa Sophia Simba kuitwa kujieleza, kuulizwa maswali na hatimaye kupigiwa kura.

Maelezo hayo, yalipingwa na Zitto kwa madai kuwa kanuni zimekiukwa na Bunge haliwezi kuendeshwa kwa ukiukaji kanuni au upendeleo kwa chama fulani.

Mjadala wa kupinga jambo hilo ulizidi kushika kasi na kumfanya Mbunge wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge (CCM), kusimama kutoa taarifa kwa mujibu wa kanuni ya 5 (4) inayohusu mamlaka ya Spika.

Alisema kanuni hiyo, inamtaka mbunge ambaye hataridhika na uamuzi wa Spika kuwasilisha sababu za kutoridhika kwake kwa katibu wa Bunge, ambaye atawasilisha malalamiko hayo kwa Spika.

Chenge alibainisha kuwa vifungu vidogo vya (5) na (6) vinaeleza Spika atawajibika kuitisha kikao cha Kamati ya Kanuni za Bunge na kulijulisha Bunge kuhusu uamuzi utakaotolewa na kamati.

Aliongeza kuwa Spika au Naibu wake hawatakuwa wenyeviti wa kikao hicho, ili kutoa nafasi na haki kwa shauri husika kusikilizwa.

Aliongeza kuwa majibizano kati ya kiti (Spika au Naibu Spika) na baadhi ya wabunge kutokana na uamuzi wa Spika hayana nguvu.

Zitto aliinuka na kumjibu Chenge kuwa Kamati ya Kanuni za Bunge bado haijaundwa, hivyo hawawezi kuwasilisha taarifa ya kutoridhishwa kwake.

Akizungumzia kuhusu uadilifu kwa kiongozi wa Bunge (Spika, Naibu wake au wenyeviti wa Bunge), kwa kutumia kanuni ya nane, inayozuia upendeleo, Zitto alitaka Sophia ajieleze na apigiwe kura.

Mjadala huo ulihitishwa na Naibu Spika, Job Ndugai, ambaye aliwaonya wabunge wanaotaka kucheza na mamlaka ya Spika au Naibu Spika kujirekebisha mara moja, ili kuepuka adhabu.

Mjadala huo, ulisababishwa na uchaguzi wa wajumbe wa Bunge la SADC.

Aliongeza kuwa mabishano hayo yanapaswa yachukuliwe na wabunge wapya kwa umakini mkubwa hasa kwa kusoma sheria na kanuni za kudumu za Bunge.

Pamoja na Sophia, wajumbe wengine wa Bunge la SADC-PF ni Mohammed Habib Mnyaa (Mkanyageni-CUF), ambaye baada ya kutangazwa mshindi kwa kura 275 dhidi ya kura 47 za mgombea wa CHADEMA, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa.

Mwingine ni Mbunge wa Arumeru Magharibi, Goodluck Ole Medeye (CCM) aliyepata kura 180. Waliopiga kura walikuwa wabunge 324.

Wednesday, November 17, 2010

Lissu, Mnyika wamtikisa Spika

TANZANIA DAIMA

WABUNGE machachari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu (Singida Mashariki) na John Mnyika (Ubungo), jana walianza kumpa wakati mgumu Spika wa Bunge, Anne Makinda, kwa kumbana kwenye kanuni kwa kutaka awape ufafanuzi.

Akizungumza kwa kujiamini, Mnyika alikuwa wa kwanza kutaka mwongozo wa Spika, kwa kutaja kanuni ya 68 (7) ya Bunge inayozungumzia usiri wa kura lakini katika karatasi walizotoa kwa ajili ya kupiga kura za kuidhinisha jina la waziri mkuu zilikuwa na namba.

Mnyika alisema uwepo wa namba hizo kunaweza kumfanya mtu kujua nani alipewa karatasi namba ngapi na kura aliyopiga ili kumkubali au kumkataa mtu Fulani, hivyo hakutakuwa na usiri tena.

“Mimi nimepata karatasi yenye namba 278, hivyo ni rahisi mtu kujua kura yangu nilimkataa au kumkubali mgombea, hapa siri haitakuwapo, naomba mwongozo wako,” alisema.

Spika wa Bunge, Anne Makinda, alisema ni kweli kuwapo kwa namba hizo kunaweza kuathiri zoezi hilo lakini kwa sababu awali hakuna mtu aliyekuwa anajua jina la waziri mkuu mteule, uwepo wa namba hizo si tatizo, kwani umefanywa na mashine.

Alisema jina la yeyote lingeweza kuteuliwa na Rais Kikwete, hivyo Bunge lingefahamu jina hilo baada ya bahasha iliyoletwa na Rais kufunguliwa bungeni.

