Thursday, November 18, 2010

WABUNGE WA CHADEMA NA KUAPISHWA MIZENGO PINDA.

CHADEMA hawatahudhuria hafla ya kumwapisha Mh. Pinda na pia hawatahudhuria hotuba ya Jakaya Kikwete.

Ufafanuzi zaidi umetolewa kuwa CHADEMA haijatamka kuwa haimtambui Kikwete kama Rais wa Tanzania bali HAWAYATAMBUI MATOKEO YA UCHAGUZI YALIYOMPA KIKWETE MAMLAKA YA KUWA RAIS. Kwa tafsiri rahisi ni kuwa Kikwete hana tofauti na wale marais wanaotumia mbinu mbalimbali kuupata urais bila ridhaa ya wananchi wanaowaongeza, amewekwa madarakani na tume ya uchaguzi lakini siyo wapiga kura.

CHADEMA haiongelei matokeo ya kura za ubunge kwa vile sheria inaruhusu kuhoji matokeo ya ubunge kwenye vyombo vya kisheria, kwa hiyo CHADEMA inategemea kuhoji matokeo ya kura za ubunge katika majimbo kadhaa. Kwa upande wa Urais ni tofauti kwa vile sheria hairuhusu kuhoji matokeo ya Urais mara tume ya uchaguzi ikishayatangaza. Kwa hiyo jitihada pekee inayoweza kutumika ni ya kisiasa.

CHADEMA hawatahudhuria matukio yote mawili kama njia mojawapo ya kuonesha kutokuridhika na kile kilichofanywa na tume ya uchaguzi ya kuhujumu demokrasia.

WABUNGE WA CHADEMA NA KUAPISHWA MIZENGO PINDA.

0 comments:

Post a Comment