Lissu, naye alimbana Makinda kwa kutumia kanuni 53 (6)a, (6)c ambapo alisema endapo hoja itatolewa na serikali bila kupitia katika Kamati ya Kudumu ya Bunge, kiongozi wa upinzani bungeni atapata fursa ya kujadili hoja lakini Bunge halikufanya hivyo baada ya hoja ya kumuidhinisha Waziri Mkuu kutolewa.

Kabla ya kutoa mwongozo huo, Makinda, alitaka uchaguzi uendelee na kura zihesabibiwe, jambo lililozusha mzozo wa pande mbili (wabunge wa CCM na wale wa CHADEMA).

Hata hivyo swali hilo lilionekana kuwaumiza vichwa wanasiasa wengi, ambapo Spika wa Bunge la tisa Samuel Sitta, alilazimika kunyanyuka kwenye kiti chake na kwenda kwenye kiti cha Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuteta naye, huku akiwa na kitabu cha kanuni za Bunge.

Wakati Sitta akifanya hivyo, Ukumbi wa Bunge ulilipuka kwa shangwe za kumshangilia, jambo lililomfanya Makinda kusema kuwa angalau amelichangamsha Bunge kwa kuwa lilikuwa kimya kwa muda kidogo.

Wakati hayo yakitendeka, Makinda naye alikuwa akipokea ujumbe wa baadhi ya wabunge ulioonekana kumsaidia namna ya kutoa mwongozo kwa wabunge hao wa CHADEMA.

Baada ya matokeo ya uchaguzi kurejeshwa kutoka kwenye chumba yalikokuwa yakihesabiwa, Makinda alitolea ufafanuzi jambo hilo, ambapo alisema kuwa aliruhusu hoja hiyo kujadiliwa ambapo wa kwanza kuijadili alikuwa ni Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela.

Alisema baada ya Kilango kutoa mchango wake, alitoa hoja ya kutaka hoja hiyo isijadiliwe na kuungwa mkono na wabunge zaidi ya 10, hivyo hakukuwa na haja ya kumpa nafasi Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

Alisema kwa mujibu wa kanuni, hoja ikiungwa mkono na wabunge zaidi ya 10 haina haja ya kuendelea kujadiliwa, ndiyo maana hoja hiyo ilifungwa.

Aidha, alisema hoja yoyote iliyoamuliwa na wabunge na Spika akiifunga, hakuna mbunge atakayeruhusiwa kuizungumzia tena.

Baada ya maelezo hayo ambayo yalionekana kupingwa na wabunge wengi, hasa wa CHADEMA, Naibu Msemaji wa Kambi ya Upinzani, Zitto Kabwe, alisimama kutaka kuuliza swali, lakini Makinda alimnyima nafasi na kuendelea na utaratibu wa kuhesabu kura.

Katika hatua nyingine Lissu, aliteuliwa kuwa msimamizi wa zoezi la kuhesabu kura za kumuidhinisha waziri mkuu, jambo ambalo lilizusha shangwe na makofi mengi kutoka kwa wabunge wa CCM.

Shangwe hizo zilitokana na msimamo uliotolewa juzi na CHADEMA wa kutomtambua Rais Kikwete kwa madai kuwa matokeo yaliyompa ushindi yalikuwa ya wizi.

Wabunge wa CCM na watu wengi walitaka kuona kama Lissu atakataa kwenda kuhesabu kura kwa sababu jina la waziri mkuu, lilipendekezwa na Rais Kikwete ambaye CHADEMA haimtambui.

Hata hivyo Lissu alionekana akijadiliana jambo na viongozi wenzake na baadaye aliinuka kwenda kwenye zoezi hilo huku akishangiliwa na wabunge.

Pinda anatarajiwa kuapishwa kesho katika Ikulu ndogo ya Chamwino mjini hapa.

Tuesday, November 16, 2010

haa haaa tujenge nchi sasa mzee wangu.


Waziri Mkuu Mizengo Pinda akifurahia jambo na aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa walipokutana nje ya ukumbi wa Pius Msekwa bungeni jana mjini Dodoma. Pinda alikwenda kujumuika na wabunge wenzake wa CCM waliokuwa na kikao cha kumteua mgombea wa Naibu Spika kwa tiketi ya chama chao. Picha na Edwin Mjwahuzi

Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa

Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa

Mbunge wa Nyamagana ( CHADEMA ) Ezekia Wenje

Mbunge wa Nyamagana ( CHADEMA ) Ezekia Wenje.

Mnyika na David Silinde wakibadilishana mawazo


Mbunge wa Ubungo (CHADEMA), John Mnyika na Mbunge wa Mbozi Magharibi (CHADEMA), David Silinde

Monday, November 15, 2010

Mbunge wa jimbo la Mbeya kwa chama cha CHADEMA,Mh.Joseph Mbilinyi

Mbunge wa jimbo la Mbeya kwa chama cha CHADEMA,Mh.Joseph Mbilinyi akila kiapo hivi karibuni ndani ya jengo la Bunge,wakati mchakato wa kuapishwa Wabunge wateule ukiendelea.Picha kwa hisani ya Richard Mwaikenda.

Mbunge wa Kawe Mh. Halima Mdee


Mbunge wa Singida mjini Mh.Mohammed Dewji akibadilishana mawazo na Mbunge wa Kawe Mh. Halima Mdee katika viwanja vya Bunge jioni

Mhonga Said Rhuhanywa baada ya kutua Dodoma


Mbunge viti maalumu CHADEMA Mhonga Said Rhuhanywa baada ya kutua Dodoma

DR W P SLAA AKISALIMIANA NA MIZENGO PINDA

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akisalimiana na mgombea urais wa Chama Cha demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa furaha kubwa

Sunday, November 14, 2010

Mheshimiwa Dk Wilbrod Slaa

Katibu Mkuu wa Chadema na aliyekua Mgombea Uraisi kupitia chama hicho Mheshimiwa Dk Wilbrod Slaa akielekea kwenye mkutano maalum na wabunge wateule wa chadema kwenye Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma

Mkurugenzi wa masuala ya Bunge na Halmashauri wa Chama cha CHADEMA,John Mrema


Mkurugenzi wa masuala ya Bunge na Halmashauri wa Chama cha CHADEMA,John Mrema, akizungumza na waandishi wa habari Mjini Dodoma

Mbunge Zitto Kabwe akichangia hoja bungeni

Mbunge Zitto Kabwe akichangia hoja bungeni.

Mbunge wa Kawe, Mh. Halima Mdee

Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akisalimiana kwa furaha na Mbunge wa Kawe, Mh. Halima Mdee, Bungeni Mjini Dodoma

Saturday, November 13, 2010

Marando akubali matokeo

MWANANCHI GAZETI

Habel Chidawali, Dodoma
ALIYEKUWA mgombea nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kupitia Chadema, Mabere Marando, amekubali matokeo yaliyompa ushindi mpinzani wake, Anne Makinda wa CCM na kwamba, lakini anakwenda kujenga chama kwa ajili ya mapambano ya mwaka 2010.

Mabere alikuwa kwenye kinyanga’anyiro hicho na kubwagwa na Makinda anayekuwa mwanamke wa kwanza kuwa Spika wa Bunge la Tanzania tangu nchi ipate uhuru.

Marando alipata kura 53 sawa na asilimia 16.2 ya kura halali zilizopigwa, ambazo ni 327 huku Makinda akipata 265 sawa na asilimia 81.03, kura tisa ziliharibika.

“Nimeshindwa na ninamtakia kazi njema yenye ufanisi wa hali ya juu, dada yangu Makinda kwani ninajua kwenye Bunge hili atapambana na changamoto kubwa, hivyo anapaswa kujiandaa kikamilifu, na sasa ninarudi kuijenga upya Chadema,” alisema Marando.

Mbunge huyo wa zamani wa Jimbo la Rolya kwa tiketi ya NCCR Mageuzi kati ya mwaka 1995 hadi 2000, alisema CCM kilimfanyia fitina kwa kuwaita wabunge wake na kuwaasa wasimchague siku moja kabla ya uchaguzi.

Pia, Marando aliwahi kuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki.

“Jana (juzi) watu wa CCM waliitisha kikao cha nguvu na kusema ni lazima kuchagua chama, sio uwezo wa mtu hali ambayo iliwafanya wabunge wengi kushindwa kunipigia kura japokuwa waliamini kabisa kuwa nina uwezo mzuri tu wa kuongoza bunge zaidi ya Makinda,” alisema.

Alisema iwapo Mungu akijalia, mwaka 2015 Chadema kitaingia na nguvu kubwa zaidi kwenye bunge hilo, ingawa alitahadharisha kuwa kinachotakiwa ni kujipanga, vinginevyo wanaweza kupoteza zaidi.

Wakati huohuo, jana katika ukumbi wa bunge palitokea kioja wakati wagombea wakiomba kura, Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, alihaha ukumbi mzima kutafuta kipaza sauti cha kutumia kuuliza swali.
Ole Sendeka alipewa nafasi na msimamizi wa uchaguzi huo, Anna Abdallah, kuuliza swali lakini kipaza sauti cha mezani kwake kiligoma kuwaka ndipo alipoanza kuhaha ukumbi mzima.

Hata hivyo, licha ya kuhaha ukumbi mzima alishindwa kutimiza azma yake, baada ya Abdallah kumweleza kuwa swali hali halikustahili kumuulizwa.